Wenye akili CHADEMA wapo kimya

Wenye akili CHADEMA wapo kimya

Leo anayasema haya kwasababu katoka CDM, kwahiyo anamaanisha huko aendako siku nako akiondoka atahara tena kama alivyoondoka CDM?

Na kwa mfano leo CDM wakasema tumeamua kusamehe ya Zitto , je, atarudi ama hatarudi? si ndo anachokipigania? na akifika huko atasema niliamua kumwaga mboga? wenye busara kamwe huwa hawamwagi mboga ndo maana tunamlaumu Pinda alipomwaga mboga kusema "wapigwe". Learn ZZK.

Kwa hiyo wewe kosa umeliona upande mmoja tu wa ZZK kumwaga mboga? Na hao waliomwaga ugali? duuu hivi watanzania tumefikia hapa?
 
Wewe ndio mpuuzi,kama hapo mwanzo uliwaona vichwa na sasa umewadharau basi kichwa chako kimejaa funza,yaani ualinganisha fikra zako na Prof Safari,Lisu,Marando na Mnyika?Wewe kweli unatania!
 
Nilishaandika hapa kwamba CHADEMA kiufupi ni CCM-B, na watu kama kina Mnyika ingawa wanaweza kuwa smart, wanaweza kuponzwa na mwenendo wa chama kizima.

Watu wakaona huyo Kiranga tu.

Na kwa kweli haya si yote, kuna mengine mabaya zaidi yamejificha.

Wanaosemana kwa mabaya hawaanzi kwa kuanika mabaya yote kwa kawaida, yale mabaya zaidi hubakishwa vita vikikomaa.

Nahofia kwamba yale machafu kabisa bado hatujayajua.

Chadema ni Ccm A na Ccm yenyewe imeshakuwa namba mbili. Yaani maovu ya CDM kwasasa ni zaidi ya wale CCM.
 
Anayefanya mambo kwa kubabaisha utamjua tu, mjinga utamjua tu. Hayo ndio maneno sahihi ya kuwaeleza kina Msigwa, Mnyika , Lissu na wengineo kama wapo lakini kifupi wamejimaliza kisiasa wamekubali kutumika kama mbwa kukamata mtu anayepita wakati mwenye mbwa katulia ndani. Tunahoji uwezo wao wa kifikra na kiutambuzi wa kuchanganua mambo. Hawajiulizi kwa nini viongozi wenzao tena wakubwa kimamlaka, kiumri, wanaoheshimika sana wamejiweka pembeni na mgogoro huu. Imekula kwenu kama hamkutambua wananchi wanataka nini. kwishiney Mnyika kwishney Lissu
 
Lissu na Mnyika wamenihuzunisha sana. Hongera zake Halima Mdee, nitampa tena kura yangu akija tena hapa Kawe. Kwa muda mrefu mchanganyiko wa Lissu, Zitto na Mnyika umekuwa na matumaini makubwa sana kwetu wapenda mageuzi. Lkn wote wanepotoka na kupotoshana. Ni pigo kwa demokrasia yetu kwa kweli.
mkuu halima mdee sio kwamba amekaa kimya kwa kupenda, bali ameambiwa uchaguzi ujao atagombea josephine mshambushi jimbo la kawe kupitia chadema. kwa hiyoanajua hana chake.
 
mkuu halima mdee sio kwamba amekaa kimya kwa kupenda, bali ameambiwa uchaguzi ujao atagombea josephine mshambushi jimbo la kawe kupitia chadema. kwa hiyoanajua hana chake.
Whaat? I can't buy this. Kwa hiyo wakati tunalalamika mkuu wa wama kuwa mjumbe huko ccm, na sisi tunakaribisha upuuzi huohuo. This is too much ikitokea. By the way, ana wasiwasi gani? Tuliona mfuko sawa kwa wote, sasa tuna wanawake na maendeleo, na yeye si atakuja kuanziasha ya kwake ".......ni zamu yao"; kwa hiyo atulie tu haipendezi kujazana families kwenye vyama utadhani ni saccos.
 
Wewe ndio mpuuzi,kama hapo mwanzo uliwaona vichwa na sasa umewadharau basi kichwa chako kimejaa funza,yaani ualinganisha fikra zako na Prof Safari,Lisu,Marando na Mnyika?Wewe kweli unatania!

