I wish to point out kuwa header ya thread imefanyiwa editing without my consent or even consultation na one of the JF's unknown moderators
Header yangu ilikuwa : WILSON MUKAMA: Public and Private Profile
Sijaweka bado personal view kama ambavyo thread header inavyosema ila nimeweka criticism on the article ambayo MUKAMA aliandika kujisifia
Naam in continuing with our tradition ya KU RECYCLE WATAWALA this time tumeletewa huyu jamaa ambaye if anything
-Alikuwa mstari wa Mbele kuwatisha Madaktari walipogoma Muhimbili. By then alikuwa ni Permanent Secretary wizara ya afya. Badala ya kutafuta njia ya maana ya kutatua ule mgogoro he was busy devising brutal methods za kuuzima ule mgomo badala ya kuangalia njia mbadala.
-Alipokuwa Mkurugenzi wa jiji la Dar hakuna lolote la maana alilolifanya ambalo tunaweza kusema kuwa lili kuwa ni major achievement zaidi ya kuwa the City was more dirtier, unsafe and disorganised than ever. Traffic police wakapewa kazi za kudumu kuongoza magari badala ya kutengeneza taa za kuongeza magari. Waliofanya naye kazi kule jiji wanasema kuwa huyu bwana if anything ali alienated a lot of people (direct and indirect) not necessarily with his policies, but with his undisguised belief kama alivyokuwa Keenja that Dar belonged to him. Bwana Mukama alisahau kuwa he was there to serve wana Dar lakini instead treated jiji like his fiefdom.
Mtakaosema kuwa namwonea lakini lets face it yeye mwenyewe aliwahi kusema hivi alipokuwa City Director:
"I want to see a much more livable Dares Salaam -- in terms of security, of course, but especially in terms of affordability".....a much more planned Dares Salaam" would eventually lead to "a much more manageable", "much cleaner" and "much safer" city.
The truth ni kuwa what we got from him was the opposite
Na kwa kuonyesha kuwa he is out of touch hebu soma solution yake kuhusu vijana wanaotafuta rizki Dar:
"of course, we have to address the causes underlying rural problems. We have to encourage the youth to stay in the rural areas so that there is less migration to Dares Salaam. But that means that there must be viable economic activities to sustain them there--cash crops, good living conditions and availability of services, for which they normally come to town, such as education, health and the provision of safe water. The temptation to move will ease if these services are made available within our rural areas and if the people there have some gainful economic activities--they produce their crops and they sell them.
Typical response from out of touch City Director ambaye kasahau kuwa its basic human right ya Mtanzania kuishi kokote kule atakako Tanzania without interference from people like MUKAMA.
Anazungumzia kupeleka huduma vijijini lakini nani kamwambia kuwa kila kijana anataka kuishi kijijini? au kila kijana anataka kuwa mkulima? dont worry, haya ndio mawazo na mentality ya MUKAMA juu ya vijana ...wakae vijijini wawe wakulima. Cha ajabu wanawe hawaishi vijijini.
MUKAMA THE RACIST:
Showing out of touch na jiji la Dar Mukama anaendelea kuwatuhumu vijana toka mikoa ya kusini kujaza jiji la Dar bila any supporting data or any facts kwa kudai kuwa:
"Most of these young men, who peddle goods on the road, are from the South."
really? Kama anazungumzia Immigration caps to Dar why single out vijana from Kusini?
MUKAMA THE OUT OF TOUCH:
Huyu bwana anajisifia alivyotumia pesa za walipa kodi kwenda kwenye mikutano ya kimatafaifa kwa kusema hivi:
In my one year as City Director of the City Council of Dar es Salaam, I have benefited from attending a number of international conferences. Some of the best practices discussed at these conferences have contributed immensely to my understanding of the ways local authorities around the world are getting the people involved, especially in the area of governance.
