Wenye LINE nyingi za simu mnakera sana..!

TheChoji

JF-Expert Member
Apr 14, 2009
4,975
15,316
Binafsi nakerwa sana na watu wenye "line" lukuki za simu. Unakuta mtu ana line ya voda, tigo, airtel, zantel nk. Zote izo za kazi gani?? Matokeo yake kila ukimtafuta mtu utasikia mara..

"Nicheki kwenye airtel hiyo Voda haina chaji.."

"Nipigie namba ya tiGo, airtel nimeacha nyumbani"

"Hela umetuma mpesa? Aaargh hiyo line siko nayo sasa mpaka nirudi home.."

"Namba iliopo WhatsApp ni ile ya Zantel.."

" Unasemaje sijakupigia, kwani hukuona namba ya tiGO imeku miss call..?"

"Mimi si ndio nilikupigia kwa namba ya TTCL, mbona hujapokea.....?"

Jamani..! Mimi nnaposave namba yako, nasevu kwa JINA sio kwa mtandao uliopo. So ata sijui namba ya zantel inafananaje?

Ukiniambia nikucheki airtel yaani unanipa kazi ya ziada kuanza kutafuta namba za airtel hua zikoje ndio nijue ni ipi?

Mi nachoka sana..
 
Si ajabu wewe ndio tukushangae kwa nn hutaki kuendana na uhalisia wa mitandao yetu bongo,Binafsi nina laini zote na kila moja hua inakua na msaada wake tu kwa wakati usiotegemea ,Kampuni hiz zisizo na usawa bora wa huduma afu niwe na laini moja? Siwezi
 
Si ajabu wewe ndio tukushangae kwa nn hutaki kuendana na uhalisia wa mitandao yetu bongo,Binafsi nina laini zote na kila moja hua inakua na msaada wake tu kwa wakati usiotegemea ,Kampuni hiz zisizo na usawa bora wa huduma afu niwe na laini moja? Siwezi
Mimi nna laini 1 ya voda nilinunua mwaka 2000 na sijawahi kuwa na laini nyingine wala sijawahi kubadilisha namba. Mbona sijapata shida yoyote? Nyie mnachokitafuta kwenye kila mtandao ni kitu gani hasa?
 
Sababu kubwa ya hii mitandao mingi ulaji mkubwa wa data hauendani na matumizi ndio mana watu wamekuwa wanahama kila siku nimetumia tigo,voda nikahami halotel mitandao yote hii data zinakata fasta sasa nipo na Airtel naona wanaunafuu
Sasa ukiwa na line zote hizo mtu anakutafuta vipi, au mtu atajuaje saizi upo mtandao gani.? Na je kila ukihama mtandao ina maana na watu wote unawaambia sasa nimehamia airtel au unawaacha kule voda?
 
Mimi huwa nasave namba moja tu ya mtu. Mimi mwenyewe nina simu moja tu yenye line 2 tu. Sitaki masimu mengi mengi.
 
Mimi nna laini 1 ya voda nilinunua mwaka 2000 na sijawahi kuwa na laini nyingine wala sijawahi kubadilisha namba. Mbona sijapata shida yoyote? Nyie mnachokitafuta kwenye kila mtandao ni kitu gani hasa?
Huwa kwenye mishemishe zako unaendaga mikoani? Hivi unajua Kuna maeneo hapa hapa nchini Voda haikamati mpaka uwe na Halotel?
 
Back
Top Bottom