Haahaa,
Sera ya Perostroika na Glasnost kwa mara ya kwanza zilipangwa miaka ya 60's hata Gorbachev hafahamiki.
Ukiangalia vizuri sera za Uchumi za Nikita Kruschev utaona kuna chembe-chembe nyingi za Glasnost na Perostroika.
Kilichovunja SOVIET UNION kilikuwa ni mkataba ambao unaitwa (the Belavezha Accords) ambao ulisainiwa kisirisiri na viongozi wa Ukraine, Belarus na Russia.
Ikumbukwe kwamba mwaka 1991 kuna mapinduzi yalifanyika ya kijeshi ili kuwaua viongozi wote wa USSR pamoja na Gorbachev ili kuzuia muungano usivunjike. Lakini Yeltsin aliwazuia wale wanajeshi basi muungano ukavunjika.
Ukweli ni kwamba hata viongozi wa KGB walijua kabisa kwa Uchumi ulivyoharibika, mfumo wao wa uongozi na rushwa ndani ya USSR ni lazima wangekuja kushindwa vibaya siku za mbeleni.
So wakaamua kujipanga upya ndiyo unawaona hadi leo tena.