Wenye nyumba za kupangisha walipe kodi

Wenye nyumba za kupangisha walipe kodi

mtoa post kama ulidhani utamkomoa mwenye nyumba wako,jua we we ndiye utakayeumia tu!/
 
mtoa post kama ulidhani utamkomoa mwenye nyumba wako,jua we we ndiye utakayeumia tu!/ MAUMIVU KWA MLAJI WA MWISHO!
 
Watu kama hawa sio wakuwapa nchi,anakurupuka tu without to assimilate the situation he just implement, idiot, miss chagga huyu atakuwa anakaa kwa wazazi wake,
kabisa mkuu na hajui hata gharama za kupanga
 
Kwa serkali hii ya JPM ambayo inaleta matumaini kuwa kodi zetu zitatumika vizuri, nipo tayari hata kesho kulipa kodi kwa vibanda vyangu ninavyopangisha
 
wenye nyumba tayari wanalipa kodi za ardhi, sio kwamba wanapata kipato bila kulipa kodi!

Havina uhusiano. Hata mwenye nyumba ambaye hapangishi analipa kodi ya ardhi. Hapa inazungumziwa pato la kupangisha nyumba. Kila pato lazima likatwe kodi. Hakuna namna nyingine.
 
Hahaha unadhani umemkomoa mwenye nyumba?

Yeye akitozwa kodi mwenyewe anapandisha tu kwa hiyo burden ya kodi inakupata wewe mlaji (mpangaji)
 
Natoka nje ya mada....



Hatari xana watu mnaharaka ya kuelewa mm nmemuelewa jaamaa vizur tu,Ni kweli kuna kodi ya ardhi na nilazima wananchi walipe,lakin kwann jumba ya kupangsha mwenye Nyumba alipa maana yake Nyumba yake kaifanya biashara xo kodi anayolipa pale ni ya biashara na si vinginevyoo.

Humo ulipoweka "x" ungeandika "s" ungepungua kilo???
 
Havina uhusiano. Hata mwenye nyumba ambaye hapangishi analipa kodi ya ardhi. Hapa inazungumziwa pato la kupangisha nyumba. Kila pato lazima likatwe kodi. Hakuna namna nyingine.

unaijua property tax inavyofanyiwa evaluation au unajua kodi ya ardhi tu. Walete tu tutapandisha kodi ya nyumba huwezi hama
 
wenye nyumba tayari wanalipa kodi za ardhi, sio kwamba wanapata kipato bila kulipa kodi!

Huenda mtaani kwao ndio hawalipi maana mitaa mingine licha ya kulipa kodi ya ardhi wanalipa property tax pia ambayo ni 3% ya thamani ya nyumba kwa nyumba za kupangisha kwa makazi, 2% nyumba anayoishi mwenye nyumba na 6% nyumba zilizopangishwa kwa biashara kama maduka, mahoteli nk
 
Wenye nyumba za kupanga wanatakiwa walipe kodi. Na hili tunamwomba Rais wetu, waziri mkuu, kamishna wa tra mliangalie hili kwa umakini mkubwa sana. Watu wanatupangisha kwa dola lakin hawalipi kodi. Ukienda masaki mbez beach sinza mikocgen tabata kimara kariakoo uoanga watu wanalipa kwa dola lakin tra hawachaj kodi. Angalia frem za kariakoo watu wanalipa.mpaka usd 2000
Lakin tra hawachukui kodi. Kama kweli Rais ana nia ya dhat ya kukusanya kodi basi.aangalie na eneo hili kuna pesa nyingi sana.
 
Havina uhusiano. Hata mwenye nyumba ambaye hapangishi analipa kodi ya ardhi. Hapa inazungumziwa pato la kupangisha nyumba. Kila pato lazima likatwe kodi. Hakuna namna nyingine.

Kuna maeneo ambayo tayari yamefanyiwa evaluation wanalipa Property Tax ambayo ni 2%,3%na 6% ya thamani ya nyumba kwa nyumba binafsi, nyumba iliyopangishwa kwa ajili kuishi na nyumba iliyopangishwa kwa ajili ya biashara kwa huo mfuatano, hizi kodi zinakusanywa na halmashauri
 
Ni heri umuelimishe huyu jamaa, hajuwi hata hilo kama kuna land rent,ni ujinga tu analeta, hajosoma hata uchumi amabapo ungemsaidia,.
Wanalipa
1.Land Rent(Kodi ya Ardhi
2Property tax(kodi ya jengo)
3.withholding Tax(kodi ya pango)
 
unaijua property tax inavyofanyiwa evaluation au unajua kodi ya ardhi tu. Walete tu tutapandisha kodi ya nyumba huwezi hama

Property tax ni kama haipo Tanzania. Nani wa kumvita paka kengele? Wakubwa wana majumba kila kona ya nchi na wasingependa walipe property tax.

Kwa nchi zilizoendelea na zenye uchumi wa kati, property tax ni chanzo kikubwa cha mapato ya serikali. Property tax hutegemea thamani ya jengo au nyumba. Kukiwa na mipango mizuri, ni vigumu kukwepa kodi hii.
 
Akili nyingine bure kabisa! Tangu lini kodi ikalipwa na mfanyabiashara? Huyo atakuwa mkusanyaji tu, hiyo kodi mtalipa nyinyi mnaohamahama na sofa za bei mbaya wkt nyumba hamna.
 
Sheria ya kodi ya mapato ko wazi. Kama unapata kipato cha aina yoyote hata ya kutokana na pango lazima ulipe kodi. Hii no tofauti na land and property tax ambazo unazilipia hata kama unaishi katika nyumba yako mwenyewe.
 
Maadamu kile anachopata kwa mwezi kinazidi kima cha chini cha mshahara lazima alipe kodi kwa sababu ana kipato!!!

Wewe unaona tu kipato anachopata baada ya kujenga, Unajua ni kiasi gani alitumia kuwekeza hapo?

Unajua ni muda gani atachukua arudishe pesa ya ujenzi ndio aanze kupata faida?

Au unataka atumie mtaji kulipa Kodi?
 
Back
Top Bottom