Ukweli ni kuwa local authorities Dar chini yake hazikuwa involved kwenye chohcote kile. Mfano chini yake leseni za Bar zimetolewa kama uyoga bila kuzingatia sheria za serikali za mitaa ( msisahau alishawahi kuwa TAMISEMI) ambazo ziko very strict on eneo la mraba na time ambazo hizi bar zinatakiwa kufunguliwa. Maoni ya wananchi waliopo eneo lile, issues za afya na biala kusahau wagonjwa na watoto..mfano mzuri chini ya uongozi wake eneo lilalo zunguka hospitali za Mwananyamala na Ilala zimekuwa na Baaa nyingi ambazo zinapiga makelele za miziki mpaka saa 9 usiku bila kuzingatia wagonjwa na watoto ambao wanatakiwa kwenda kusoma kesho yake.
Sasa whats the point of kujisifia kwenda kusoma halafu kakuna faida ya hiyo misafara?
KUHUSU DAR
Mukama the Walter Mitty Character anasema hivi:
"I want to see a much more livable Dar es Salaam--in terms of security, of course, but especially in terms of affordability. A city, in other words, where people have a good income and can afford to pay for the various services available to them--housing, transport, recreation areas. We plan to carry out an urban renewal in some areas, because if we don't have enough open spaces, our city won't be able to breathe and will choke. We are attempting to make our beaches safe and clean so that people can relax there. They should not just always spend their free time inside their houses because they have no better choice. We need more open spaces, with more gardens, recreational parks."
Sina haja ya kusema mengi kuhusu hili kwani kila mtu anajua what we got in return.
Baadae ntarudi na mengine
Lakini in short this is another incompetent propagandist aliyeteuliwa ambaye hana jipya...infact amekuwa RECYCLED like the other lot
source ya majisifa aliyojipa Mukama iko hapa:
'A Much More Livable Dar Es Salaam': Sustainable Urban Development. Magazine Title: UN Chronicle. Volume: 38. Issue: 1. Publication Date: March-May 2001. Page Number: 24+. COPYRIGHT 2001 United Nations Publications
Umejitahid ku-quote mengi na mazuri ya Bwana Mkama.Wasi wasi wangu ni uelewa wako mdogo juu ya uwezo na nafasi aliyokuwa nayo Bwana Mkama.Kwa yote nadhani alipaswa kuchangia katika utekelezaji na ni kitu alichokifanya.Kumbuka kuwa hakuna anayesifika katika good reform ya jiji la Dar es Salaam zaidi yake na hicho ndicho kilichompandisha hadi hapo na si Ukada.Tuhuma ama criticisms zako zote zimelenga as if Mkama alikuwa Waziri Mkuu ama Rais wa nchi ambaye anauwezo wa kuinfluence policy at any time.Kuwa Mkurugenzi wa Jiji si sababu ya wewe kufanya miujiza labda ingekuwa Serikali ya Majimbo kama USA.
Hoja zake ni za Msingi,tambua tatizo kubwa la mobility hasa from rural to urban ni hali ngumu ya kimaisha huko vijijini.Hali ikiboreshwa vijiji hugeuka kuwa miji na majiji.Tazama Dar es Salaam miaka ya nyuma(Ukoloni),ilikuwa kama baadhi ya vijiji vilivyopo leo na utambue kuwa hakuna mji unaokuwa bila kuchipukia katika hatua ya kijiji.Mkama was right na mtu mwenye maono ya utaifa mbele kama yeye hatunabudi kumuunga mkono na kuacha itikadi uchwara zenye hoja za majitaka.Nashangaa mazuri una-quote lakini ufafanuzi wako juu ya ulicho-quote ni incapability to judgement.
Nashukuru umekuja na hii hoja hapa,nenda kasome tena vizuri na utambue kuwa mtu anaowafikiria watanzania walioko vijijini na namna ya kuwafanya nao wajisikie kama wewe ulieko Dar ama kwingineko mjini si wa kubezwa hata kidogo.Shule ama Chuo au Supermarket si lazima Mjini kama unavyodhani,vyote vinawezekana vijijini.Kumbuka hakutamka kuwa wasomi ama ambao wanakwenda mijini kwa masomo,wafanyabiashara au watumishi wasiamishiwe mijini ama kukimbilia mijini hasa Dar ila wale wasioridhika na maisha ya shamba yasiyokuwa na muelekeo hasa jembe la mkono na kilimo cha kutegemea mvua tu,na hatimaye kuona unafuu kuwa mjini kama Machinga Kariakoo na kwingineko.Hili ndilo tatizo kubwa.Aidha amekuwa katibu mkuu ama bado ni Mwanachama sasa anapaswa kushauri chama kwa uwazi jinsi ya kutekeleza hayo kitaalam na kusaidia vijana tusichoke na maisha ya vijijini.
