Wiki ya Sheria: Rais Magufuli awabadilikia Waziri Kabudi, AG Masaju na DPP kwa kukwamisha haki kutendeka

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,968
141,976
Karibu ufuatilie matangazo hayo mubashara kupitia luninga ya ITV! Kwa hotuba ya leo kuna kila dalili ya mtu fulani kutumbuliwa soon!


=====

UPDATES

JAJI MKUU
Wananchi wa Tanzania, watarajie huduma bora za uendeshaji wa kesi, uwazi na huona hukumu kwani Tehama itarahisisha yote haya na sisi majaji, mahakimu na watendaji wa Mahakama tubadili fikiri zetu na kuijua Tehama kwani karne hii inahitaji kwenda na wakati

Utaratibu unafanyika ili kukamilisha mfumo wa menejimenti za kesi ambayo itatumika kulipa ada, uendeshaji wa kesi kwa masafa ya mbali.

Idadi ya majaji waliopo hayaendani na majalada wanayopewa kuyasikiliza kwani majaji waliopo ni 62 pekee na kila mwaka wanabeba majalada 535 badala ya 225 wanayopaswa kuyasikiliza.

Huu ni mzigo mkubwa sana na iko nje ya makubaliano kwamba kila jaji amalize majalada 225 lakini kwa idadi hii ni mzigo mkubwa sana

Mpaka sasa ni mikoa 14 kati 26 pekee ndizo zenye Mahakama Kuu ambapo malengo ni kuwa na Mahakama Kuu katika mikoa 22 ifikapo mwaka 2020. Malengo ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2020 wilaya zote 139 za Tanzania bara zinakuwa na Mahakama za wilaya.

Hatutamwonea mtumishi lakini hatutamvumilia mtu anayetupaka matope sisi kama Mahakama

MAKAMU WA RAIS TLS

Matarajio yake (Rais Magufuli) hayafiki kwetu sisi na kwa maoni yangu matarajio ya kiongozi wangu huyu yanaakisi matarajio ya wananchi

Mahakama inafaa kuwa mahali iliyotukuka kwani ni mahali pekee tunapokuwa na migogoro, pale tunapoililia sheria tunakwenda mahamakani na hii haijalishi aina ya mtu.

Tusiitumie Mahakama kama majaribio, maabara au jumba la kamari. Majaji msiitumie hata Mara moja kwani mnalindwa kisheria na msimamie hilo ili Mahakama isionekane ya ajabu ajabu


RAIS MAGUFULI

Kwa kuadhimisha siku hii ya sheria maana yake ni kwamba nchi yetu inatambua umuhimu wa sheria katika kusimamia haki, kudumisha amani na kuleta maendeleo ya nchi

Maadhimisho haya ya siku ya sheria ni muhimu kwa vile yanatoa fursa kwa vyombo vinavyohusika na masuala ya sheria na utoaji haki, yani Mahakama, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jeshi la polisi, Magereza, TAKUKURU, Mwendesha Mashtaka wa Serikali na Mawakili.

Napenda kutumia fursa hii kuvipongeza vyombo vyote vinavyohusika na masuala ya sheria na haki nchini, kwa kazi kubwa ya kusimamia sheria na kutoa haki kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita

Naipongeza Mahakama ya Tanzania kwa kazi kubwa na nzuri iliyofanya ya kutoa haki, lakini katika hotuba yangu mbele huko nitatoa changamoto lakini nimeanza kuipongeza kwanza, kwahiyo yale yatakayokuja ni changamoto tu

Ucheleweshaji wa kesi umefanya baadhi ya makampuni zikiwemo benki kufirisika hii ni moja ya sababu zinazofanya riba za benki zetu kuwa juu.

Pamoja na pongezi nilizozitoa kwenu hivi punde, jambo moja lipo dhahiri kwamba usimamizi wa sheria na mfumo wa utoaji haki nchini bado unakabiliwa na matatizo mengi, na moja ya matatizo hayo ni kupungua kwa uadilifu kwa watumishi wachache wa vyombo vyetu

Utafiti uliofanywa na Taasisi ya Twaweza hivi karibuni umeonesha kiwango cha rushwa kimepungua kwa 85%, ikilinganishwa na miaka 5 iliyopita huku Polisi na Mahakama zikiongoza kupokea rushwa, tunaweza tukawa hatuutaki utafiti, lakini hatuwezi kupuuzia.

