Wenye akili CHADEMA wapo kimya

Wenye akili CHADEMA wapo kimya

Ni Lazima niseme ukweli kuwa CHADEMA imeyumba mno na kama jitihada za makusudi hazijafanyika basi hiki chama kinakufa rasmi.

Haya Madudu ya akina Mbowe yanayoendelea kuanikwa na kutolewa utetezi usioeleweka yananifanya mimi niliyekuwa naichukia CCM nianze kutafakari upya kwani kwa sasa SIONI TOFAUTI YA CCM na CHADEMA (na huenda CHADEMA wanaweza kuwa hatari zaidi).

Nimefuatilia kiasi kauli za wabunge wa CHADEMA [ambao ndiyo wanafahamika sana] wakiongea kuhusu swala la Kitila, ZZK, Mwigamba -kwa kweli nimesikitika sana. Nimesikitika kwa kuwa mwanzoni niliwaona wabunge hawa kuwa vichwa ila kwa sasa nawaona viumbe hatari sana.

Ukiachilia mbali mbunge Lema ambaye yeye amekuwa haeleweki vema kwenye baadhi ya kauli zake kwa muda mrefu sasa, Mnyika, Mch. Msigwa na Lissu kwa kweli wameharibu CV zao vibaya mno kwa utumbo waliouongea kuhusiana na mgogoro unaofukuta Chadema. Sikuamini mtu kama Mnyika, Msigwa na Lissu wanaweza ku-support udikteta wa akina Slaa na Mbowe (na wengine wote) wa kuwaona wahaini watu ambao wanamawazo mbadala wa namna ya kumpata kiongozi wa chama. Mnyika ndo niliyekuwa namwamini sana lakini naye kajitosa kwenye siasa za ki-imla hata sijui kwa sababu gani.

Naomba nichukue fursa hii kuwapongeza wabunge na wanachama mahsusi wa Chadema ambao at least wameonyesha akili kwa kukaa kimya.

Ndiyo, pamoja na kwamba kukaa kimya wakati madudu yanaendelea ni unafiki, lakini ni heri ukae kimya uonekane una-akili kuliko kuongea ku-support madudu. Pongezi hizi ziende kwa Mbunge Joshua Nassari, Mbunge Halima Mdee, Wakili Mabere Marando, Prof. Safari na wengine wote ambao wamesahaulika wakati wa kutoa maoni haya.

UPDATES

Wakili Mabare Marando na Prof Safari nimewatoa rasmi kwenye list ya kupongezwa baada ya kusoma gazeti la Mtanzania wakisema wanaunga mkono maamuzi ya kamati kuu ya Chadema kwa maamuzi yaliyofanyika dhidi ya wale wanaoitwa wahaini. Vituko havitaisha Tanzania!


Chadema hawezi kuwa mtu kama wewe.Kama hukuweza kuona ujinga wa Zitto kuazia miaka kadhaa na mwenendo wake ndani ya Chama kuweka makundi more than 2 times akina Shonza , mikoani leo kundi la Kitila na hata kuhamishia ofisi facebook basi una akili ndogo sana .Wabunge wanao ongea wana mandate ya kufanya hivyo ndani ya Chama sasa ukitegemea kilamtu aongee wakati ile ni taasisi ?
 
Wengi tumekuwa disapointed na Uongozi wa chadema. Inawezekana hawa watu walikuwa na makosa ila kwakuwa chama ni cha wanachama sisi nasi wanachama wa kawaida tulipswa kujuzwa huo usaliti, uhaini nk ambao hawa ndugu wamehusika nao. ukifuatilia kwa ukaribu utaona hakuna sababu ya msingi ambayo imeshatajwa yenye mashiko ya kuitwa Uhaini/usaliti ni visingizio tu. Waraka wenyewe huo hauna hata chembe ya uhaini.

Ati hupaswi kuwa na mpango wako kama mwanachama wa kuweka mikakati ya ushindi kama una nia hio, ati uujulishe uongozi nia yako na mkakati wako. Huu ni ujuha, hivi kweli Slaa/Mbowe hawana wanachopanga vichwani mwao kuhusu nafasi zao hapo mbeleni. Kupanga kichwani na kuandika tofouti yake nini? Huu ni Unafki.

Basi tunaimbishwa tuu wimbo wa uhaini bila ya kujiuliza upi huo!
 
