Wimbo wa Bahati Bukuku ''DUNIA HAINA HURUMA''

Wimbo wa Bahati Bukuku ''DUNIA HAINA HURUMA''

Kaka umenena kweli mi huwa naongezea kusikiliza na za rebbeca, kweli waimbaji wa bongo gospel hakuna wanalofanya, mwingine kaimba shetani na mama mkwe wamekalia misumari

Mi siwachukulii kama wasanii wa nyimbo za anjili bali wajasiriamali.
 
Daud alipopokea sanduku la bwana yerusalem alichezaje??nguo zilimfanyaje??je aliyemdharau daud kwa kucheza kma chizi mbele za bwana alifanywaje?? Furaha iliyopitiliza ina mpangilio maalum kuionyesha???
 
Huu wimbo Bahati alitakiwa auite hadithi ya kutunga,hakuna injili yoyote zaidi ya hadithi
ya kubuni,tena isiyo na utunzi stadi'
 
Mi siwachukulii kama wasanii wa nyimbo za anjili bali wajasiriamali.

Waimbaji wengi wa nyimbo za injili Tanzania hawajui kuwa wanahubiri kwa njia ya kuimba,bali
wanajua wanaimba ili watoke kimaisha matokeo yake nyimbo zao hazina faida kwa ufalme wa Mungu
zaidi ya burudani tu kama muziki wa kidunia' tena wakipata umaarufu kidogo,ndio kabisa'
 
Waimbaji wengi hasa wa nyimbo za injili wanaimba nyimbo kama wanawaimbia watoto wadogo maana hawazingatii uhalisia wa yale wanayoimba sasa bahati bukuku anasema ATM hazisomi tena. Katika ulimwengu huu je inawezekana ATM zote zikagoma kwa wakati mmoja? Waimbaji badilikeni jamani.
 
Daud alipopokea sanduku la bwana yerusalem alichezaje??nguo zilimfanyaje??je aliyemdharau daud kwa kucheza kma chizi mbele za bwana alifanywaje?? Furaha iliyopitiliza ina mpangilio maalum kuionyesha???

binafsi sio mkristo ila kuhusu swala la daud mavazi kumdondoka akimshangilia bwana nilikuta wakristo wawili wakibishana kuwa hata daud mavazi yalimvuka mwenzake akamjibu kuwa ishu ya daud ilitokea automatically wakati hawa wengine wanaenda training ambacho anahisi ni money maker
 
binafsi sio mkristo ila kuhusu swala la daud mavazi kumdondoka akimshangilia bwana nilikuta wakristo wawili wakibishana kuwa hata daud mavazi yalimvuka mwenzake akamjibu kuwa ishu ya daud ilitokea automatically wakati hawa wengine wanaenda training ambacho anahisi ni money maker

Maudhui ya muziki wa injili miaka hii haupeleki ujumbe ulionukuliwa kwenye vitabu vitakatifu, ila kwa kiasi kikubwa unakuta masimango zaidi, binafsi nilitegemea wangejaribu kunukuu vitabu vitakatifu vinawataka wanadamu watende nini maishani
 
ni wimbo mzuri wenye mdundo mzuri na ujumbe unaotia. simanzi lakini uliokosa uhalisia na unaitwa ni wimbo wa dini lakini kimsingi asilimia tisini haujakaa kidini bali ni hadithi ya maisha
Tuangalie uhalisia unapokosekana
1.Baaada ya kupata masaibu ya mme wake anahangaika kutafuta msaada wa mawifi na rafiki wa mumewe lakini kila mtu anakuwa na udhuru, ina maana kati ya wote hakuna hata mmoja mwenye msaada?basi kama ni hivyo una matatizo wewe
2.Anajaribu bank lakini akounti zote anakuta zina shida hivyo hawezi kutoa pesa ,,,katika dunia hii ya utandawazi ni kitu ambacho hakiwezekani na ikitokea hivyo una bonge la nuksi
3.Unafika hospitali daktari anakataa kumtibu mgonjwa kwakuwa huna pesa lakini unamiliki vogue .jamani tuwe wakweli ina maana unamiliki vogue lakini huna hata bima ya afya yenu? na hiyo ni hospital au ni kidispensari? kwakuwa hospital kubwa ya hadhi yake hawatangulizi hela bali matibabu kwanza malipo baadae
4.Daktari anakataa kuchukua gari kama bond kwakuwa inakula sana mafuta, hv unaweka bond au unampa dokta aitumie? na hicho ni kidispensari cha mtu binafsi na si hospital .hospital ya kweli ni taasisi ambayo kuna utaratibu wake hivyo huwezi kwenda kuongea na dokta kuhusu malipo
5.una miliki vogue lakini nyumbani huna hata hakiba ya laki5? au huna biashara au huna rafiki binafsi wa kuweza kumkopa ?au hujui wale wanaochukua mali na wakatoza riba ukachukua kiasi unachohitaji?

