Why UKAWA will loose the 2015 Election

Why UKAWA will loose the 2015 Election

Bado kuna sababu nyingi UKAWA kupoteza

ikiwepo baadhi ya member wao kusapoti viongozi wa CCM
ikiwemo Lowasa kwa maana hyo watampigia kura Eddo....
 
Wote wanaomini mtazamo wako wanatoka ccm na kwao ni faraja bila uhalisia.

@.

Kwanini kuna hii imani lakini? Kwamba kila anayekubaliana na zitto au kuwa mfuasi wa Zitto ni mtu wa Ccm?? Ccm hawahawa waliojeruhiwa na Zitto bungeni kwa miaka nenda rudi leo wawe na mahaba na Zitto??
Hamuamini kuwa wapo watu wanafikiri na kutenda tofauti na nyinyi??? Na bado hamuamini kuwa Chadema ilikuwa na wafuasi wengi nyuma ya mgongo wa Zitto?? Hamuamini ya kuwa kuna vijana wengi waliovutiwa na siasa kwa mgongo wa zitto na wengine leo hii ni wabunge na nafasi nyinginezo za kisiasa??? Hamuamini ya kuwa kwa kadri zitto anavyosurubiwa kwa kuitwa msaliti basi mashabiki na wafuasi wake wameamua kukaa kimya na mapenzi yao kifuani?? Mkiona kimya mwajua " mmemumaliza?"
 
Kutumia "Kisa mkasa" cha Kenya kufanya uchambuzi wa siasa za Tanzania ni jambo lenye kuleta ukakasi. Rais Uhuru Kenyata alishindwa ktk uchaguzi wa mwaka 2002 na Mzee Kibali kwa sababu kura za Wakikuyu walizigawana na watu wenye kusikilizwa/ushawishi ktk makabila mengine mfano Raia Odinga, Najibu Balala walikuwa upande wa Mzee Kibaki. Mwaka 2012 Uhuru aliamua kuwa na Rutho kwa sababu ndie mtu pekee aliekuwa na ushawishi katika Kabila lake. Hapa kilichokuwa kinatafutwa si nguvu ya kuunganisha makabila ndio maana hata Najibu Balala waliamua kuwa nae. Kingine kilichowasaidia ni mkakati wao wa kampeni kujenga vijana zaidi na ndio maana kuna baadhi ya wasanii wa hapa nyumbani walichukuliwa. Tujiulize hizo kura milioni 1.5 alizozishika Ndg Zito Kabwe ni za kundi lipi hasa. Je, ni za watu wa Kigoma? Ni za wasanii? Ni za vijana wa vyuo? Au ni za kina nani? Kenya ukisema fulani anashikilia kura mfano laki 5, tafsiri lahisi ni anaungwa mkono na watu wa kabila Lake.
 
Impossible to a new political part like ACT to get more than 1million votes, (poor estimates) since you have taken into consideration only one factor (new member ZZK).
Your estimates is not clear and valid enough to convice voters because it is not recent data (2010) perhaps u could use recent data as well as other recent research to make your argument strong, this could avoid biases, also there could be no room to question your objectivity also your competence.
You didn't provide your recommendations towards your opinions provided,

Its not impossible to get 1m votes for a new political party, especially those formed on election year, i put into the fact the new voters registration system, it will bring around 3-5 new voters who are up for grabs. I have also put into consideration social media as a new marketing tool( Zitto has perfected in this), moreover the ability of the man to win new voters is not in question, plus there is sympathy voters for him; Chadema defectors e.t.c SO its around 1 m what he and his new party will get.
In making political analysis for the presidency, you can only use the last presidential election as your base, of course you put into consideration the by elections and how they can swing the votes.
I am not after convincing voters to vote for any political party but rather trying to analyze the coming election.
My objective is to learn about political situation in Tanzania and air my opinion just like any other concerned Tanzanian. My competence is not so relevant for you, here in JF we look at the content not the person, that is why we have avatars and not real names.
RECOMMENDATIONS are coming from different members through the debate;
 
Mjadala wa aina hii unasikitisha sana. Yaani tunaweka akili zetu kwenye mikakati ya ushindi kama vile ndio "mwisho wa yote" - an end in itself - badala kuwianisha na mustakabali mzima wa taifa. Sioni Kabisa umuhimu wa kufikiria ushindi wa chama chochote cha siasa kama hautaleta mabadiliko ya msingi kwa mwelekeo wa taifa hili. Kama UKAWA watamuhitaji Zitto ili almuradi washinde uchaguzi tu hata kama haendani na mtazamo wao (wa kuleta mageuzi) basi nao watakuwa janga jingine kulikumba taifa hili baada ya uozo wa CCM.
 
