SHIEKA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,244
- 4,258
Nikiwa mtumiaji mkubwa wa usafiri wa daladala mkoani Kilimanjaro nilianza kulisikia hili neno likitumiwa sana na makondakta wa daladala. Nilisikia sana usemi huu: "Haya, panda fasta wale wa Kwa Sadala, Boma mpaka Sanya. Fanya fasta!"Hii ilikuwa mwanzo mwa miaka ya 2000 - 2002 - 2005 hivi.Nikawaza: eee! hiyo fasta ndo ana maana gani? Kwa nini asiseme tu "panda haraka?" Nikajua hawa watu wanataka kuonesha kuwa hata wao ung'eng'e upo! Sasa hivi hili neno fasta limeshamiri sana kila mahali - hata hapa JF hutumiwa sana. Si la Kiswahili wala kiingereza ila kwa kweli ni kiingereza kibovu - tena sana. Maneno 'haraka' au 'upesi' yameshapewa likizo na neno fasta kuingia kazini! Mimi naona huu ndio mwanzo wa kuua lugha yetu ya Kiswahili. Au mwaonaje wadau?