Tatizo la Bukuku ni tatizo la waimbaji wengi hawana watu mahiri wa kuhariri kazi zao wanatunga wanapeleka studio produser anaweka beat ngoma inaenda hewani matokeo yake ni kutoa sub standards



Napenda kumtetea Bahati Bukuku dhidi ya shutuma zilizotolewa dhidi yake kama ifuatavyo;

Hoja 1. Baaada ya kupata masaibu ya mme wake anahangaika kutafuta msaada wa mawifi na rafiki wa mumewe lakini kila mtu anakuwa na udhuru, ina maana kati ya wote hakuna hata mmoja mwenye msaada?basi kama ni hivyo una matatizo wewe

JIBU. Hapa anajaribu kuonesha hadhira ya watizamaji na wasikilizaji kwamba yapo madhaifu ya wanaume katika ndoa zetu na jamii inayotuzunguka wakati wa matatizo

Hoja2.Anajaribu bank lakini akounti zote anakuta zina shida hivyo hawezi kutoa pesa ,,,katika dunia hii ya utandawazi ni kitu ambacho hakiwezekani na ikitokea hivyo una bonge la nuksi

JIBU Ni kweli ilikua nuksi maana hutokea intenet zikawa hazifanyi kazi kwa wkt fulani benk zikawa zimefungwa (sikukuu)

Hoja 3.Unafika hospitali daktari anakataa kumtibu mgonjwa kwakuwa huna pesa lakini unamiliki vogue .jamani tuwe wakweli ina maana unamiliki vogue lakini huna hata bima ya afya yenu? na hiyo ni hospital au ni kidispensari? kwakuwa hospital kubwa ya hadhi yake hawatangulizi hela bali
matibabu kwanza malipo baadae

JIBU Siku ya kufa nyani miti yote huteleza. Daktari alikua na shida yake sio gari lakini hata pale Muhimbili watu wanakufa kwa kukosa fedha

Hoja 4.Daktari anakataa kuchukua gari kama bond kwakuwa inakula sana mafuta, hv unaweka bond au unampa dokta aitumie? na hicho ni kidispensari cha mtu binafsi na si hospital .hospital ya kweli ni taasisi ambayo kuna utaratibu wake hivyo huwezi kwenda kuongea na dokta kuhusu malipo

JIBU Umeshajibiwa ref Qn No.4

Hoja 5.una miliki vogue lakini nyumbani huna hata hakiba ya laki5? au huna biashara au huna rafiki binafsi wa kuweza kumkopa ?au hujui wale wanaochukua mali na wakatoza riba ukachukua kiasi unachohitaji?

JIBU Hapa anamwakilisha mama wa nyumbani (mke wa boss) wa jamii isiyothamini wake zao mbona wapo wengi tu.Alafu kuwa na Vogue sio issue labda ya mkopo?

Kwa ujumla unapaswa (kama usomavyo kitabu) kuusikiliza wimbo huu hadi mwisho ili uweze kuelewa ujumbe uliobebwa na wimbo wenyewe;

1 Uaminifu katika ndoa umepotea kwake mume, mke na daktari hivyo jamii
2 Rushwa ya ngono kwa daktari na hivyo maofisini
3 Upendo umetoweka miongoni mwetu tusaidiane wakati wa matatizo
4 Kuomba msamaha kwa uliyemkosea ili kuweka sawa mambo yako na MUNGU
5 Uwezo wa MUNGU wa kumsamehe mwanadamu
6 Tunanyoosheana vidole kati yetu "nani kati yenu hana kosa na awe wa kwanza kumtupia mawe" walitawanyika wote pasiwepo wa kumtupia mawe.NAWAKILISHA.
 
