stanlthecreator
JF-Expert Member
- Jan 9, 2014
- 1,947
- 648
Kwa upande wangu...
1. Takribani wapiga kura milioni 1 wa mwaka 2010 hawatapiga kura mwaka huu
2. Takribani wapiga kura milioni 15 watapiga kura mwaka huu, milioni 8 wakiwa "wapya"..
3. Takribani wapiga kura milioni 1 waliopigia CCM mwaka 2010 hawataipigia tena mwaka huu (hii itashuhudiwa zaidi Arusha, Manyara, Mtwara, Lindi, Songea, Morogoro, Singida na Tabora)
4. Takribani wapiga kura laki 2 walioipigia CDM kura mwaka 2010 hawataipigia mwaka huu (Kigoma, Rukwa, Katavi)
5. ACT haitaweza kupata zaidi ya kura laki 2 kwenye uraisi kwa sababu haitakuwa na mgombea mwenye nguvu, na hata yenyewe haitakuwa na nguvu za kufanya kampeni
Halafu
1. Asilimia 50 ya wapiga kura hadi sasa wameshaamua chama watakachopigia kura bila kujali mgombea ni nani
2. Asilimia 25 ya wapiga kura watapiga kura kwa kuangalia mgombea ni nani
3. Kati ya hao asilimia 25, asilimia 10 ni watiifu wa Lowassa, kama hatapitishwa, asilimia 8 kati yao watapigia vyama vingine kwa hasira
4. Asilimia 25 ya wapiga kura wataamua kutokana na upepo na ushawishi wa kampeni
5. CCM kwa kutumia tume ya uchaguzi na dola, watalazimisha asilimia 5 ya kura kwao...
Kazi bado ni ngumu...
Nice analysis,nakubaliana na wewe kuhusu mtazamo wa watanzania wengi kwa sasa,wanaangalia sana mgombea gani kuliko chama hii ni tofauti na 2010.Kwa mantiki hii kura laki 2 kama ulizoandika hapo za ACT zinaweza kuwa zaid (mayb even million) japo sina data za population za kigoma na tabora bt Zito popularity inaweza kuchange upepo wa upinzani na kuongeza kula za ACT.