Kwa vile nafahamu kuwa watumishi wengi wa vyombo hivi ni wazuri na waadilifu lakini hawa wachache hatupaswi kuwaacha kwa vile matendo yao yanavichafua sana vyombo vyetu, hawa ndio wanaodai rushwa, kuwabambikiza kesi wananchi, wanachelewesha upelelezi

Mimi nina uwezo wa kusema hadharani sababu nilipewa jukumu hilo na watanzania,mimi nimeumbwa kusema ukweli na hiyo ndio tabia yangu na sitaibadilisha unipige ,uniweke kwenye shimo, univuruge nikitoka nitasema ukweli.

Kinachoshangaza pamoja na hatua nzuri ya Serikali kupeleka 'Legal Aid Act' ya mwaka 2017 na mapendekezo mbalimbali kwa ajili ya kuwasaidia wananchi lakini 'regulation' mpaka saizi hazijaletwa ila Waziri yupo tena Mwanasheria, tena ni Profesa, AG yupo, Deputy AG yupo

Jamani mtanisamehe sana mimi ndivyo nilivyo nawasema hapa hapa kwa hiyo wewe Profesa Juma na majaji na mahakimu hamna 'Instrument' za kuweza kutoa uamuzi. Wabunge wao wamepitisha sheria, mimi nikaletewa nikasaini lakini regulations mpaka leo miezi tisa imepita

Watu wapo wanakula tu mishahara, magari wanayo na viyoyozi vipo ila wananchi wanapata shida na muda mwingine mtasingiziwa mahakama kwamba hamtoi haki kumbe ni Serikali watendaji wake hawatoi haki kwa Watanzania,

Ndiyo maana nawaambia changamoto zingine zipo ndani ya Serikali lazima na mimi nijitathimini ninachaguaje hawa watu ambao wanachelewesha chelewesha, hiyo ndiyo tathimini ambayo ninaanza kujifanyia kuanzia leo.

Bado kuna tatizo kubwa ofisi ya DPP (Mkurugenzi wa Mashtaka) na AG (Mwanasheria Mkuu), panakuwa na ushahidi na nyie Majaji mnaona lakini hakuna wa kuutetea. Mwaka jana nililamika, mwaka huu nitalishughulikia, tena kabla ya Februari hii kuisha

Naipongeza sana tume ya utumishi wa Mahakama ambayo ipo chini ya Jaji Mkuu kwa kuwachukulia hatua za kinidhamu ikiwemo kuwafukuza watumishi wa Mahakama wapatao 112 ambao walibainika kuhusika na vitendo vya rushwa

Hivi majuzi nilitoa msamaha kwa wafungwa, lakini nimesikitika kusikia baadhi yao tayari wamekamatwa kwa uhalifu tena,ipo haja kuangalia upya mafunzo ya magerezani.

Wanatoa hukumu zinazopendelea watu, kuchelewesha hukumu au kesi na kati ya 112 waliofukizwa au kustaafishwa 27 walikuwa Mahakimu na wote walipokwenda Mahakamani walishinda

Walikuwa Mahakimu 14 walifukuzwa kazi, 67 watumishi wa kawaida walifukuzwa kazi. Wito wangu kwa vyombo vingine IGP, Mkuu wa Magereza, Takukuru muige mfano wa Profesa Juma (Ibrahim Juma-Jaji Mkuu.

Habari zaidi....

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema Serikali inaunga mkono utekelezaji wa matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwa Mahakama ili kuongeza ufanisi wa majukumu yake.

Mhe. Rais Magufuli ametoa kauli hiyo tarehe 01 Februari, 2018 wakati akihutubia katika siku ya sheria, maadhimisho ambayo yamefanyika katika Mtaa wa Chimala, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam, yakiwa na kauli mbiu “Matumizi ya Tehama katika utoaji wa haki kwa wakati na kuzingatia maadili”.

Pamoja na kuunga mkono matumizi ya TEHAMA kwa Mahakama, Mhe. Rais Magufuli ameipongeza Mahakama kwa kazi inayoifanya ikiwemo kupunguza mrundikano wa kesi na ameahidi kuwa Serikali ipo tayari kusikiliza ushauri wa Mahakama juu ya maslahi ya wafanyakazi utakaotolewa mwezi huu na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma.

Pia Mhe. Rais Magufuli amesema yupo tayari kufanya uteuzi wa Majaji wengine kadiri atakavyoshauriwa na Mahakama ili kukabiliana na changamoto ya upungufu mkubwa wa Majaji iliyosababisha ongezeko kubwa la mrundikano wa mashauri katika Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani.

