When Did Rushwa become a normality na Wizi ukawa sifa

VoiceOfReason

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
5,194
1,355
Naomba mwenye jibu anijuze... Ni vipi tumefika hapa tulipo sasa.

Rushwa sasa imekuwa kama kitu cha kawaida, wafanyakazi serikalini hawakupi huduma eti mpaka uwape takrima.... Wamegeuza shughuli za umma miradi yao. Hivi hawa Takukuru wapo?

Suala la pili mtu unapopata kazi yenye wadhifa watu wanategemea baada ya mwaka uwe umeiba na kutajirika.... Usipoiba wanakuona mjinga... Utasikia watu wanasema aahh Jamaa mjanja sana yupo kazini miaka miwili tu sasa ana nyumba tatu. Je watu hawa hawajui kwamba huyu mtu ni mwizi au wizi ndio sifa siku hizi.
 
Ingawa ni vigumu kwangu kukumbuka tarehe pamoja na mwaka ambapo rushwa ilianza kuonekana kama utaratibu wa kawaida wakujiongezea kipato,hata hivyo nakumbuka hali hiyo ilianza kujitokeza baada ya watu wengi kuwa na hisia kwamba hata mwenye nyumba anashiriki kwenye mchezo huo.
 
Ingawa ni vigumu kwangu kukumbuka tarehe pamoja na mwaka ambapo rushwa ilianza kuonekana kama utaratibu wa kawaida wakujiongezea kipato,hata hivyo nakumbuka hali hiyo ilianza kujitokeza baada ya watu wengi kuwa na hisia kwamba hata mwenye nyumba anashiriki kwenye mchezo huo.

Kitu kinachosikitisha hii imeshakuwa culture yetu. mtoto anayezaliwa leo na kukulia katika hali hii ya rushwa, just imagine huyu mtu akikua na kuwa kiongozi... kwakweli hali itakuwa ngumu, tulipofika sidhani kama tunaweza kurudi nyuma maadili yamebadilika
 
Zamani Ulikuwa uombwi rushwa ila wewe mwenyewe unatoa ili mambo yako yaende haraka sasa unibidi utoe ili mambo yako yaende au inabidi usahau kushughulikiwa
 
Back
Top Bottom