What really happened in Simba Sc Vs Stella Abidjan in 1993?

What really happened in Simba Sc Vs Stella Abidjan in 1993?

fuatilia mahojiano ya FIKIRI MOHAMMED MAGOSO, Beki wa SIMBA iliocheza na Stella Abidjan! Mahojiano yanafanyika AZAM SPORTS 2 Jumamosi na Jumapili Saa 1.30 Asubuhi!

Hii Stori naitamani Sana niielewe kiundani wake zaidi. Nawaomba wale wajuzi wa kitu waje kutujuza basi.
 
nakumbuka 1992 au93 marehemu Gulamali alilia badala ya kucheka Yanga walipofanya kweli pale kampala na kubeba ndoo ya cecafa bila kutegemea mdosi akawa ameahidi donge nono kama wangewafunga villa wenyeji kwenye final ambayo zamoyoni mogela alitupia goli 2
azim dewji yeye alizimia kwa mshtuko mechi ya kabla ya fainali akidhani SIMBA haitatoboa to final. (Maelezo haya ni kutoka simulizi ya Fikiri MAGOSO... Beki wa SIMBA iliofika fainali)
 
Simba waliuawa na mtu mmoja aliyeitwa Boli Zozo baada ya kumgeuza kama chapati kwa chenga mlinzi wa Simba Rashidi Abdallah.
 
Tulianza Kwa kuwatoa Ferroviario ya Msumbiji Kwa advantage ya Goli la ugenini hapa tulitoka bila nila kwao tukatoka Moja Moja

Tukaenda Robo Fainali tukamchapa nje ndani Timu ya Manzini ya kule Swatziland

Tukaingia nusu Fainali tukacheza Na Club bingwa ya Angola ya wakati huo inaitwa Atletiko Aviacao hapa Taifa Tukampiga Tatu Kwa Moja then kwao tukapigwa Moja bila wakawa wametoka

Tunaingiza Fainali Sasa hapo, Ikawa Simba vs Stella Andijaa

Mechi ya kwanza tukaanza kule Kwao Ivory Coast tukatoka nao suluhu ya Bila ya kufungana

Sasa Kombe Uwanjani ya Kombe la CAF Africa nzima ikafanyika Uwanja wa Taifa

Mgeni wa Heshma akawa Rais Ally Hassan Mwinyi akisindikizwa Na Waziri wake wa Michezo Prof Philemon Sarungi ( Mshabiki wa Simba damu)

Wakati huo Kocha wa Simba akiwa Abdallah King Kibaden Mputa Na Msaidizi wake akiwa Hassan Hafif

Tukapigwa Goli la kwanza Uwanja Ukawa kimyaaaaa Mara likaingia la pili Mchomo uliopigwa umbali wa mita 18 hapo ndipo Kelele za Mashabiki wa Yanga '...Uzalendo umetushinda...' Ndio zikaanza

Mpaka Mwisho bila ya kutegemea Mzee Mwinyi akashuka Jukwaaani Kwa huzuni usoni lakin akiwa Na furaha moyoni Kwa Kuwa Nae Ni Yanga Damu Kuliko Mzee Akili Mali

Baadhi ya Wachezaji ninaowakumbuka wa Simba Ni Mohamed Mwameja, Hussein Masha, George Magere Masatu, Alfred Kategile, Damian Kimti, Alfred Kategile, Alphonce modest, Makenzi Ramadhan, Dua Said, Edward Chumila n.k

Personally naamini Kwa Umri wangu niliosalia sitoishuhudia Simba bora ya kiwango ile
Mzee Mwinyi akakabidhi Kombe Kwa kina Bolizozo nao usiku ule ule wakaondoka Na Kombe kupumzika Nairobi

Nakumbuka Siku chache kabla ya Mechi, Uongozi Na Mashabiki wa Simba hawakuwa wakijadili Mikakati ya Ushindi wa Mechi hiyo bali walikuwa wakijadili Kombe litakaa wapi baada ya Mechi hiyo wengine walisema Ikulu, wengine BOT hakuna kujadili Mikakati ya Ushindi
Mkuu umesahau Al harach ya algeria
 
Simba waliuawa na mtu mmoja aliyeitwa Boli Zozo baada ya kumgeuza kama chapati kwa chenga mlinzi wa Simba Rashidi Abdallah.
Boli Zozo huwezi sahaulika katika kumbukumbu za wana Simba.
 
Huu ni uongo. Hayo magari walikuja kupewa pamoja na kufungwa ile match. Simba walifungwa sababu ya uchovu walizunguka siku mbili kabla wakiamini ile game wameshashinda.wakawa na uchovu mkubwa sana. Wameingia uwanjani wakiwa wamechoka na kukutana na kipigo.
 
Ilikuwa ni game ya fainali ya kombe la Caf mwaka 93 kati ya Simba Sport Club Vs Stella Abidjan ya Ivory Coast.. Tetesi zilizoenea mitaa ya jiji la Dar WS Salaam na viunga vyake ni kwamba Simba Sc waliuza hiyo game..Wadau wa Soka la Bongo ..What do u think ? Ni kweli Simba waliuza hiyo game ? Kama waliuza nani walihusika na mchezo huo mchafu ?
 
u
Aliahidi gari aina ya KIA kwa kila mchezaji,wachezaji walikua 30,sasa piga hesabu..baniani ikabidi afanye ubaya wake,akatembeza hela kwa wachezaji muhimu wa simba,simba akafungwa kizembe,mzee mwinyi akiwa mgeni rasmi ilimuuma sana,akawaomba wamwingize lunyamila,akaambiwa yule yanga
Uongo mtupu,hakuna aliyeuza game,uwezo uliishia pale hakuwa na la zaidi la kufanya.Wachezaji wa ndani tu na ligi ya ridhaa unachukuaje continental trophy? Miaka 22 baadye ndo timu inacheza final nyingine hamuoni kwamba nyakati zilikuwa bado?
 
Back
Top Bottom