Hata hivyo Mhe. Rais Magufuli ametoa wito kwa Mahakama kuendelea kurekebisha dosari ambazo zimekuwa zikiuchafua mhimili huo wa Dola ikiwemo Majaji na Mahakimu kujihusisha na vitendo vya upokeaji wa rushwa na ucheleweshaji wa kesi ambavyo vinasababisha hasara kubwa kwa Taifa.

“Nilikuuliza Mhe. Jaji Mkuu na mimi nasema kwa uwazi kabisa, katika vibali vingi vya kusafiri nje ya nchi ninavyoombwa na Majaji na ambavyo vyote huwa ninaruhusu, na vimenisaidia kufanya utafiti wangu, wengi huwa wanaomba kwenda likizo nje ya nchi, Afrika Kusini, Uingereza, nakadhalika, na wanaenda na familia zao, wanakaa huko kwa siku 28, na pale chini wanaandika kuwa watajigharamia, hili huwa ni swali ninalojiuliza sana, maana mshahara wa Jaji ninaujua.

“Na ukweli huwa nafuatilia anapokwenda kule anakaa hotel na nani amehusika kulipa hotel hiyo yenye gharama za juu, na kwa nini ni fulani fulani tu, Mhe. Jaji Mkuu majibu hujayapata na mimi sijayapata, sasa Mhe. Jaji Mkuu fuatilia hili” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amempongeza Mhe. Jaji Mkuu kwa hatua alizochukuwa kuwafukuza kazi watumishi 112 wa Mahakama wakiwemo Mahakimu 17 waliojihusisha na vitendo vya ukiukwaji wa maadili na amevishangaa vyombo vingine ambavyo hushirikiana na Mahakama kama vile Jeshi la Polisi, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Magereza na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kwa kutowawajibisha watumishi wake wanaokiuka maadili.

“Mwaka jana nililalamika, sasa mwaka huu sitalalamika, nitachukua hatua, tena mwezi huu wa pili hautaisha, pale ofisini kwangu napokea barua nyingi za malalamiko ya ucheleweshaji wa kesi, kila kesi upelelezi haujakamilika, ni lazima kuwe na utatuzi wa jambo hili, hivi sasa kuna kesi za Shilingi Bilioni 169.1 na Dola za Marekani Milioni 38.2 zinasubiri tu na nchi inakosa mapato” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Halikadhalika Mhe. Rais Magufuli amemtaka Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi, kukamilisha kanuni za sheria ya msaada wa kisheria (Legal Aid Act, No.1 of 2017) ambayo imepitishwa na Bunge na kusainiwa na Rais tangu miezi 9 iliyopita, ndani ya kipindi cha mwezi mmoja kuanzia sasa.

Mapema kabla ya hotuba ya Mhe. Rais Magufuli Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma alisema Mahakama imedhamiria kuanza matumizi ya TEHAMA katika shughuli zake na ametaka watumishi hasa Majaji na Mahakimu wajiandae kutumia teknolojia hiyo, na pia ameahidi kuwa Mahakama itaendelea kuchukua hatua dhidi ya vitendo vya ukiukwaji wa maadili na kusimamia uwajibikaji.

Nae Makamu wa Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) Mhe. Godwin Simba Ngwilimi amesema TLS inaunga mkono dhamira ya kutumia TEHAMA katika shughuli za Mahakama na amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa uongozi wake unaoakisi nia na matarajio ya Watanzania.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam
 
A mockery of justice

upload_2018-2-1_10-43-2.png




We need to have respect for due process
BIGSTOCK
We cannot simply punish people on the streets
Last month, a teenage boy, Sagor, was tied to an electric pole and beaten to death by a gang of men, simply because he was suspected of stealing a water pump from a hatchery in Char Sreerampur village of Mymensingh district.

Among his torturous murderers were Akkas Ali, the owner of the hatchery, his son, and four to five of his employees.

Every time Sagor tried to close his eyes, Akkas’s cronies viciously pounded with a slab of wood. The boy repeatedly pleaded for help and forgiveness, cried for water, and begged for his life to be spared.

However, Akkas and his men showed no signs of mercy and the incessant beatings and torture continued until Sagor finally breathed his last.

Thereafter his bloodied body was dumped in nearby bushes to rot, where the police discovered it on Tuesday, about 30 hours after the incident.

