Will you marry a jobless man? Toa maoni yako

Will you marry a jobless man? Toa maoni yako

Adam aliumbiwa Hawa kama msaidizi wa kufanana naye na hii haimanishi kwamba Adam alitakiwa kufanya kila kitu kwasababu tu Hawa ni msaidizi.

Unataka kusema kuwa “mume” ni kuwa na kazi/pesa? Kwamba yeyote mwenye kazi/pesa tayari ana sifa za kuwa “ mume”? Kama hii ndio sifa ya kuwa mume babu/baba zetu wasingeoa hakika na pengine tusingekuwepo duniani.

Mke akinihudumia kwa kila kitu sio mbaya ndiyo maana halisi ya ndoa inapojidhihirisha (kwenye shida na raha). Au mwenzangu unaitafsiri vipi ndoa? Kwamba ni mwanaume tu ndiye anayetakiwa kumhudumia mke kwa kila kitu?

Kuhusu mahari haina shida mwanaume yeyote anayeamua “kuoa” mahari atapambana kwa namna yeyote aipate regardless ni jobless.

Nashukuru kwa kukubali mafanikio ya mwanaume yeyote yule huchagizwa na mama yake.
Sasa tunaenda sawa, sifa ya kwanza ya mwanaume ni kuwa "provider". Then mambo mengine yanafuata, hivyo si kwamba ukiwa na kazi basi umemaliza bali kuna mengine ya muhimu yanaambatana na hilo.

Babu zetu hawakuoa ilimradi wanaoa, walioa kwasababu walikuwa wapo "tayari" kuoa. Huo utayari ni jambo pana sana ndio na hiyo "kazi" inaingia hapo.

Kama ambavyo unapambana kwa hali na mali ili uweze kupata mahari basi upambane pia uwe na kazi ndio uoe. Maana mahari ni part ndogo mno ya responsibility ya mume katika ndoa.
 
Kwa kipindi hiki cha JPM ule msemo wa "Hujafa hujaumbika" una apply sana. Leo utasema No kwa jobless na Yes kwa employed man ila huyo employed keshokutwa na yeye anakua jobless man with experience
 
Sasa tunaenda sawa, sifa ya kwanza ya mwanaume ni kuwa "provider". Then mambo mengine yanafuata, hivyo si kwamba ukiwa na kazi basi umemaliza bali kuna mengine ya muhimu yanaambatana na hilo.

Babu zetu hawakuoa ilimradi wanaoa, walioa kwasababu walikuwa wapo "tayari" kuoa. Huo utayari ni jambo pana sana ndio na hiyo "kazi" inaingia hapo.

Kama ambavyo unapambana kwa hali na mali ili uweze kupata mahari basi upambane pia uwe na kazi ndio uoe. Maana mahari ni part ndogo mno ya responsibility ya mume katika ndoa.
Kuwa “provider” haimaanishi kuwa na kazi! Wapo waume ambao hawana kazi na bado wanazihudumia familia zao vizuri zaidi ya hao wenye kazi.

Nikupe mfano hai mmoja tu wa mababu zetu. Katika kabila la wasukuma miaka ya nyuma huko mtoto wa kiume alipofikisha umri wa “kuoa” baba yake alimlipia mahari ng’ombe si chini ya thelathini kutegemea na wasifu wa binti. Kijana alioa na kuishi na mke wake katika wigo wa baba yake huku baba/wazazi wakimhudumia kijana na mke wake karibu kwa kila kitu.
Wahenga wakisukuma wapo hapa naomba watoe ushuhuda kwenye hili.

Jaribu kubadili “mindset " yako kama utaendelea kufikiri kwa namna unayofikiri sasa “mfumo dume” kamwe hautoisha. Kwasababu ninyi wanawake ndiyo mnaouchochea kuanzia “kifikra” mpaka “kiuchumi” na bado mmekuwa mkilalamika kuwa wahanga wa huu “ mfumo dume”.
 
Kuwa “provider” haimaanishi kuwa na kazi! Wapo waume ambao hawana kazi na bado wanazihudumia familia zao vizuri zaidi ya hao wenye kazi.

Nikupe mfano hai mmoja tu wa mababu zetu. Katika kabila la wasukuma miaka ya nyuma huko mtoto wa kiume alipofikisha umri wa “kuoa” baba yake alimlipia mahari ng’ombe si chini ya thelathini kutegemea na wasifu wa binti. Kijana alioa na kuishi na mke wake katika wigo wa baba yake huku baba/wazazi wakimhudumia kijana na mke wake karibu kwa kila kitu.
Wahenga wakisukuma wapo hapa naomba watoe ushuhuda kwenye hili.

