Wewe ni nani? Swali gumu sana

Wewe ni nani? Swali gumu sana

Ubishe wenu hatutoweza kuelimishana poa eendeleeni na mabishano
 
Hili swali huwa linaulizwa sana sana kwenye interview mbalimbali. Ila ninachojua mimi ni kwamba unatakiwa kutoa historia yako kwa ufupi. Kutoka ulikozaliwa, historia ya elimu yako, kazi ulizowai kufanya, ulipo kwa sasa, madhaifu yako pamoja na mazuri yako. Ni mtizamo wangu tu.
OVER
 
Im Tycoon for Life, Field Marshal Al Hadji Professor Amalinze The cat my back never touch the ground, VC, DSO, MC, Lord of All the Beasts of the Earth and Fishes of the Seas and Conqueror of the British Empire in Africa in General and Tanzania in Particular"
We kiboko nimecheka karibu waite ambulance. Duuu hatareee
 
Wewe ni nani?
Ni swali ambalo ukiulizwa unaweza kuliona rahisi sana na kulijibu haraka haraka Kwa kutoa jibu linalotaja jina lako. Mimi ni James, ama Mimi ni Janeth!! Lakini ni ukweli ulio wazi kua wewe si jina lako. Wewe ni zaidi ya jina lako.

Ama unaweza kujibu kwa kutaja kazi yako, wewe ni nani? Ukajibu, mimi ni Mkurugenzi wa Masoko wa CRDB, mwingine atasema mimi ni Mbunge au mimi ni Waziri, ama mimi ni Mwalimu. Lakini ukweli ni kwamba wewe si kazi yako, wewe si cheo chako. Wewe ni zaidi ya kazi yako. Na kazi yako sio wewe.

MIMI NI NANI?
Naweza kujibu hivi.
Mimi ni mimi duniani kote, nipo mimi mwenye mawazo ya aina yangu, Hakuna mwingine kama mimi, Nikifa. Akizaliwa mwingine akapewa jina langu, atakua mwingine mwenye jina langu. Mimi hana mbadala ila kuna mwingine atakayefanya niliyofanya. Mimi hawezi kua ndani ya mwingine popote, kabla yangu na baada yangu.

Je! Wewe ni Nani?
Kwa mfano unagonga mlango halafu mtu wa ndani akakuuliza wewe nani? Je utatakiwa umjibu vp?
 
Roho inajitambua kuliko mwili, roho inayohisia kuliko mwili, Roho Ina macho yanaona vizuri kuliko ya mwili, Ina masikio,Ina nguvu kuliko mwili,
ningeuliza roho ikoje/inasifa zipi ungenijibu hivi lkn nimekuuliza unawezaje kuihisi roho...?
 
mtoa mada if you had a right answer could be better come up for the answer......coz umesema ni sehemu ya kufundishana, but lastly no clear answers. what is your intention to convince or confuse? thus y you got confused replies.....
 
Mbona sio swal gumu ndo mana hat wew umewez kuliuliza.Labda jibu ndo linaweza kuwa gumu
 
Swali gumu sijapata ona, àsilimia 99.9 ya watu hawajijui wao ni akina nani
 
Back
Top Bottom