Mbona unaanza na kuchimba biti watu hapa??
Kuwakwako member toka mwaka 2007 kinatusaidia nini sisi hapa? Jenga hoja yako bila kutoa vitisho utaeleweka tu, huna haja ya kutengeneza baunsa kwa vitisho vyako hapa... alalaaaaah..!!!! Ukiongea hoja yenye mantiki itajadiliwa hoja, ukiandika upuuzi hapa utajadiriwa upuuzi wako..!! hatuna haja ya kujua umejiunga lini Jf. Na huu ndio uzuri na changamoto ya Jf ya sasa.!!
Back to the topic.
Eti unasema Chadema pekee wana kura 2ml?? Na Zitto pekee ana kura 1.5ml...!!! We jamaa kunasehemu umeamkia kweli si bure.. Hivi Unajua idadi ya wanachama wa Chadema nchi nzima?? Yaani kwa hoja yako unataka kusema kuna watu zaidi ya Milioni moja nukta tano, wameondoka na Zitto kwenda Act?? Jitafakari upya kaka..!!! Hii ni 2015 wala si 2010,2005 or 2000/1995...!!!
Binafsi mimi sina tatizo na Zitto, nunamuunga mkono tangu zamani, ila ninakuhakikishia pindi akisimama Zitto kugombea Urais Sambamba na Mgombea yeyote wa Chadema/UKAWA, Zitto aisahau kura yangu. Kumuunga kwangu mkono Zitto ni ktk Ubunge Yaah namuhitaji Bungeni kwaajili ya kuongeza nguvu ya upinzani Bungeni maana naye anajitanabaisha kwamba ni mpinzani. Yes hili nitalipigania kwa nguvu zangu zote hata kwa maombi.
Halafu tambua, ujanja wa Kenyatta Uhuru ndio uliopelekea yeye kuungana na Ruto pale Kenya. Kabila la Ruto ndilo lililompa u-Vice President pale Kenya na si vinginevyo..!!!
Kenyatta baada ya kutambua nguvu za kabila lake na nguvu za Kabila la William Ruto ndio akaamua kuomba kuungana, maana kwa siasa za ukabila za Kenya Kenyatta asingepata chochote kwenye uchaguzi ule ,zaidi angemtengenezea njia rahisi ya kuingia ikulu bwana Odinga. Sisi hapa Tanzania hatuna siasa za ukabila ile sema siasa za Udini zinaanza kutuvamia taratibu bila kujijua (kilaaniwe chama kilichopo madarakani) Lakini hata tukija kwenye hizo siasa za udini UKAWA imekuwa tumaini la Wananchi kwasababu ya hizo siasa za udini, (Sote tunatambua namna ccm walivyovivumisha vyama viwili Cdm na Cuf) Na hapa ndipo ninapikushangaa unapodai ati ni heri kwa Chadema kuomba kuungana na Zitto kuliko kuomba kuungana na Lipumba (Cuf) nadhani mkuu umeamua kufuraisha baraza hapa.!!!
Hivi Lipumba kwa siasa zetu hapa Tanzania hana impact yoyote isipkuwa Zitto..!!!! Jamani hata kama tunawajenga watu kwa malango wa nyuma tijitafakari maana tunaweza kuwa tunawabomoa kwa mlango na lengo lilelile tulilokuwa tunadhani tunawajenga.
Khaaaaaaaa....!!!!!
BACK TANGANYIKA