Sawasawa kabisa, hata uliyoyaandika hapo juu nayo ni kwa mujibu wa mtazamo wako. Kumbuka kuwa akina ZZK, Kitila na Mwigamba walivuliwa nafasi zao za uongozi ndani ya chama KABLA hata ya kupewa nafasi za kusikilizwa. Na kwa maana hiyo na MBOWE inatakiwa afukuzwe kwenye nafasi ya uongozi bila hata ya kusikilizwa baada ya KASHIFA nyingi dhidi yake KUIBULIWA. Nionavyo mimi kashfa ya Mbowe ni kubwa kuliko hata ya akina ZZK ya kupanga mkakati wa kugombea uongozi -kwanza hii haifai hata kuitwa kashfa labda kwenye chama kama CHADEMA chini ya utawala wa Mbowe.

Ni matarajio yangu kwamba kama bado kuna watu wana busara ndani ya uongozi wa CDM wamshauri Mbowe ajiondoe ktk uongozi wa chama. Lakini wapendekeze mabadiliko makubwa ktk CC ya chama. Ya sasa imechafuka sana.

Kama chama kitaingia ktk uchaguzi na uongozi huu tuhesabu aibu ya mwaka. Maisha ya siasa na uungwaji mkono kwa chama ambacho nilizoea kuita chama changu cha CDM hayataendelea kuwa kama kabla ya mgogoro huu! Naungana na mkuu Kiranga kwamba kuna mengi ya aibu yaliyo fichwa yanakuja!

Mimi naamini kama ni kwa mapenzi ya Mungu basi ametufunulia pazia aina ya watu ambao walikua wanajiandaa kuingia Ikulu. Ni wakati wetu kuisafisha CDM bila kuangalia jina,sura wala ukongwe wa muhusika. Tuhuma ambazo zimerushwa kwa Mwenyekiti Mbowe siyo ndogo wala kunyamazia kuchukuliwa hatua.
 
Chadema hawezi kuwa mtu kama wewe.Kama hukuweza kuona ujinga wa Zitto kuazia miaka kadhaa na mwenendo wake ndani ya Chama kuweka makundi more than 2 times akina Shonza , mikoani leo kundi la Kitila na hata kuhamishia ofisi facebook basi una akili ndogo sana .Wabunge wanao ongea wana mandate ya kufanya hivyo ndani ya Chama sasa ukitegemea kilamtu aongee wakati ile ni taasisi ?

Wewe mwenye akili nyingi sana kwa nini hukujiuliza toka mwanzo kwa nini hayo makundi (unayodai yalikuwepo, Pamoja na kwamba najua ni stori za mitaani) yatokee? Huoni kuwa ZZK alianza kupambana na udikteta wa akina Mbowe na Slaa muda mrefu? Na kwanini hayo unayoyasema (ya akina Shonza) HAYAKUINGIZWA KWENYE LIST YA MAKOSA ALIYOPEWA ZITTO? umesoma kweli wewe makosa yaliyoandikwa na akina Slaa dhidi ya ZITTO? Kinachonishangaza na nyie wapenzi wa Chadema ni kuwa karibu wote mnadhani ZZK ndo tatizo na kusahau wanaoiua demokrasia ya kweli ndani ya chama.

Nenda ukasome katiba ya chama chenu ujue mwenye mandate ya kuongea ni nani? Naona umeanza kuchanganya mambo kwa makusudi ili kuupotosha umma wa Jamii forum. It reaches a point when you need to accept challenges for your own benefits.
 
utaonaje utofauti kati ya Chadema na ccm wakati hujitambui, unaota ndoto za mchana eti Chadema itakufa, kweli kuwa gamba lazima ujitoe ufahamu, na mwenzio Zitto alijitoa fahamu magamba yakamgambalize, sasa amekuwa kimeo kila kona hatakiwi, haya aliyoyafanya Zitto hata mkeo au mpenzi wako analaani, kama huamini mwambie siku moja akupe mtazamo wake bila unafiki, utapata jibu, wanakutumia vibaya, amka ndugu, watanzania wa leo hatuko hivyo, wasaliti wote sio muda mtaiona nchi chungu hii, na hao wanaowatumia hamtawaona tena, shauri yako.
 
CHADEMA is a time bomb waiting to explode!.

