hatukukukaa kimya kama unavyodhania. Tumepeleka malalamiko yetu kwa viongozi wote tuliowachagua yaani diwani, mbunge, wizara et al.
Kama ulikuwa hujui sasa ujue pia kuwa mbunge ni moja ya chombo husika. Moja ya tatizo kubwa la jimbo la kawe ni uvamizi wa maeneo ya wazi na ni moja ya pledge zake mdee kwenye kampeni ya ubunge.
Usijaribu kutetea kutokuwajibika kisa ni mbunge wa CDM.
Kwenye hii thread kuna madai ya ukweli kama unafahamu halima mdee mwambie.
Awe anaonekana jimboni na awe anapatikana.
So far performance yake jimboni kama ya rita mlaki
Mbunge wa CCM wa tarime amepora uwanja wa mpira wa miguu mbezi beach eneo la jogoo. Halima mdee uko wapi?
Wakati mnamsubiri mbunge, mmechukua hatua gani za kulifikisha suala hili katika vyombo husika vya kiserikali?
Mdee bado yuko bize anashughulikia kumsaidia lulu kesi yake na Kanumba. ...maana aliitolea macho kweli yaani
Basi wana Chadema popote pale watakaokuja hapa kulalamikia utendaji wa wabunge wao wa CCM kwenye majimbo yao tuwaulize hilo swali pia!. Utagundua sasa hamna umuhimu wa kuwa na mbunge regardless ya chama anachotoka!
Mbunge wetu Halima Mdee ni mtoro jimboni kwani mara baada ya kumalizika kikao cha bunge la bajeti, hajaonekana jimboni hata ofisi yake pale Kinondoni wilayani, muda wote imefungwa.
Tunashangaa akiwa bungeni ni hodari kuuza sura katika TV huku akiomba miongozo isiyo na tija kwa wapiga kura wake.
Yafuatayo ni matukio ambayo mbunge makini angekuwa karibu na wapiga kura wake, lakini kwa Halima Mdee imekuwa tofauti, akizidi kuwa MTORO kwa wananchi wa jimbo la Kawe:
1. Kushindwa kuwatetea wakazi wa Madale waliogeuziwa kibao na wenye pesa na kuitwa wavamizi wa ardhi ambako nguvu ya ziada imetumika na kuwachomea makazi na mashamba yao.
2. Waislam kugomea Sensa hasa maeneo ya Ununio, Bunju, Boko na Tegeta Kibaoni ; yeye ameshindwa kuwahamasisha wahesabiwe ili waingizwe katika mipango ya maendeleo ya serikali.
Mwisho wana CDM mutoe ushauri kwa Halima Mdee kuwa ubunge ni kazi ya kuwatumikia wananchi wakati wa RAHA na SHIDA inabidi uwe karibu na wananchi.
Mkuu Mwita,
Mtu anamtafuta mbunge wake hamuoni mimi namfahamisha wapi alipo kosa langu nini?
Chama
Gongo la mboto DSM
Mbunge wa CCM wa tarime amepora uwanja wa mpira wa miguu mbezi beach eneo la jogoo. Halima mdee uko wapi?
Mara ya mwisho nilimuona Halima Mdee, kwenye maandamano ya Mwanza amejipamba utadhani anakwend kwenye harusi, unaenda salon kusuka rasta unapaka na rangi ya mdomo halafu unaingia kwenye maandamano, halafu unasema unataka kuwakomboa wana Kawe.
Ritz yaani natamani nikukumbatie wallaih...........wewe Mdee kiukweli kura yangu inaniuma borea lingerudi liRita tu tujue tunaendelea kuumia kulikoa kujipa moyo na matumaini ya mabadiliko halafu hamna kitu!!!!Huyu ni mbunge wangu lakini nashangaa kakimbia jimbo lake, wakazi wa Msasani Mandazi road hawana chochote cha kujivunia kutoka kwa Mdee, wakazi wa Mtongani hawana maji, wavuvi wa Kunduchi mpaka leo wanasubiri soko lao la samaki waliopewa ahadi na Mdee wakati wa kampeni za ubunge, wakazi wa Msasani maeno ya TMJ wanalalamika mitaro hakuna mvua ikinyesha kidogo tu mafuriko.
Non-emotional and Politically unbiased answers only please......
Yupo kawe anahesabiwa ..nenda nyumbani kwake..
Mkuu chama tangu lini umekuwa msemaji wa Chadema?
nasikia sikuhizi kageukia filamu nae anataka kuwa kama WolperMkuu wangu Maundumula,
Umeongea kitu cha msingi sana na chenye ujenzi. kama mambo yenyewe ndio hivyo kama anavyosema "Mang'ana" basi tusitoe lawama kwa mbunge yeyote.