Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro inakufa

Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro inakufa

kwenye suala la maendeleo Rombo imezipita Wilaya nyingi tu apa Tanzania. Labda mleta uzi wewe unapima maendeleo kwa kuangalia idadi ya wanywa soda
Unachosema ni kweli ila kwa hali ya hewa na rutuba iliyoko haistahili kuwa hivyo, fananisha na jirani yao Marangu uone tofauti iliyopo japo nayo siku hizi vijana wamejiingiza kwenye ulevi hawataki kazi.
 
kwenye suala la maendeleo Rombo imezipita Wilaya nyingi tu apa Tanzania. Labda mleta uzi wewe unapima maendeleo kwa kuangalia idadi ya wanywa soda
Hamna hata mmoja anaweza leta picha ya sehemu nzuri zaidi hapo Rombo??
 
Wilaya yako je ni ipi ili tulinganishe na Rombo jamani.
Isije ikawa Ile kauli ya " bia moja ni tofali mbili, Sasa wewe ambaye haunywi unazo tofali ngapi"
Mada hii hailinganishi wilaya na wilaya isipokuwa ni kuitaka serikali iisaidie wilaya ya Rombo iondokane na balaa la unywaji pombe.
 
Rombo iko nyuma sana kimaendeleo??Hivi kuna watu wamejenga kwao kama Warombo?..Kwa standard yetu duni ya Tz,Rombo iko vizuri.

Umeme upo long time tu huko..hata barabara nyingi zinapitika fresh..watu wamejenga pia sana.

Hii Tanzania yetu duni ni Wilaya chache tu ambazo zitalingana na Rombo kwa unafuu..(tukitoa wilaya lizilobeba mji wa Mkoa)

Pombe ni kweli zinanyweka vibaya mno..serikali iingilie hizi pombe kali za bei rahisi rahisi zidhibitiwe.
 
Hamna hata mmoja anaweza leta picha ya sehemu nzuri zaidi hapo Rombo??
Bahati mbaya haukuona kipindi cha Uchunguzi Kamili kilichorushwa na ITV jana Alhamisi saa 3:30 mpaka 4:300 usiku, usingeamini kinachoendelea Rombo, wanawake wanawalalamikia waume zao na vijana wamechakaa kiasi hawajulikani kama ni watoto au wakubwa, walimu wanalalamika utoro shuleni na makanisa yako hoi waumini wako kwenye pombe!
 
Nimewahi kuitembelea wilaya ya Rombo mkoa wa Kilimanjaro nilichokiona huko kinatisha, Rombo ni wilaya ambayo iko nyuma sana kimaendeleo na watu wake hawana habari yoyote ya maendeleo zaidi ya kunywa pombe!

Pombe, pombe, pombe hakuna cha mzee au mtoto hata mwanafunzi! Shule zinakosa wanafunzi kiasi cha kufikia kuunganisha shule au madarasa! Rombo hakuna makaburi! Utashangaa kuona mafuvu ya watu kwenye migomba! Ni kitu cha kawaida sana.

Nirudi kwenye ulevi, pombe nyingi za chupa zinazotengenezwa majumbani huuzwa shilingi mia tano tu na ni kali sana! Wazee kwa watoto wanazinywa sana kuanzia asubuhi mpaka usiku hakuna kufanyakazi na watu wazima wanaume nao majukumu ya kuendeleza kizazi kinawapiga chenga kiasi cha kuwafanya wake zao watafute mamluki wa kutekeleza jukumu ya kuendeleza kizazi.

Serikali iwasaidiaje, serikali iwaelimishe madhara ya pombe pamoja na kidhibiti viwanda bubu vya pombe. Nini mbadala wa pombe, serikali iwafundishe kilimo cha miparachichi ya muda mfupi tofauti na waliyonayo, ardhi ya Rombo ni nzuri kwa miparachichi.

Watalimaje, iwaweke kwenye vikundi vidogo vidogo ambavyo vitakuwa rahisi kudhibitiwa.

Ninaamini wazazi wanaume wakidhibitiwa kwenye ulevi watoto ni wazi hawatafurukuta watarudi shule.

Serikali ione kinachoendelea Rombo ambacho kimeanza kuiambukiza Marangu ni janga la taifa.
Una makasiriko, kutoka wapi [emoji1][emoji1][emoji1]

Kunywa maji moyo ueleee, Rombo ni Next level
 
Ukikuta watu wanakusema wewe jiambie mimi ni jembe na endelea kuchapa kazi. Ukianza kutafuta umbea nawe utakuwa ni mmoja wa wambea.
Hakika, wivu tuu unampeleka jamaa pabaya
 
Baada ya Mods kushindwa kuihamishia Post hii kwenda kwenye siasa, naona Post imepoteza lengo kwa walengwa hivyo nafikiria kuifuta.
 
Back
Top Bottom