#COVID19 WHO: Usitumie dawa za maumivu (painkillers) kabla ya kupata Chanjo ya COVID-19

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
631
960
Painkillers (2).png

Je, unatumia dawa za kupunguza maumivu kabla ya chanjo ili kuepusha athari (side effects) zake?

Shirika la Afya Duniani (WHO) linaonya kuwa inaweza kupunguza ufanisi wa chanjo.

WHO inasema kuwa athari za kawaida za chanjo kama vile maumivu ya kichwa na uchovu mara nyingi hutokea kwa kiasi kidogo

“Kutumia dawa za kupunguza maumivu kama vile paracetamol kabla ya kupokea chanjo ya COVID-19 kuzuia athari (side effects) zake haifai. Hii ni kwa sababu haijulikani jinsi dawa za kutuliza maumivu zinaweza kuathiri namna chanjo inavyofanya kazi. Hata hivyo, unaweza kuchukua paracetamol au dawa zingine za kupunguza maumivu ikiwa utapata athari kama vile homa, maumivu ya kichwa au maumivu ya misuli baada ya chanjo.” Inasema WHO

Pia shirika linashauri kuwa ni vema kuwasiliana na mtoa huduma ikiwa kuna wekundu au maumivu yanayoongezeka katika eneo ulilochomwa chanjo baada ya masaa 24, au ikiwa athari hizo haziondoki baada ya siku chache.

=====

"Taking painkillers such as paracetamol before receiving the COVID-19 vaccine to prevent side effects is not recommended. This is because it is not known how painkillers may affect how well the vaccine works. However, you may take paracetamol or other painkillers if you do develop side effects such as pain, fever, headache or muscle aches after vaccination." -- World Health Organisation
 
Padri wangu jumapili kanisani alinichekeshaa sana katika mahubiri yake. Alisema "Kwa sasa nchi imegawanyika ktk makundi mawili kundi la kwanza ni lile lililo chanjwa na kundi la pili ni ambalo halijachanjwa. Kundi la waliochanjwa linasubiri ambao hawajachanja WAFE na ambao hawajachanja wanasubiri waliochanjwa wageuke MAZOMBI"mwisho wa kunukuu.
 
Padri wangu jumapili kanisani alinichekeshaa sana katika mahubiri yake. Alisema "Kwa sasa nchi imegawanyika ktk makundi mawili kundi la kwanza ni lile lililo chanjwa na kundi la pili ni ambalo halijachanjwa. Kundi la waliochanjwa linasubiri ambao hawajachanja WAFE na ambao hawajachanja wanasubiri waliochanjwa wageuke MAZOMBI"mwisho wa kunukuu.
Alitisha Padre
 
Back
Top Bottom