Sagor’s father, Shipon Miah, maintained his son was innocent and demanded justice. “My son is a scrap collector. He was not a thief.”

Bearing this clarification in mind, it may well have been the case that Sagor had items in his possession which were not necessarily stolen. Sagor’s elder sister Fatema said: “We want immediate and exemplary punishment to the culprits. We don’t want anything else.”

Onlookers and surrounding villagers, far from coming to Sagor’s aid, either hurled abuse at him or silently enjoyed the show. The incident was even recorded by an onlooker and uploaded on social media where it went viral.

In the footage, two teenagers on either side of Sagor can be seen simply smirking away as though Sagor’s torture was some sort of sport on display for their entertainment.

Are they so blind to see that it could just as easily have been them in Sagor’s position? That a mere suspicion is all it takes to warrant their deaths?

The pecking order

We live in a country where someone’s lack of socio-economic standing is seen as a license to maltreat them, by those “above” them in the social hierarchy.

Sagor is the son of a poor hawker, so naturally his life is worthless and disposable in the eyes of men like Akkas, and can be taken at their whims and fancies.

Akkas seemingly had no fear of any consequences, probably because he is used to seeing so many of his kind get away with their crimes or buy their way out of punishment.

We live in a country where someone’s lack of socio-economic standing is seen as a license to maltreat them, by those ‘above’ them in the social hierarchy

Interestingly, Sagor’s mother alleged that two unknown individuals visited their slum home at midnight and woke them up from bed.

When asked by Sagor’s family to identify themselves, they remained silent and simply offered them Tk10,000 in cash.

While the visitors did not expressly reveal what the money was being offered in exchange for, Sagor’s parents knew what was being implied and categorically refused to take the money.

“They could have pressurised us to withdraw the case after giving the money. I don’t want money in exchange of my son’s life. I want justice,” said Sagar’s mother Hasina Khatun.

Victims of circumstance

This is precisely how criminals like Akkas seek to dodge punishment.

Maybe next time, the amount on offer will be larger and may keep on increasing until Sagor’s family’s willpower finally begins to falter in light of their economic needs.

Sagor’s father said: “Sagor and I would run the family with our earnings. I’m now worried about how to run the family alone.”

Sagor’s case has undeniable parallels with the infamous murder of Samiul Alom Rajon, the 13-year-old boy who was also tied to a pole and brutally tortured to death with a metal rod on suspicion of stealing a rickshaw in Sylhet.

His murderers likewise recorded his horrific ordeal and uploaded the video on social media, where they could be heard laughing and jesting in the background, illustrating just how lightly they took something as grave as the brutal murder of a child.

However, children are not the only ones prone to the threat of vigilantism.

In July 2015, a suspected robber Shamul Islam Monir was lynched to death and, even more alarmingly, the local imam of the village had riled up people using the loudspeaker used to call for prayers.

Similarly, Lucky Akhter, a transgender woman, was lynched to death when she and her friends were asking for gift money at a wedding celebrations as per tradition.

Vigilante justice has no place in a civilised society, or even one that claims to be civilised. There is a reason why “innocent until proven guilty” is the basic premise of the criminal justice system in most countries, including ours.

Everyone has the right to a fair trial from an impartial body. One group cannot at the same time be the complainant, investigator, judge, jury, and executioner as they are by default incapable of being objective in exercising their judgement.

The prevalence of vigilante justice in Bangladesh is rooted in the rampant corruption and inefficiencies of our legal system and the impunity that perpetrators enjoy.

It is high time our country became a place where one’s socioeconomic standing had no bearing on the proper implementation of justice.

Taqbir Huda is currently working as a research officer at Bangladesh Institute of Law and International Affairs and volunteers at Bangladesh Society for the Enforcement of Human Rights.
 
A mockery of justice

View attachment 688578



We need to have respect for due process
BIGSTOCK
We cannot simply punish people on the streets
Last month, a teenage boy, Sagor, was tied to an electric pole and beaten to death by a gang of men, simply because he was suspected of stealing a water pump from a hatchery in Char Sreerampur village of Mymensingh district.

Among his torturous murderers were Akkas Ali, the owner of the hatchery, his son, and four to five of his employees.

Every time Sagor tried to close his eyes, Akkas’s cronies viciously pounded with a slab of wood. The boy repeatedly pleaded for help and forgiveness, cried for water, and begged for his life to be spared.

However, Akkas and his men showed no signs of mercy and the incessant beatings and torture continued until Sagor finally breathed his last.