Chama kilisimama kwenye misingi ya ulaghai na kuwaaminisha wananchi kuwa wao ni wapiga vita ufisadi na wakombozi wa wananchi but little known kuwa wao ndiyo walikuwa ni catalyst wa ufisadi kwa sababu chama kilikuwa kinaendeshwa na pesa za 'mafisadi'.

Nilipomuona Mabere Marando na yeye ameingia kwenye majukwaa ya siasa ya CHADEMA akipiga vita ufisadi wakati yeye ni wakili wa mafisadi, basi nikafamu kuwa timer ya bomb la ulaghai wa CHADEMA iko on.

Huu ni mwanzo tu wa mlipuko wa bomu na wajiandae kisaikologia kwa yanayokuja huko mbeleni.

Kama JK alivyosema, watu wajiandae kisaikolojia
 
msaliti ni mbowe,mmedanganywa kura ziliibiwa kumbe watu wamepiga pesa za mafisadi kama hii haijawavunja moyo kwenye siasa nitawaita majuha

Ni majuha tayari......yaani kwao kinachotamkwa na Mbowe ndicho wanaelewa.....akisema Zitto ni msaliti haibadiliki tena mpaka hapo atakapotamka kuwa yeye (Mbowe) ndiye msaliti............ndio (majuha) wataitikia kwa vichwa wakisema.........anhaaaaaa.....
 
Siwezi kuipenda CCM eti kwasababu CDM wanarushiana maneno,yanayoendelea ndani ya CDM sio yanayosababisha umaskini wa Watanzania,yanayoendelea CDM sio yanayosababisha hati chafu kwenye halmashauri,mzozo wa CDM sio unaofanya mama wajawazito walale chini kule Mahospitalini...........kinachoendelea CDM ni kati ya wasaliti na wenye mioyo imara.........Nitaipenda CCM siku wakiweka maslahi ya Mtanzania mbele na mafisadi wote kwenda kwenye makazi yao kule Segerea na Ukonga au pengine penye hadhi hiyo.
 
Mlisema Zitto akifukuzwa chadema kitakufa, zzk alipokuwa kigoma mkasema zitto ameimaliza chadema, sasa mbona mmemtuma mahakamani kama kweli mlikuwa mnataka chadema kife kwa kumfukuza zzk? na huko mahakamani nasikia mnaandaa utaratibu fulani hivi ili jamaa at least uanachama wake uendelee kubaki ICU
 
sio lazima kama hauna cha kupost na wewe upost!kama jina lako lilivyo!!!
 
Wewe mwenye akili nyingi sana kwa nini hukujiuliza toka mwanzo kwa nini hayo makundi (unayodai yalikuwepo, Pamoja na kwamba najua ni stori za mitaani) yatokee? Huoni kuwa ZZK alianza kupambana na udikteta wa akina Mbowe na Slaa muda mrefu? Na kwanini hayo unayoyasema (ya akina Shonza) HAYAKUINGIZWA KWENYE LIST YA MAKOSA ALIYOPEWA ZITTO? umesoma kweli wewe makosa yaliyoandikwa na akina Slaa dhidi ya ZITTO? Kinachonishangaza na nyie wapenzi wa Chadema ni kuwa karibu wote mnadhani ZZK ndo tatizo na kusahau wanaoiua demokrasia ya kweli ndani ya chama.

Nenda ukasome katiba ya chama chenu ujue mwenye mandate ya kuongea ni nani? Naona umeanza kuchanganya mambo kwa makusudi ili kuupotosha umma wa Jamii forum. It reaches a point when you need to accept challenges for your own benefits.

Ni kwelu kabisa kwa sasa we have to accept challenge for our own benefit.
Kama sasa hivi nimeanza kufuga nguruwe ili tembo watakapoisha huko porini nitaikodishia serikali hawa nguruwe wawapeleke huko ngorongoro, mikumi, serengeti n.k ili watalii wakija wangalie tembo wa siku hizi.
We have to accept challenge.
Umeme umepanda bei sasa tufanyeje?? Tuihujumu tanesco kwa kuiba umeme, Challenge!!
 
Watanzania wengi hawajui yaliyo nyuma ya pazia. Z msaky relationship, msaky chemba relationship, ugaidi wa rwakatare. Mnajua who is behind Soweto Arusha bombing? Mnajua sababu ya Z kukwepa sana Ars? Jaribuni kuona mbali zaidi ya urefu wa pua zenu.
 