Tazama wewe,ukija Dar es Salaa maadam Mungu kakutunuku uwezo wa kifedha kama si shetani kukupa ufisadi wengi wetu upenda kujenga nyumba ata tano Mjini.Hutaki kurudi kijijini na kujenga ama kufungua ata mradi mdogo unaoendana na hali ya uchumi wa kijiji kisa Utalogwa!!!!!!!!!!Sasa elewewa ni sisi wasomi,wafanyabiashara na Wafanyakazi ndio tunaweza kuvibadilisha hivyo vijiji na kuvifanya sehemu nzuri ya kukalika kwa wazazi wetu na jamii zetu zilizopo huko."Nchi itajengwa na Wananchi wenyewe".
Nashukuru kwa kuileta mada hii,umenifungua kichwa kutambua ni jinsi gani wasomi tunavyopotosha jamii kwa itikadi za vyama ama ushabiki uliotukuka.Lakini elewa kuwa hakuna kiongozi asiyelaumiwa hasa yule ambaye anajikuta akipendwa na watu hasa katika kipindi cha KAMPENI.Wananchi huwa na matarajio makubwa ambayo yeye kwa tamaa ya madaraka hujifanya kuyabeba hata yanayokuwa nje ya uwezo.Hili ni funzo kwa kikwete na hata atakayekuja.Mkapa hakukubalika sana na watu lakini leo hii tunasema angalau alifanya kitu.Tuwe makini kwa kuwapima hawa viongozi na kuona nini wamekifanikisha sio kwa wizi ila kwa bidii zao kuanzia nyumbani(familia) hadi nje kwa maana ya Watanzania.
Tunasema si vizuri kuingilia maisha ya mtu binafsi lakini historia mbaya ama nzuri za viongozi wetu,nyingi zinaakisi tabia zao za kuzaliwa hasa suala la UBINAFSI.Wengi wanaoanguka utakuta hata tabia zao za kuzaliwa kwa maana ya nyumbani au utotoni zinachangia.Ukiwa mchochezi,mwenyetamaa,mwizi,ubinafsi,chuki ama chochote kisichokubalika na Mungu katika maisha ya utoto ama kifamilia,sidhani kuwa miujiza ya kupata uongozi itakubadili na kuwa mtakatifu.Kwa hili ni wachache ambao hutokewa na hekima hizo.
Tazama kunamgombea mmoja wa U-Rais,pamoja na kuwa mbunge na kiongozi wa taasisi mbalimbali zisizo kuwa za kiserikali wala kisiasa.Mtu huyu na imani huko kote hakuwa anajitolea ila kuna kipato alichokuwa akipata japo kinaweza kuwa kidogo ama kikubwa.Sote tunafahamu Bungeni kulivyo patamu kimapato.Mtu huyu katika mbio za U-rais kama unavyojua siasa,vyombo vya habari vikawahi kijijini kwa Mzee kuona anamaono gani kwa Mwanaye.Inasikitisha,inatia huruma na haistaili kusimuliwa HIVI kweli Mzee pamoja na kuteseka kwake juu yako bado anaishi na Mbuzi ndani?nyumba duni,chakula duni,mavazi duni eti kisa yuko kijijini.Ni AIBU kubwa sana kwa huyu ambaye tunaamini anakipato cha kutosha hakumtendea heli Mzazi wake ili aendelee kumbariki!je ataweza kwa Watanzania kila mmoja kuisha nyumba bora?
Wasalaaaaaaaaaaaaaaaaaaam.