Wimbo uko poa sana aisee....ujumbe mzuri sichoki kusikiliza
 
cjui kama umesikiliza vizurihuo wimbo mwimbo ni mzuri hauna shida yoyoye maana mwisho anasema nataka kutengeneza na yesu kwahyo baada ya yote hayo amegundua hata yeye amekosea anataka kupatana na mungu hyo ndio lengo baada ya kisa upo hapo.

Kajitahidi bana .
 
cjui kama umesikiliza vizurihuo wimbo mwimbo ni mzuri hauna shida yoyoye maana mwisho anasema nataka kutengeneza na yesu kwahyo baada ya yote hayo amegundua hata yeye amekosea anataka kupatana na mungu hyo ndio lengo baada ya kisa upo hapo.

Cdhani km umemuelewa mleta mada! Kutokana na Msg ya WMBO inaonyesha hana ndg wala Rafiki wakweli wakumsaidia inawezekana kwenye maisha yetu haya yakiswahili? mi ndhani wa2 wako kiBZ zaidi!
 
haiwezekani kila unaemfata akutose eti hadi marafiki wa karibu manake we unaishi dunia gani sasa ya kukosa hata laki 5 kwa personality aliyoigiza nayo kwenye vid haiwezekan

hujawahi kupata shida ww ndi6 maana unaropoka!
 
Wasanii wa bongo kuanzia BONGO MOVIES, BONGO FLEVA, GOSPEL.. Wengi wao hawana uhalisia. At least Hip hop huwa kuna maneno yenye kuleta maana kiasi.
 
ukifikiria kidogo utapata kidogo.ule ni wimbo wenye lengo la kutoa ujumbe kwa jamii.alikuwa anajaribu kuwa kioo cha yatendekayo ndani ya jamii zetu.katika kuchambua kazi kama hii ya fasihi jaribu kuangalia mawazo makuu ya mtunzi.nadhani analysis uliyoifanya hapo juu imeshatupa jibu kuwa kipo kilichosemwa ndani ya wimbo.kumbuka bahati anaisemea jamii ya watu milioni 45 kwa kutumia mtu mmoja.matatizo yaliyotajwa yaweza yasimkumbe mtu mmoja ila ukweli tunafahamu kuwa wapo wanaokataliwa na mawifi zao,benki huwa zinashindwa kufanya kazi muda mwingine tena sababu yaweza kuwa mtandao tu,ni hospital ngapi hushindwa kuhudumia watu kwa kuwa hawajatanguliza pesa..........

fasihi huisemea jamii kuichambua yahitaji uitazame jamiii yenyewe
 
mi siku ya kwanza nilidhani ni wimbo mpya wa DK REMMY ONGALA maana ndio alikuwa na hadithi za kuchanganya amdesa kama huyo bukuku eti itm hazisomi zote
 
mi siku ya kwanza nilidhani ni wimbo mpya wa DK REMMY ONGALA maana ndio alikuwa na hadithi za kuchanganya amdesa kama huyo bukuku eti itm hazisomi zote

Hujawahi kuona?? Waulize watu wa akiba commercial bank leo na jana ilikuwaje
 
huu wimbo haujakaa kidini,umekaa kibongo fleva au taarabu

Wengi hamjaelewa lengo la wimbo.mlitaka alitaje jina la mungu kila line? Au mlitaka atumie vinanda vya kanisa? Ameonyesha jinsi gani dunia haina huruma.........unapoongelea bongo fleva ama taarabu hapo unaongelea mapigo ya ala yalivyopangika.south African Gospel yaweza isifanane na ya Tanzania ukiisikia utasema siyo nyimbo ya dini??? America kuna rap Gospel doesn't matter what kind of music but the message
 
Back
Top Bottom