Wimbi la Makonda wa kike

Wimbi la Makonda wa kike

ila tatizo la hawa wadada makonda ni kujivika udume flani hivi. wawe tu wanawake kawaida
 
Wanalea saa ngapi watoto?
Waume zao wakibandua mabeki tatu wasilalamike,maana wanawaachia fursa wenyewe.

hoja yako imechoka sana mkuu. Kuhusu kulea watoto, ebu niambie wanawake wote ambao ni madaktari, walimu na wafanyakazi ktk sekta mbalimbali na wafanyabiashara watoto wao wanalea saa ngapi? Think big mazee
 
Ni upepo tu unapita...dawa yao kuwapiga mimba tu watuachie kazi zetu

Ukiona ana mimba ujue kataka kuzaa otherwise family planning zimejaa au unaishi karne ipi mwenzetu? Maana kutia mimba is nothing hata mbwa anatia acha kina mama wafanye kazi tupunguze umaskini wanaume wenyewe mmefilisika mkiombwa pesa midomo inakuwa juu kama waomba mchiriku
 
Hahhaa hii kali mana naskia wakiwaacha nyumbani wanaibiwa kweli waje zao madereva bora kutoka nae kushinda nae na kurudi nae

Na watoto? Wanawaweka siti ya mwisho?
 
halafu nimekumbuka. eti hawa watoto wa kike ni chambo kwa mtrafiki hasa wa kiume. ni kweli siku moja konda wa kike alimbananisha trafiki na baada ya muda mfupi tukaondoka
 
mmh!!Tutake radhi tafadhali

Niitake kwa lipi?unataka kuniambia ni wajane wale wote au wanaume makenge wezi wa mayai ya mamba kutaka kulelewa tu nyambafu zao ..kaulize hao mabinti asilimia kubwa wamezaa wakaachiwa watoto
 
Kwa uzoefu wangu wa ukondakta wa daladala....kazi ya ukonda ina changamoto nyingi sana ambazo zinahitaji uwe shupavu sana....na nilishawahi kufanya kazi na wanawake mlangoni lakini maumbile yao kibaolojia hayaendani na kazi....kwa mfano unaweza ukampitia mkaamshe gari anakwambia leo nipo kwenye siku zangu na tumbo linanisumbua...inabidi utafute mtu mwingine wa dharula....mara utasikia kashikwa na tumbo la chango..................yaani ni full majanga......kwa kifupi hii kazi wanawake haiwafai...........
 
Back
Top Bottom