WHY SLAA MUST RESIGN...! "..effect of the crowded house.."

WHY SLAA MUST RESIGN...! "..effect of the crowded house.."

Slaa akiresign itakua pigo kubwa sana kwa chadema kwa wakati huu wa kukijenga chama. Na itakua ni ushindi kwa chama tawala.
 
Kwanza mimi sio mwanachama wa CHADEMA ni mtanzania mwenye kiu ya mabadiriko, Pili Alichokisema mnyika ni kwamba uchunguzi wa shutuma na tuhuma zinazotolewa umeanza kufanywa, uchunguzi ukikamilika unaweza kuja na matokeo ya kuwapo kwa makundi yote mawili, au moja au hakuna makundi au kuja na mambo mengine kabisa kama tatizo halisi.

Wewe umekwishakutoa hukumu tayari. wewe ni kama mungu kabisa wewe

wahi lumumba za kesho chapu
Slaa unadhani unaweza kumwondoa kama mukama unadhani unaongea na nec ya kizota yamkini hujitambui unawashauri wakina nani ushauri wako unastahili nec ya sisimu kumuondoa kinana
chadema huwez kuishauri hvyo kama unaelewa siasa za Tz kama wewe si mwanachama
 
Nashukuru wanajamvi wazalendo threats za Kimasalia au P7 au za kuua panya kwa kosa la mwingine hawazijibu kihoja bali kiviroja kama zinavyoletwa wanawapa ushauri waandishi wa kimasalia wanaachana na mawazo yao na ushauri wao.
Soma wapuze waattack na umasalia wao usichambue hata kama watatumia falsafa kututeka tuwashauri wawah za mgao maana wakina tandale na wenzake wamejeruhiwa na kamanda ben hawajui wanachoandika
 
Jamani, hizi Jitihada za kumuzoofisha DR SLAA na CHADEMA nadhani zinafanyika kwa imani kwamba zitafanikiwa kama ambavyo iliwezekana kumzoofisha Augustine Ryatonga Mrema na NCCR yake.

Kuna mtu anaweza kutuchambulia kama mbinu zilizotumika kummaliza Mrema ndio hizi tinazoziona dhidi ya DR na kama mapungufu yaliyokuwa NCCR wakati huo ndio yaliyopo CHADEMA pia.



Je? DR SLAA ataufikia Mwisho wake kama ilivyotokea kwa MREMA au ndio CHURA anasaidiwa kuruka kiaina?

Hii itanisaidia mimi binafsi kusheherekia xmass hii kwa amani kidogo.
 
Mgogoro upi huo ni huu wa kupikwa na CCM baada ya kuona wananchi wamekosa imani nayo au ni upi huo?
Ni mtanzania gani asiyejua mbinu chafu na za zamani zinazotumiwa na CCM kwa yeyote wanayemuona kuwa ni tishio kumpaka matope ili aonekane hafai?

Anzia kwa wakati ule Augustino Mrema, CUF, CDM kuwa ni chama cha wachaga, lakini baada ya kuamka usingizini na kukuta chama kimeenea na kukubalika nchi nzima, sasa wamekuja na gia ya kumchafua Dr. Slaa ambaye wanamhofia kwa kutokuwa na suluhu na wala rushwa na mafisadi.

Mgogoro mkubwa uko kati ya wananchi walioamka toka usingizi wa kudanganywa kila siku kuwa Tanzania ni kisiwa cha amani wakati wachache wanaendelea kugawana raslimali za nchi, na watawala wanaokumbatia rushwa na ufisadi uliokithiri. Acha kupagawa kwa mageuzi yanayokuja kwa kasi nchi hii dhidi ya utawala dhalimu.

Yako wapi mabilioni yaliyowekwa Uswiss kutokana na rushwa, wako wapi wanyama wetu, madini yetu na misitu yetu na ardhi yetu?. Mbona huoji hayo kama unaitakia mema nchi hii?

Wako wapi usalama wa Taifa waliopaswa kuhakikisha raslimali za nchi hii zinalindwa lakini badala yake wamekuwa ni taasisi ya kuhakikisha watawala wanaendelea kutawala kwa gharama yoyote ile?. Ni vipi mwananchi raia tu wa kawaida aambiwe ataje majina ya mafisadi wakati vyombo vya dola ambavyo leo vinatanua kutokana na kodi zetu vipo na vinajua kila kinachoendelea ktk nchi hii?

Unapaswa kuwa mwangalifu ktk hoja zako, zisizidishe hasira kwa watanzania waliokata tamaa na kuvumilia kwa muda mrefu. Nchi inahitaji kuwa na kiongozi ambaye yuko tayari kuifia nchi ili iwe na usawa ktk mgawanyo wa rasilimali za nchi na isonge mbele, na aone matatizo ya wananchi kama mzigo wake, hata kama itabidi afe maskini.

