Wenye nyumba za kupangisha walipe kodi

Wenye nyumba za kupangisha walipe kodi

Wewe unaona tu kipato anachopata baada ya kujenga, Unajua ni kiasi gani alitumia kuwekeza hapo?

Unajua ni muda gani atachukua arudishe pesa ya ujenzi ndio aanze kupata faida?

Au unataka atumie mtaji kulipa Kodi?

Ni matakwa ya sheria tu. Labda tuombe ibadilishwe.
 
Hivi biashara ya nyumba inalipa? Naona kama gharama ya ujenzi ni kubwa sana.
 
Hahahaha kodi zote ni burden kwa mwananchi. Ungefafanua unalenga kundi lipi. Kuna ma-landlords wanapangisha tena kwa dola na mkataba unaingiwa kati ya mpangaji na mwenye nyumba. Kodi hailipwi. Maelezo uliyotoa ni sawa na kuhimiza wenye maduka wasitoe risiti kwa kuwa unanufaika kwa kulipa gharama ndogo. Hatuwezi kufika. Wafanyakazi ndio wanaokamuliwa haswaa kwa PAYE. Halafu baba mwneye nyumba wako halipi kodi. Noway!!!!

Tunahitaji kurasimisha biashara zote ili kila mtu alipe kodi stahiki. Hatuwezi kulilia huduma bora huku tunashiriki No kulinda baadhi ya makundi ya kijamii yasilipe kodi.

No stone should remain unturned!

Dah!
Siungi mkono hoja, lengo kuu la serikali ni kuboresha na kushusha gharama za maisha kwa wananchi. Watanzania wengi hatuna nyumba bado, tumepanga! Wakitozwa kodi, wananchi wa kawaida ndo tutakuwa tunalipa. Wataongeza kodi!
 
Wenye nyumba wanalipa property tax Na hii haijalishi Kama in nyumba ya kupangisha au unakaa were mwenyewe. Kwa wale ambao nyumba ziko kwenye viwanja vilivyopimwa Na wana hati, basi wanalipa pia land rent. Kwa kipato cha kupangisha nyumba, ni vyema wakalipa kodi kidogo serikalini.
 
Mbona kodi tunalipa sana tuu, hata nyumba za makazi tunazilipia ila tozo yake inatofautiana na nyumba za kupanhisha
 
ukiona wenye nyumba wanafaidika sana na wewe kajenge yako upangishe, serikali ikilipisha kodi na mwenye nyumba anapandisha huwezi rudi kijijini kwenu!

Hii ni kauli ya MTU anayeishi mahali Fulani hivi uswahilini!!!!!!
 
Back
Top Bottom