Tulianza Kwa kuwatoa Ferroviario ya Msumbiji Kwa advantage ya Goli la ugenini hapa tulitoka bila nila kwao tukatoka Moja Moja
Tukaenda Robo Fainali tukamchapa nje ndani Timu ya Manzini ya kule Swatziland
Tukaingia nusu Fainali tukacheza Na Club bingwa ya Angola ya wakati huo inaitwa Atletiko Aviacao hapa Taifa Tukampiga Tatu Kwa Moja then kwao tukapigwa Moja bila wakawa wametoka
Tunaingiza Fainali Sasa hapo, Ikawa Simba vs Stella Andijaa
Mechi ya kwanza tukaanza kule Kwao Ivory Coast tukatoka nao suluhu ya Bila ya kufungana
Sasa Kombe Uwanjani ya Kombe la CAF Africa nzima ikafanyika Uwanja wa Taifa
Mgeni wa Heshma akawa Rais Ally Hassan Mwinyi akisindikizwa Na Waziri wake wa Michezo Prof Philemon Sarungi ( Mshabiki wa Simba damu)
Wakati huo Kocha wa Simba akiwa Abdallah King Kibaden Mputa Na Msaidizi wake akiwa Hassan Hafif
Tukapigwa Goli la kwanza Uwanja Ukawa kimyaaaaa Mara likaingia la pili Mchomo uliopigwa umbali wa mita 18 hapo ndipo Kelele za Mashabiki wa Yanga '...Uzalendo umetushinda...' Ndio zikaanza
Mpaka Mwisho bila ya kutegemea Mzee Mwinyi akashuka Jukwaaani Kwa huzuni usoni lakin akiwa Na furaha moyoni Kwa Kuwa Nae Ni Yanga Damu Kuliko Mzee Akili Mali
Baadhi ya Wachezaji ninaowakumbuka wa Simba Ni Mohamed Mwameja, Hussein Masha, George Magere Masatu, Alfred Kategile, Damian Kimti, Alfred Kategile, Alphonce modest, Makenzi Ramadhan, Dua Said, Edward Chumila n.k
Personally naamini Kwa Umri wangu niliosalia sitoishuhudia Simba bora ya kiwango ile
Mzee Mwinyi akakabidhi Kombe Kwa kina Bolizozo nao usiku ule ule wakaondoka Na Kombe kupumzika Nairobi
Nakumbuka Siku chache kabla ya Mechi, Uongozi Na Mashabiki wa Simba hawakuwa wakijadili Mikakati ya Ushindi wa Mechi hiyo bali walikuwa wakijadili Kombe litakaa wapi baada ya Mechi hiyo wengine walisema Ikulu, wengine BOT hakuna kujadili Mikakati ya Ushindi