Thereafter his bloodied body was dumped in nearby bushes to rot, where the police discovered it on Tuesday, about 30 hours after the incident.

Sagor’s father, Shipon Miah, maintained his son was innocent and demanded justice. “My son is a scrap collector. He was not a thief.”

Bearing this clarification in mind, it may well have been the case that Sagor had items in his possession which were not necessarily stolen. Sagor’s elder sister Fatema said: “We want immediate and exemplary punishment to the culprits. We don’t want anything else.”

Onlookers and surrounding villagers, far from coming to Sagor’s aid, either hurled abuse at him or silently enjoyed the show. The incident was even recorded by an onlooker and uploaded on social media where it went viral.

In the footage, two teenagers on either side of Sagor can be seen simply smirking away as though Sagor’s torture was some sort of sport on display for their entertainment.

Are they so blind to see that it could just as easily have been them in Sagor’s position? That a mere suspicion is all it takes to warrant their deaths?

The pecking order

We live in a country where someone’s lack of socio-economic standing is seen as a license to maltreat them, by those “above” them in the social hierarchy.

Sagor is the son of a poor hawker, so naturally his life is worthless and disposable in the eyes of men like Akkas, and can be taken at their whims and fancies.

Akkas seemingly had no fear of any consequences, probably because he is used to seeing so many of his kind get away with their crimes or buy their way out of punishment.

We live in a country where someone’s lack of socio-economic standing is seen as a license to maltreat them, by those ‘above’ them in the social hierarchy

Interestingly, Sagor’s mother alleged that two unknown individuals visited their slum home at midnight and woke them up from bed.

When asked by Sagor’s family to identify themselves, they remained silent and simply offered them Tk10,000 in cash.

While the visitors did not expressly reveal what the money was being offered in exchange for, Sagor’s parents knew what was being implied and categorically refused to take the money.

“They could have pressurised us to withdraw the case after giving the money. I don’t want money in exchange of my son’s life. I want justice,” said Sagar’s mother Hasina Khatun.

Victims of circumstance

This is precisely how criminals like Akkas seek to dodge punishment.

Maybe next time, the amount on offer will be larger and may keep on increasing until Sagor’s family’s willpower finally begins to falter in light of their economic needs.

Sagor’s father said: “Sagor and I would run the family with our earnings. I’m now worried about how to run the family alone.”

Sagor’s case has undeniable parallels with the infamous murder of Samiul Alom Rajon, the 13-year-old boy who was also tied to a pole and brutally tortured to death with a metal rod on suspicion of stealing a rickshaw in Sylhet.

His murderers likewise recorded his horrific ordeal and uploaded the video on social media, where they could be heard laughing and jesting in the background, illustrating just how lightly they took something as grave as the brutal murder of a child.

However, children are not the only ones prone to the threat of vigilantism.

In July 2015, a suspected robber Shamul Islam Monir was lynched to death and, even more alarmingly, the local imam of the village had riled up people using the loudspeaker used to call for prayers.

Similarly, Lucky Akhter, a transgender woman, was lynched to death when she and her friends were asking for gift money at a wedding celebrations as per tradition.

Vigilante justice has no place in a civilised society, or even one that claims to be civilised. There is a reason why “innocent until proven guilty” is the basic premise of the criminal justice system in most countries, including ours.

Everyone has the right to a fair trial from an impartial body. One group cannot at the same time be the complainant, investigator, judge, jury, and executioner as they are by default incapable of being objective in exercising their judgement.

The prevalence of vigilante justice in Bangladesh is rooted in the rampant corruption and inefficiencies of our legal system and the impunity that perpetrators enjoy.

It is high time our country became a place where one’s socioeconomic standing had no bearing on the proper implementation of justice.

Taqbir Huda is currently working as a research officer at Bangladesh Institute of Law and International Affairs and volunteers at Bangladesh Society for the Enforcement of Human Rights.
Ngoja nimsikilize Magufuli kwanza, nitaisoma!
 
Mzee wa matukio naona siku hizi kiki kubwa kubwa hana tena, amebaki kuwa mgeni rasmi kwenye matukio yaliyo na hadhi ya wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri!
 
Anasema mwezi huu wa pili hautaisha atakuwa amenyoosha vyombo vya dola vinavyohusiana na masuala ya kesi, TAKUKURU na attorney general make mkao wa kunyooshwa
 
Back
Top Bottom