Mfano wa marehemu Sokoine. Na usitegemee hata siku moja kuwa mtu wa aina hiyo atakubalika ktk mfumo wa utawala wa sasa.

hata hili nalo ni mbinu chafu..? ushauri huu unafanana na mbinu chafu..? hivi ni kweli kuwa ufahamu wenu unawatuma kuamini kuwa hii ni mbinu chafu ya CCM katika kuihujumu chadema.,ushauri huu unafanana na hujuma, kwa mfanano upi hasa.,ama kwenu hujuma ni ipi..? mnatafsir vipi hujuma..? kuhusu hayo mengine ninashauri kwa wakati na wasaa wangu kama ninavyoshauri hapa juu ya chadema.
 
Wabongo huwa hawataki kabisa kusikia kitu inaitwa RESIGNATION

Lazima tubadilishe hii mentality.,hatukuzaliwa hivi kama taifa.,tunayo misingi ambayo kama tukishikamana nayo haya yanayojitokeza sasa hayatatuyumbisha.,ni wazi kuwa huko nyuma kiongozi katika level yeyote ilikuwa ni fahari kwake anapotajwa kuhusika na shutuma zozote ku-resign, tofauti na leo hii ambapo anayeresign na hata wale wanaopokea resignation hiyo wote hudhani kuwa ni fedhea kubwa na kujishusha thamani.

Hili ni la kulibadilisha...!
 
Kweli mti wenye matunda ndio unaopopolewa na mijiwe!
 
Mtasema mengi sana wakati huu kuondoa fikra zetu katika hisia za kuleta mabadiliko. Hata hivyo bidii hizo hazitafua dafu mpaka lengo letu la kujikomboa likamilike. Baada ya hapo kama kuna mtu mwenye agenda yake ajitokeze na tutamsikiliza.

hili nililolisema kwa namna yeyote linawatoa nyie katika fikra zenu za kuleta mabadiliko..? ni fikra zipi hizo ambazo zinahukumu ushauri huu..? zina mlengwa gani fikra hizo, zinataka mabadiliko yapi ambayo thread hii haiyataji kuwa ni muhimu ama haishauri mabadiliko hayo, kwani kama ni mabadiiliko basi nadhani nimeshauri mabadiliko tena makubwa ndani ya chama ili kujenga mustakabali mpya wa chama hiko...!
 
Thibitisha madai yako ndo tujue wewe huna nia chafu!
 
Slaa akiresign itakua pigo kubwa sana kwa chadema kwa wakati huu wa kukijenga chama. Na itakua ni ushindi kwa chama tawala.

Mtazamo huu siuhafiki, ni mtazamo wenye makengeza kudhani kuwa bila slaa hakuna chadema, sitaki kuamini kuwa mnanishawishi niamini kuwa Chadema kuna uhaba wa viongozi wa kuweza kukisimamia chama hiko na kukiendesha. kama hivyo ndivyo basi chadema kuna hatari kubwa kuliko vile nilikuwa nikidhani...!
 
Hakika ndugu tandale unatisha katika kuchambua mambo ! ni watu waliotulia na vichwa makini wataelewa uloyaandika humu ,! chadema wafuasi wamelewa mvinyo wa kisiasa watajuta nasema kwa dhati ya moyo wangu nimeongea na viongozi wa wilaya kadhaa wengi wanahaira ya slaaa ,kubalini kilio cha watu msione watu wametumwa skilizeni maoni ya wanachama bila hayooo,mtakuja juta ,tatizo hamuamini lolote kwa sasa hata mkiambiwa ukweli juu ya udhaifu wa huyu mungu wenu slaa mnaona ametumwa hawa ,saa inakuja ambapo mtayaweka matumaini kwa mkombozi wa kweli Mungu wa Yakobo
 
Kama ni ngumi basi Dr Slaa kawakaba kwenye kona, wanatafuta kila namna ya kutoka hata kama ni foul play lakini refa yuko macho, na bado!
CCM hoyiiiiiiiiiiiii!
 
Uharo mwingine wa kukaribisha Xmas .Bia za bure hizi na bahasha za Kinana .Waacheni Chadema na mambo yao wewe si mwanachadema wala shabiki na mpenzi ya nini kuumia .Jipangeni kuua tembo kaka
Lunyungu,hawa watu wanastahili kuitwa wapumbavu.Mara Slaa ni pandikizi lao,mara anataka uraisi 2015,hivi ni wapi Slaa alipotamka anataka hilo? Hata uchaguzi uliopita tuliona jinsi CDM walivyotumia nguvu ya ziada kumshawishi Slaa kusimama kugombea. Ni upuuzi kumsemea adui yako eti fulani ni mzuri zaidi ya yule kupambana na mimi.huyo wanayemuona mzuri sii wamchukue!
 
