capito
JF-Expert Member
- Nov 16, 2011
- 424
- 229
Nadhani mtoa hoja tungekupongeza sana kama ungekuja na njia mbadala ya kushugulikia chanzo cha mgogoro ndani ya CHADEMA; ambao kila mmoja anatambua kuwa ni "usaliti" wa ndg Zitto ndani ya chama.
Wewe kama mtu mwenye akili, weledi na busara ni vizuri kushauri bila upendeleo ili kukinusuru chama; ila ni wazi kabisa kwamba dawa pekee ya usaliti ni kutimua.
Huwezi kuvumilia pale unapo hujumiwa. Ushahidi wa kutosha uko wazi jinsi Zitto alivyo tumiwa na wabaya wa CHADEMA ili aue chama.
Kama naye alikuwa na tuhuma dhidi ya Mbowe, mbona kakaa kimya siku zote aje kufunguka leo baada ya kuchinjiwa baharini? Si angeongea mapema akiwa bado na heshima zake ndani ya chama ili watu wamwelewe na kuchangia hoja?
Kumbukeni Zitto analeta janja ya kuku kuwa na nguvu nyingi z kutaka kuruka na kukimbia mara tu akishakatwa kichwa.
Huo ushaidi wa Zitto kukisaliti chama uko wapi mbona hatuuoni au kuandaa mkakati wa 2013 ndio usaliti? Acha kukaririshwa mambo bila kufikiri. Leta ushahidi kuwa Zitto ni msaliti na sisi tutakuamini. Unatumia waraka ulioandaliwa kumchafua ndio uasema ushahidi? Mbona mkanda wa video ya ugaidi ya Lwakatare mnasema ni wa kutengeneza? kwa nini waraka wa kumchafua Zitto huamini kuwa ni wa kutengeneza pia?