Kwanini kuna hii imani lakini? Kwamba kila anayekubaliana na zitto au kuwa mfuasi wa Zitto ni mtu wa Ccm?? Ccm hawahawa waliojeruhiwa na Zitto bungeni kwa miaka nenda rudi leo wawe na mahaba na Zitto??
Hamuamini kuwa wapo watu wanafikiri na kutenda tofauti na nyinyi??? Na bado hamuamini kuwa Chadema ilikuwa na wafuasi wengi nyuma ya mgongo wa Zitto?? Hamuamini ya kuwa kuna vijana wengi waliovutiwa na siasa kwa mgongo wa zitto na wengine leo hii ni wabunge na nafasi nyinginezo za kisiasa??? Hamuamini ya kuwa kwa kadri zitto anavyosurubiwa kwa kuitwa msaliti basi mashabiki na wafuasi wake wameamua kukaa kimya na mapenzi yao kifuani?? Mkiona kimya mwajua " mmemumaliza?"

Ndio tatizo kubwa ya ndugu zangu wa Chadema, ukipingana nao kihoja au ukikubaliana na BAADHI ya hoja za ZZK wewe unakuwa ni adui wao na kibaraka wa CCM. Jambo ambalo si kweli,
Yapo mambo ya msingi ZZK amelifanyia taifa hili, kama alikosea kwenye chama chake na wakamuadhibu hiyo ni mambo yao ya chamani. Hata CCM wanagombana kila siku,,lakini sisi kama watanzania hayo si muhimu kwetu. Cha muhimu kipindi cha uongozi wake kasimamia madini na sheria zake; Uwajibikaji serikalini: Kachochea mwamko wa kisiasa kwa vijana wengi na mengineyo ambayo sote tumeyaona kama watanzania.
 
ACT bado mnasafari ndefu sana kuitoa CCM madarakani, hiki chama kina MIZIZI MIZITO sio rahisi rahisi kukitoa madarakani, kina mambo mazito siku kikitoka madarakani na mungu aepushie mbali nchi hii haitakaa salama, labda niwaambie inaweza kutokea labda " WATANZANIA WALIMUONA MWALIMU NYERERE KWA MACHO WAISHE WOTE HUKU DUNIANI".

Freema Mbowe alitumiwa na mizizi mizito kuiua CUF mwaka 2000, akafanikiwa, Leo mtatumika nyinyi kuiua CHADEMA na hilo litafanikiwa , mjiandae kulikamilisha hilo kwa umakini mkubwa na endelevu.


CCM CCM haitakaa itoke madarakani hajazaliwa bado wa kuiangusha CCM, CHAMA CHA MAPINDUZI, chama imara nchini.
 
ACT bado mnasafari ndefu sana kuitoa CCM madarakani, hiki chama kina MIZIZI MIZITO sio rahisi rahisi kukitoa madarakani, kina mambo mazito siku kikitoka madarakani na mungu aepushie mbali nchi hii haitakaa salama, labda niwaambie inaweza kutokea labda " WATANZANIA WALIMUONA MWALIMU NYERERE KWA MACHO WAISHE WOTE HUKU DUNIANI".

Freema Mbowe alitumiwa na mizizi mizito kuiua CUF mwaka 2000, akafanikiwa, Leo mtatumika nyinyi kuiua CHADEMA na hilo litafanikiwa , mjiandae kulikamilisha hilo kwa umakini mkubwa na endelevu.


CCM CCM haitakaa itoke madarakani hajazaliwa bado wa kuiangusha CCM, CHAMA CHA MAPINDUZI, chama imara nchini.
 
Mjadala wa aina hii unasikitisha sana. Yaani tunaweka akili zetu kwenye mikakati ya ushindi kama vile ndio "mwisho wa yote" - an end in itself - badala kuwianisha na mustakabali mzima wa taifa. Sioni Kabisa umuhimu wa kufikiria ushindi wa chama chochote cha siasa kama hautaleta mabadiliko ya msingi kwa mwelekeo wa taifa hili. Kama UKAWA watamuhitaji Zitto ili almuradi washinde uchaguzi tu hata kama haendani na mtazamo wao (wa kuleta mageuzi) basi nao watakuwa janga jingine kulikumba taifa hili baada ya uozo wa CCM.

