Wezi wa simtank mbele ya mahakama ya wananchi

Wezi wa simtank mbele ya mahakama ya wananchi

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,965
Reaction score
831,512
1415887884098.jpg
 
kha! nakwambia wakipona hapo hawarudii
 
Huu ni udhalilishaji wa binaadam.

Wangeshikwa wakabebeshwa hilo tank na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria lakini si kuwachwa utupu.
 
Huu ni udhalilishaji wa binaadam.

Wangeshikwa wakabebeshwa hilo tank na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria lakini si kuwachwa utupu.

Ni kweli na hata mi naona kwa mbali wale jamaa wa bakari kichwa wazi ni huzuni na kicheko
 
Wangeshikwa wakabebeshwa hilo tank na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria lakini si kuwachwa utupu.
Wangewabebesha tank lakini wasiwavue nguo?

Huna hatia mpaka utakapothibitishwa vinginevyo kwenye chombo cha sheria maana yake hata kitendo cha kumbebesha tank ina maana tayari umeshamhukumu! Kwa nini nibebe tank na mimi sijaiba?

Na kuna sababu.

Prosecuting attorney akiipitisha mahakamani picha ya mtumiwa kama kielelezo cha utambulisho wake, akiwa kabeba Sim tank anaelekea polisi hii psychologically ina affect mind ya mtoa haki, hakimu ama wazee wa baraza n.k. kwamba hawa jamaa kwa kiasi fulani wanakiri kosa kwa kubeba tank wenyewe, kumbe wamebeba kwa hofu mbele ya fimbo na mawe na mafuta ya taa. Tuzidi kujizatiti katika utawala wa sheria ambao kwa kweli bado ni dhana za kigeni kwetu.
 
Dawa yao ndo hiyo .wanao ona waogope wakipelekwa kwa vyombo vya sheria wanarudim
 
Wangewabebesha tank lakini wasiwavue nguo?

Huna hatia mpaka utakapothibitishwa vinginevyo kwenye chombo cha sheria maana yake hata kitendo cha kumbebesha tank ina maana tayari umeshamhukumu! Kwa nini nibebe tank na mimi sijaiba?

Na kuna sababu.

Prosecuting attorney akiipitisha mahakamani picha ya mtumiwa kama kielelezo cha utambulisho wake, akiwa kabeba Sim tank anaelekea polisi hii psychologically ina affect mind ya mtoa haki, hakimu ama wazee wa baraza n.k. kwamba hawa jamaa kwa kiasi fulani wanakiri kosa kwa kubeba tank wenyewe, kumbe wamebeba kwa hofu mbele ya fimbo na mawe na mafuta ya taa. Tuzidi kujizatiti katika utawala wa sheria ambao kwa kweli bado ni dhana za kigeni kwetu.

Mimi si mwanasheria lakini nimeona wako utupu na hilo ndilo nimeona kuwa ni udhalilishaji wa binaadam.
 
Ndio Tanzania hiyo, ukiiba simtank upate hela ya kula ugali utapigwa, uvuliwe nguo, udhalilishwe na kuuwawa. Lakini wezi wa mabilioni ya wananchi wananyenyekewa na kuabudiwa kama miungu.
 
Tatizo sio kufikishwa kwenye vyombo ila wakifikishwa kwenye dola wanaachiwa kesho yake.wanarudi kuiba...hawa vibaka wanfanya mambo mabaya.sana
 
Natamani mafisadi kama El,chengge,le profeseli, wafanyiwe hii kitu sio kuonea hawa dagaa!
 
Mimi si mwanasheria lakini nimeona wako utupu na hilo ndilo nimeona kuwa ni udhalilishaji wa binaadam.
Sawa kabisa, lakini baada ya kuliongelea hilo la kudhalilishwa kwa utupu hukuishia hapo, uka advocate abebeshwe tenki. Halafu unasema wewe sio mwanasheria. Ukisema, kwa mfano, mafuta ya mkunazi yanatibu Ebola, ukaambiwa unapotosha jamii, huwezi kujibu "mimi sio mganja."

Unapombebesha mshutumiwa Sim tenki unampoka haki yake ya kutokuwa na hatia mpaka atakapothibitishwa vinginevyo, hata ungemvisha tai.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom