Binafsi nadhani jamaa ana points, na sidhani kama ni kundi la kina Tuntemeke hata kama ni mmojawapo lakini amekuja vizuri! Lakini suala la kujiuzulu Slaa siafiki hata kidogo, ila nachojua kwa namna yoyote ile hizi scandal zitaharibu staha ya chama!
Mimi concern yangu ni kwa Watz, wengi wao si wa kuchambua mambo kwa kina, hivyo haya mambo yanayoendelea hatujui jinsi gani yanavyowagawanya! Watz ninaomaanisha si wale ambao kila siku wako humu JF, bado kuna asilimia kubwa dunia kwao sio kijiji kama ilivyo sasa! Binafsi nina imani V, wanajua kinachoendelea lakini wana subira ya kufanya maamuzi kwa wakati muafaka, lakini nina imani wamepima umuhimu wa maamuzi hayo sasa na athari zake, ama kufanya maamuzi hayo baadae na athari zake hii ndio imani yangu! Lakini huwa nawaza kuwa, ili kuchukua nchi tunahitaji hata hzo kura za hao wengine, ambao wana excuse kibao utadhani kwenye nyumba yao ni wasafi kihivyo!
Uchaguzi uliopita, niliwahi kumsikia Mzee mmoja wa makamo akimuuliza mtu, " Hivi kwa mfano V wakichukua nchi watatosha kweli kwenye baraza la mawaziri"....Yaani bado kuna kazi ya kuwaaminisha watu kwamba na jinsi gani wana nia ya dhati kuchukua nchi, siasa ni game moja mbaya sana unawezwa kupotezwa sekunde tuuu! Yes cc tunajua kuna watu wanatumiwa, lakini unaweza kuona bado kuna watu wanawasapoti hao wanaotumiwa, na hwa lazima washughulikiwe ili wasieneze hizo sumu kwa watu ambao wakisikia kitu basi wanakibeba kama kilivyo! Bado naamini Slaa anastahili, lakini lazima Chama kishughulikie hawa wapuuzi mapema kwa maslahi wa Watz wengi ambao nina mashaka nao kwenye uelewa wao!
Mimi Nawaza hivyo,