Sawasawa mkuu, mapema miaka ya 1960 wakati nchi nyingi za kiafrika zikipigania uhuru kutoka kwa mkoloni wengi wa wapambanaji walikuwa tu zaidi na ile dhamira ya kumwondoa mkoloni, tujitawale. Na wapo wabaya ambao hasa walichokifikiria ni kuchukua nafasi zilizokuwa chini ya mkoloni na sasa ziwe zao na kufaudi meza zenye kuku wa mirija walizoketi wazungu. Kukosekana umakini katika hili ulisababisha nchi nyingi za kiafrica kushindwa kusonga mbele baada ya kupata uhuru na nchi nyingine kurudi nyuma kabisa. Hii ilielezwa vizuri na Mwandishi Rene Dumont katika kitabu False start in Africa miaka ya 60. Leo hii napozitazama siasa za Tanzania na sehemu nyingine za Africa mwelekeo wake unashabihiana na hali niyoelezea hapo juu, kwamba tatizo kuu la Tanzania ni chama kilichoko madarakani ccm, na suluhisho la matatizo ni kuiondoa tu ccm madarakani, kana kwamba mara ikitokea tu hivyo basi tunaingia nchi ya maziwa na asali, tumesahau kuangalia ni kina nani hao hasa watakaoongoza taifa hilo na wana uwezo gani kuleta mageuzi ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Hivi vyama vyetu ni mavazi tu lakini cha msingi ni miili na roho zilizoko ndani yake, katika africa vyama karibu vyote vina sera sawasawa tu na raia wengi hawajihusishi na sera, watu ndo wanatawala maamuzi katika chaguzi zetu sio vyama!
 
mleta maada ameonyesha upungufu na uvivu mkubwa wa fikra.hata kuokota data inamshinda namshauri arudie darasa la sita
 
Kwanini kuna hii imani lakini? Kwamba kila anayekubaliana na zitto au kuwa mfuasi wa Zitto ni mtu wa Ccm?? Ccm hawahawa waliojeruhiwa na Zitto bungeni kwa miaka nenda rudi leo wawe na mahaba na Zitto??
Hamuamini kuwa wapo watu wanafikiri na kutenda tofauti na nyinyi??? ..."

Tatizo ni Zitto kupigiwa chapuo na wapinzani wakali wa CHADEMA hapa JF. Halafu, CCM si moja. Zitto ana uswahiba wenye mashaka na watu wenye nafasi zao ndani ya CCM ambao haonekani kugusa maslahi yao kabisa. Kama vile nao wanamtumia kimkakati kuwazima washindani wao ndani ya chama. Anyway, CHADEMA wana intelijensia kamili ya suala hili - toka hukohuko ndani ya CCM na dola.
 
Hahaahaa moron mangoose et zitto has 2 million votes??alishinda ubunge kwa kura ngapi?wait and see what will happen ayatollah hafui dafu
 
Kwa jinsi ulivyomalizia uzi wako wewe mleta mada unaonekana kama unajishuku hivi. Hiyo mifano unayotolea kuhusu Kenya sidhani kama ungeitolea kwenye upande wa maendeleo.

Ni hivi hapa naona kama umekuja kuandaa watu kisaikolojia kwamba Ukawa watashindwa na unalazimisha sababu iwe ni Zitto.

Kama kweli unachokisema ni hicho mbona hao CHADEMA hawakushinda urais 2010 wakati Zitto akiwa bado cdm?

Umeweka na idadi kabisa ya wapiga kura kwa mujibu wa mtazamo wako, lakini ukiangalia ni kama vile mada yako inalazimisha kwamba bila Zitto basi Ukawa hawawezi kushinda urais!!

Hivi ni nani unaweza kumdaganya tena kwa hisia za kwamba bila Zitto CHADEMA hakuna. Wote wanaomini mtazamo wako wanatoka ccm na kwao ni faraja bila uhalisia.

Naomba nikupe mfano mrahisi wa karibuni, hivi majuzi kumefanyika uchaguzi wa serekali za mitaa, ukiachia mbali zoezi kuendeshwa kwa hila na mapungufu mengi, CHADEMA wamezoa viti vingi sana bila mchango wowote wa Zitto.

Sasa nashangaa unalazimisha data za mwaka 2010 unaacha za hivi karibuni kabisa na madhara yake kwa uchaguzi mkuu ujao.