Nadhani mtoa hoja tungekupongeza sana kama ungekuja na njia mbadala ya kushugulikia chanzo cha mgogoro ndani ya CHADEMA; ambao kila mmoja anatambua kuwa ni "usaliti" wa ndg Zitto ndani ya chama.

Wewe kama mtu mwenye akili, weledi na busara ni vizuri kushauri bila upendeleo ili kukinusuru chama; ila ni wazi kabisa kwamba dawa pekee ya usaliti ni kutimua.

Huwezi kuvumilia pale unapo hujumiwa. Ushahidi wa kutosha uko wazi jinsi Zitto alivyo tumiwa na wabaya wa CHADEMA ili aue chama.

Kama naye alikuwa na tuhuma dhidi ya Mbowe, mbona kakaa kimya siku zote aje kufunguka leo baada ya kuchinjiwa baharini? Si angeongea mapema akiwa bado na heshima zake ndani ya chama ili watu wamwelewe na kuchangia hoja?

Kumbukeni Zitto analeta janja ya kuku kuwa na nguvu nyingi z kutaka kuruka na kukimbia mara tu akishakatwa kichwa.

Mkuu, chama ni kama ndoa, ili ujue maovu ya pande zote ni pale tu wanandoa wanapotengana, otherwise for good for bad. Utaanza kusikia nilikuvumilia sana, nilishakufumania nikakaa kimya, jitu lenyewe jizi, malaya etc. Kuna hadi kusingiziana kwamba mtu mwenyewe husimamishi.

Sasa hapa ni akili za kuambiwa, tuchanganye na zetu.

Swali kwako: Kwa sababu Zitto kayasema sasa na si huko nyuma, na kama mambo yenyewe ni ya kweli, je ni makosa au sio makosa? Mbowe ajibu au asijibu?

Kama alivyosema Kiranga kwenye no 5, hili ni jiwe tu, rungu litafata, then panga, mshale, bunduki, bomu, gurunet, silaha za maangamizi ni mwishoni kabisa.
 
Last edited by a moderator:
ZZK tangu chuo UDSM alikuwa na silka za namna hiyo, walokuwa kwenye siasa za chuo 2002/3 wananielewa.The guy is over confident and that is self destructive.Anaona anaweza kumchalenji yeyote na popote na vyovyote.Lkn anasahau shingo haiwezi kuzidi kichwa.Wazee alowakuta CDM wakamlea wakampa fursa akawa mpaka alivo leo then kuwatibua kwa kigezo cha ku excercise democracy hata ningekuwa mm Mbowe zzk ningemchinjia baharini tu.Angevuta subira hakika angekula mbivu wala hiyo haihitaji kuwa na Phd kulijua.Kaona kawa maarufu kuliko chama, kweli ngoma ikivuma sana mwishowe hupasuka!maoni yangu tu!

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Ni ujinga wa kufikiri uko hivi kama kweli ni mwana mageuzi huwezi kuwaza namna hii, haiwezekani kupata mabadiliko kamili bila kufuata hatua kwa hatua kama ulikuwa unasema uko katika harakati za kutafuta mabadiliko kisiasa na kimfumo lazima utambue jitihada ndogo za chama kikuu cha upinzani hasa Chadema, ila kama ulikuwa unatafuta mfano wa malaika Ndani ya chama wewe bado hujatambua unataka nini katika harakati hizi na uvivu zaidi wa kufikiri kama utasema iwapo hujaona malaika Ndani ya upinzani, eti ubaki ccm! ! Tujitambue

Mabadiliko ya hatua with genuine mistakes is one thing.

A gross scam is quite another.

Don't get it twisted.
 
Nilishaandika hapa kwamba CHADEMA kiufupi ni CCM-B, na watu kama kina Mnyika ingawa wanaweza kuwa smart, wanaweza kuponzwa na mwenendo wa chama kizima.

Watu wakaona huyo Kiranga tu.

Na kwa kweli haya si yote, kuna mengine mabaya zaidi yamejificha.

Wanaosemana kwa mabaya hawaanzi kwa kuanika mabaya yote kwa kawaida, yale mabaya zaidi hubakishwa vita vikikomaa.

Nahofia kwamba yale machafu kabisa bado hatujayajua.


Copy to JMAkamba maana mna undugu
 
Last edited by a moderator:
Chemba tunasema mbowe hatumtoi hata iweje na msitupangie ,,,vinyago nyie
 
Back
Top Bottom