Mwambie kwanza wa kwenu arisaini? Mbona mambo kibao na hamsemi neno? Acheni mambo ya masihara!! Kweli mnaiogopa CDM. Kubalini yaishe kuwa hakuna wa kupambana na dr. bila uchakachuaji!!
 
1.Kwanza ni huu mtego kwa dr slaa eti ajiuzulu halafu hoja zinazokuja za yeye kujiuzulu ni za kipuuzi mno na dhaifu mno,lakini ninachokiona ni kutokana na dr slaa na misimamo yake ya kuwa serious na kutotaka utani kwenye kazi hivyo kwa wale waliotaka wanufaike kupitia chama na wameshindwa ni lazima waanze kutapatapa huku na kule huku wakijua dr slaa akiondolewa chamani labda ndio watapata unafuu wa kufaidika na chama(kwa yale makundi yanayoratibiwa na zitto).
2.kundi jingine ni wale waliotoka ccm na kuja chadema baada ya muda wanarudi ccm,wakiulizwa kwanini wametoka chadema wanaanza unajua tulidhani hiki chama kina lengo la kumkomboa mtanzania kumbe hakuna kinaongozwa kikanda na mengine mengi kumbe ni hakuna kitu isipokuwa ameona hanufaiki na chama kimaslahi na kuamua kurudi ccm ambapo mambo hayaendi bila posho za mara kwa mara na wakati ukiwa chadema ni full kazi ileile kama hutaki timua.
3.Mwisho ni hawa watu wanaojipambanua kwa kujiita "pindua mbowe PM7" wakiongozwa na zitto kuwa wao ndio wanaofaa na kukemea mambo ndani ya chama eti chama kinakiuka demokrasia,lakini ukiwasoma kwa umakini hakuna kingine tofauti na mashambulizi yao kila kukicha kuyaelekeza kwa dr slaa kitu ambacho kinaonyesha dhahiri wana agenda yao ya siri iliyofichuliwa na huyu ben saa8,mchange analalama kuenguliwa kwake kwenye uchaguzi wa mwenyekiti bavicha lakini hata ukisoma ushahidi wa kuhusika kwake na rushwa kwenye gazeti la mwanahalisi hapo mwaka jana kwenye uchaguzi unaridhika kabisa kila ki2 kimeanikwa kuhusika kwake kuwahonga wajumbe wapiga kura.
Kuhusu zitto ndio kaonyesha bado mchanga wa siasa kabisa,kwanza zitto nilimfahamu kwenye siasa baada ya sakata la buzwagi na kufukuzwa bungeni,,baada ya hapo chama kikazunguka naye nchi nzima kupinga uonevu wa ccm bungeni,,na hapo watz wengi ndio tukamjua zitto,,baada ya kufahamika dogo akavimba kichwa na kijiona kuwa kumbe nakubalika na ninastahili urais na kuanza kutoa makauli ya kipuuzi mara kikwete ni rafiki yangu na mbo mengine baada ya kuanza kuzila pesa za serkali kupitia kuwemo kwenye ile tume iliyoundwa na kikwete kwenye sakata la buzwagi.
Hadi leo zitto kishasahau kuwa umaarufu wake uliletwa na chama,kama dr slaa hafai kwenye ukatibu mkuu si asubirie uchaguzi wa chama ufike achukue fomu na kwenye kujinadi awashawishi wajumbe kuwa dr slaa hafai kwa sbabu hizi na hizi then wamchague yeye na hapo mchezo kwisha na hiyo ndiyo demokrasia,kwenye urais hivyo hivyo achukue fomu.Lakini humu JF ilianzishwa political poll ya kumpambanisha zitto na dr slaa,,dr slaa hadi sasa ameshampita mbali saaana lakini wapi bado kanalazimisha ubabe wake na si kufuata demokrasia.
HADI SASA ZITTO NA HAO WAKINA TUNTEMEKE WAKE WAMEFUNGUA ID NYINGI SANA HUMU LENGO NI KUANZISHA THREAD NA KUANZA KUJISAPOTI WAO KWA WAO KWA KUTUMIA ID TOFAUTI TOFAUTI WALIZONAZO.HIVYO KUENI MACHO HUYU MWANASIASA UCHWARA,,namshauri huyu bwanamdogo zitto aje huku herujuu kasulu(kigoma) nimpe ushauri kuliko kuendelea kuwavuruga wanamageuzi wa kweli akina dr slaaa na huku kigoma wengi tutamuunga mkono dr slaa na utaishia kufilisika kisiasa kama mwenzako kaburu alivyobakia historia hadi leo kinachowaponza hawa wanasiasa wengi wa kigoma ni ulimbukeni tu,akisifiwa kidogo anavimba kichwa
 
Jifunze Kufupisha maelezo,marefu sana.

Muda bado Slaa kuresign,ataendelea kuwapa wakati mgumu...
 
Back
Top Bottom