Kama ni kweli usemacho nilitarajia uchaguzi huu uliopita miezi michache ndio ingekuwa sehemu ya wewe kujengea hoja na sio mwaka 2010 ambapo hata aina ya matokeo yalipatikana kwa vitisho na ugomvi mkubwa.

Kama unataka kumtetea Zitto wewe mtetee kwa njia nyingine na sio zaidi ya hapo.

du! kaka, ukawa wakitajwa unakasirika lo! hiyo si demokrasia, unatakiwa uwe na ngozi ngumu
 
Tanzania politics is based on what????

Where ZZK political forces came from???

Please explain more ndugu,,tunajifunza tu hapa



Sounds like you didn't have a clear insight into what kind of political wave Zitto was riding on to play his political cards right in the first place!Youths?No,Don't count Youths into leaning to Zitto and his ACT come election day. Youths are rebellious in nature against any ruling party and they are impatient enough to even trust an infant political party like ACT to help them realize their dream of seeing CCM out of power,So they will obviously stick with UKAWA as the most reliable political force that will help them achieve their goal of ousting CCM out of the power.
When you think of Muslims as his reliable voting block then you will be making a mistake. Muslims will never follow Zitto, He is not the guy they would trust like they did to Kigoma Malima.
So I really don't know what your point is, Sir.
 
Simple kuwa member since 2007 siyo hoja kwanza.

Pili uliyoyaongea yaweza kuwa kweli au yakawa si kweli ni namna ya kuziweka changamoto zitakazoikumba UPINZANI.

Tatu yake kumbuka wenye pesa zao ndiyo waliofanya Zitto akashindwa kesi,kwa kuiondoa tu kesi kwa mlango wa nyuma.

Nitakupa sababu zangu kadhaa:

1.Zitto anajua fika hata yeye bila UKAWA Jimbo la Kigoma mjini hapiti,hivyo anahitaji UKAWA sana tu.

2.Zitto pia anaubinafsi akiona ni njia ya kupata UBUNGE basi atawamwaga wenzake njiani kwa kutowasaidia kwenye kampeni na hivyo indirect kujiunga na UKAWA.

Na ukimsikiliza vyema kwenye HOTUBA zake anasema wazi anasupport UKAWA na hivyo indirect sababu pale ndiyo nguzo yake na yeye ili ashinde kwa kishindo lazima ale na kipofu.

Hivyo basi kwa kula na kipofu hawezi kuwaumiza UKAWA na cha msingi UKAWA wawe tu waangalifu kwenye kuweka makubaliano na Zitto.

Na mwisho ukiangalia kwa makini Zitto kwenye uchaguzi wa 2010 hakuwasaidia wenzake wa CDM ili waweze kupata kura nyingi zaidi.Tumemuona Kafulila akihangaika mwenyewe,John Mnyika nk,hivyo sidhani kama Zitto peke yake anaweza bali anatakiwa awe na wenzake ili kuweza kuiweka motoni CCM.

Mwisho kabisa Zitto aliondoka CDM miaka mingi iliyopita alikuwa hajishughulishi kabisa na CDM hivyo sidhani kama ile nguvu ya kuiumiza sana CDM bado anayo.

Na kumbuka Zitto siyo Chama na ukishaweka mwanachama kuwa ni muhimu kuliko Chama basi ujue utajenga CCM nyingine.
 
Zitto ni mrema wa pili hana mpyaa jipya act-wasaliti is the begining of his total colapse hana ubunge wala udiwani kafulia hana mpyaa
 
Perhaps it's a typo in your title - I think you intended 'lose' instead if 'loose'. If so, please make a correction.
 
Ndio tatizo kubwa ya ndugu zangu wa Chadema, ukipingana nao kihoja au ukikubaliana na BAADHI ya hoja za ZZK wewe unakuwa ni adui wao na kibaraka wa CCM. Jambo ambalo si kweli,
Yapo mambo ya msingi ZZK amelifanyia taifa hili, kama alikosea kwenye chama chake na wakamuadhibu hiyo ni mambo yao ya chamani. Hata CCM wanagombana kila siku,,lakini sisi kama watanzania hayo si muhimu kwetu. Cha muhimu kipindi cha uongozi wake kasimamia madini na sheria zake; Uwajibikaji serikalini: Kachochea mwamko wa kisiasa kwa vijana wengi na mengineyo ambayo sote tumeyaona kama watanzania.

ndugu zako chadema,je ww uko chama kipi?,,,poor act
 
Back
Top Bottom