Jaribu kubadili “mindset " yako kama utaendelea kufikiri kwa namna unayofikiri sasa “mfumo dume” kamwe hautoisha. Kwasababu ninyi wanawake ndiyo mnaouchochea kuanzia “kifikra” mpaka “kiuchumi” na bado mmekuwa mkilalamika kuwa wahanga wa huu “ mfumo dume”.
Hahahaaaaa!! Mkisikia kutimiza majukumu yenu ndio mnakumbuka mfumo dume!! Funy!!

Naomba tu utambue kuwa kuna mambo hayahusiani na mfumo dume wala jike. Its nature, mwanaume ana wajibu wake na mke pia. Kuhudumia familia ni jukumu la mume hilo na ni sharti uwe na kazi. Hata huyo alokuwa anaolewa mke si kuwa alikuwa kajibweteka tu akisubiri kula na kulala. Walifuga na walilima pia. Hivo jambo unaloongelea wewe ni zilipendwa za wahenga.

Hauwezi kuihudumia familia kama hauna kazi, unless urudi zama za ujima za baba anakuolea mke kisha anakutunza wewe na familia yako(ni kama vile mmeolewa wote) na mume wa hivyo simtaki jamani. Abakie tu huko kwao aendelee kulelewa.

Baada ya kusema hayo, nikutakie usiku mwema kama ulipo pia ni usiku.
 
Lilijuwa munaoishi fake life lazima mguswe tu

Espy usijari mumy kama nipesa niko vizuri karibu Kigoma
 
Sisi wa NGUMBALU umetuacha,siku nyingine andika lugha yetu tuchajngie kwa kujiachiea
 
Siku nyingine uje na uzi unaosema " Will you marry a jobless woman?"

Hivi kama manufaa ya kipato ni kuweza kutimiza mahitaji ya msingi katika familia,kwa nini ionekane haramu kipato cha mwanamke kutimiza hayo mahitaji ikiwa mumewe hana? Kuna sababu gani ya mwanawake kuajiriwa na kulipwa mishaara? Unakuta mwanamke ameajiriwa ana mshaara mkubwa lakini anatafuta mume mwenye kazi na yenye mshaara wa kutosha kutimiza mahitaji yake sasa hizo pesa anazopata kama mshaara hazina kazi sasa. Wakati mwanaume mwenye kazi anaoa mwanamke asiye na kazi na wanaishi kwa mshaara huo. Hili suala ni la kuangalia kwa jicho la tatu kuna upotevu wa pesa.
 
Nakufahamu espy ww ni mbishi sana, ila atleast umepata somo kidogo.
 
Nakufahamu espy ww ni mbishi sana, ila atleast umepata somo kidogo.
Yes nimepata somo kuwa mwanaume lazima awe na kazi ndio aoe, kama hauna usifikirie hata kuwa na girlfriend.
 
Mbona hueleweki!!! Si ungeandika kichwa cha habari kwa kingereza au!!!!
 
Yes nimepata somo kuwa mwanaume lazima awe na kazi ndio aoe, kama hauna usifikirie hata kuwa na girlfriend.
No wonder wanawake wenye mtizamo kama wako huwa tunawachukulia kama “malaya” mnatofautiana kwenye formalities za kuuza tu, kwamba wengine wanasimama kabisa barabarani na wengine wanauza indirect way kama hii unayoitetea ww.
 
No wonder wanawake wenye mtizamo kama wako huwa tunawachukulia kama “malaya” mnatofautiana kwenye formalities za kuuza tu, kwamba wengine wanasimama kabisa barabarani na wengine wanauza indirect way kama hii unayoitetea ww.
Haya.
 
How would it be possible for a sound minded man to be jobless without a reasonable cause...
 
Hebu soma mada kwanza uielewe, mada inaongelea jobless au mwenye kipato kidogo?
Wahenga walisema "kuzaliwa ktk familia masikini sio kosa lako bali kuolewa na mume masikini ni kosa lako mwenyewe".
Sio maneno yangu ni ya wahenga hayo.
Chukulia mfano mtu ambaye mnafahamiana vizuri na mnapendana sana vilevile unajua kabisa anatoka katika familia ya kipato cha chini kabisa. Muda wake mwingi ametumia kusoma tuchukue katumia miaka msingi kusoma tuseme miaka 18 primary hadi chuo. Na anafanya kazi hizi za pata potea(hana kazi specific) . sasa hapo huwezi kukubali akuchukue muwe pamoja kama mume na mke?
 
Back
Top Bottom