Who really killed Prof. Mwaikusa?

Luteni

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
2,274
Reaction score
305
Friday, 16 July 2010 08:31

Fidelis Butahe na Aziza Masoud wa Mwananchi

MTOTO wa Profesa jwan Mwaikusa ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa nje ya nyumba yake, amesema hahusishi mauaji hayo na ujambazi kwa kuwa waliotoa maisha ya baba yake hawakupora chochote.

Magazeti yetu mengine sijui hayana wahariri wakuu?
 
VANgi

Mkuu wakati tunaendelea kuyatafuta majibu ya maswali yote hapo juu, sisi kama Wakristo inatupasa kuachilia damu ya Yesu Kristo ili Mungu aweze kufuta laana kwaajili ya damu iliyomwagika mahali pale, kwa lengo la kutoa laana juu ya nchi dhidi ya damu hiyo.

Hii ni laana na isipofutwa kwa kuachilia damu ya Kristo, Mauaji yataendelea na kuendelea kama ilivyo sasa.
 
Last edited by a moderator:
Wakati mwingine tuchunguze pia maisha ya prof huko nyuma, pengine alitengeneza maadui kutokana na kazi yake, inaweza kuwa ni serikali au watu binafsi all is possible. watu wengi wameuawa kwa style hii, wengine kutokana na dhuluma, wengine kutokana na kujua siri za mambo fulani hivyo kutishia usalama wa kundi fulani n.k

Pengine watu wanaomjua Prof vizuri wanaweza japo kutudokeza..
 

It don't matter nothing. Dude's dead as a doornail, and whoever did it will never be caught.
 
Tuangalie tafsiri halisi ya neno JAMBAZI. Ukishaipata hiyo ndio utaweza kujadili kikamilifu mada hii.
 
Katika taarifa ya ITV saa mbili usiku huu, jeshi la polisi limeeleza kuwashikilia watuhumiwa sita kwa mauaji ya Prof. Mwaikusa
 
Breaking News?

It might have been a News Alert probably - but not Breaking News!
 
Breaking News?

It might have been a News Alert probably - but not Breaking News!
Msemaji wa polisi anasema watuhumiwa wote wamekamatwa Dar es Slaam na Polisi wanaamini kuwa watuhumiwa wanahusika katika mauaji
 
Aisee, kama ni kweli afadhali mkondo wa sheria uchukue nafasi yake na haki itendete.
 
Inanikumbushia mambo ya kina Dumisani Dube,cha msingi ni usikute watu wamepewa kesi ama maigizo bongowood style.
 
Jamaa yangu mmoja ana handle hii issue, walichokosea hawa jamaa walisepa na simu ya mtoto wa Prof, hawajui kwamba ku tract simu ni rahisi mno, halafu wakawa wanaitumia kuwasiliana, so mmoja alikamatwa Dodoma, wengine Mbagala. Prof alikuwa aenda kumfunga mtu Burundi huko kwenye kesi za mauaji ya Kimbari, alikuwa na Doc muhimu sana za hiyo kesi, so jamaa walikuwa wanazitaka hizo doc wakidhani jamaa anatembea nazo kwenye gari kumbe kaziacha ofisini bana. Imenisikitisha sana hii issue Mungu amlaze mahali pema peponi Prof.
 
Kam wamewakamata itakuwa nzuri sana. Wasilete maigizo tu.
 
Asante kwa hii habari. Chimunguru ni kesi ya mauaji ya Burundi au Kwa Kagame wa RPF?
 
Usalama wa taifa una fanya kazi gani?! Inakuwaje watu wageni au kwa faida ya wageni waingue nchini kutenda mauaji bila ya wao kujua!?
 
Aisee, kama ni kweli afadhali mkondo wa sheria uchukue nafasi yake na haki itendete.

Wasiswasi niliokuwa nao tangu mwanzo ni jeshi la polisi kuwa na majibu kati ya haya matatu yaliyotengenezwa
a. majambazi ndio walio husika na mauaji b. wauaji hawajulikani c. mauaji yanahusiana na maisha binafsi ya marehemu, hata kama serikali ya Tanzania inahusika au Rwanda

Suburini, utasikia taarifa ya ajabu ya uchunguzi wa polisi
 
Kwa kweli kama hawa wauaji watakuwa ni wauaji toka Rwanda, Selikali inatakiwa kuchukua uamzi wa kueleweka kabisa, na ikiwezekana, watupiliwe mbali kabisa hata kwenye east africa community, fukuza kabisa hata balozi wao.

Kwa sababu kama mauaji yatakuwa ndo ya aina hiyo ya ICTR tribunal issue, basi selikali ya Kagame lazima itakuwa inahusika....kwa visirani vyao na Wahutu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…