Ungeandika bila kutukana ningekuona huna funza kichwani, ila mpaka hapo umedhihirisha kuwa ni hamnazo. Kwani prof Safari, Lissu, Marando na Mnyika ni nani? si ni binadamu tu waliopitia shule kama wengine tu. Sasa waongee pumba bado niwaone sawa eti kwa kuwa wao ni pro Safari, Lissu, Marando na Mnyika. Anyway, ukikua utaacha!
 
Kama kupanga kugombea nafasi ya uenyekiti wa chama ni njama za kukiuua chama basi hicho chama hakifai hatakuwepo. Kwani ZZK angepata wapi kura za kushinda hata kuwa mwenyekiti? Na kama mtu ambaye hafai anapata kura nyingi mpaka kushinda kosa lake lipo wapi? kosa si lipo kwa waliomchagua? ZZK, Kitila na Mwigamba hawakufanya kosa kiasi cha kufukuzwa uanachama, ni ubabe tu wa akina Slaa na hofu ya kuondoka kwenye nafasi zao na kukosa hayo mamilioni wanayopata makao makuu wakati wenzao wilayani na kwingineko wanajitolea kufanya kazi za chama.

Mtabwabwaja sana lakn ukweli upo palepale,wasaliti wamefukuzwa! kamati kuu imetenda kazi yake iliyotukuka!
 
Ungeandika bila kutukana ningekuona huna funza kichwani, ila mpaka hapo umedhihirisha kuwa ni hamnazo. Kwani prof Safari, Lissu, Marando na Mnyika ni nani? si ni binadamu tu waliopitia shule kama wengine tu. Sasa waongee pumba bado niwaone sawa eti kwa kuwa wao ni pro Safari, Lissu, Marando na Mnyika. Anyway, ukikua utaacha!

Unasumbuliwa na ushabiki wa kijinga!
 
mkuu halima mdee sio kwamba amekaa kimya kwa kupenda, bali ameambiwa uchaguzi ujao atagombea josephine mshambushi jimbo la kawe kupitia chadema. kwa hiyoanajua hana chake.

Akili za misukule utazijua tu! huna jipya kachukue buk7 lumumba
 
Sasa kuna mtu amekulazimisha kuongea?
Mbona povu kubwa sana umekunywa sumu
Tukupe maziwa fresh nayo ni CDM
Mpango mzima usisikilize wahuni na
Wasaliti.
 
Unasumbuliwa na ushabiki wa kijinga!

Heri yako wewe mwenye ushabiki wa AKILI uliyeishia kuandika sentensi moja bila hata kutoa sababu ya kwa nini unasema hivyo, pole sana lakini.
 
jina lenyewe una tania ililkujua kuwa chadema inakufa njoo huku Nyasura Bunda uone maana CCM hawana mgombea katika kata hii kisa watu wote wana iamini chadema endeleeni na siasa zenu za jamiiforums huku chadema wana pasua anga ndio mtajua kuwa siasa si kwenye keyboard
 
Lissu na Mnyika wamenihuzunisha sana. Hongera zake Halima Mdee, nitampa tena kura yangu akija tena hapa Kawe. Kwa muda mrefu mchanganyiko wa Lissu, Zitto na Mnyika umekuwa na matumaini makubwa sana kwetu wapenda mageuzi. Lkn wote wanepotoka na kupotoshana. Ni pigo kwa demokrasia yetu kwa kweli.

Umemsahau Wenje mkuu! Jamaa kakaa kimya hii safi sana!
 
Lissu na Mnyika wamenihuzunisha sana. Hongera zake Halima Mdee, nitampa tena kura yangu akija tena hapa Kawe. Kwa muda mrefu mchanganyiko wa Lissu, Zitto na Mnyika umekuwa na matumaini makubwa sana kwetu wapenda mageuzi. Lkn wote wanepotoka na kupotoshana. Ni pigo kwa demokrasia yetu kwa kweli.

Huo mchanganyiko ulikuwa haumfai Zitto, wakati wenzake wanadhamira ya dhati ya kuleta mabadiliko, kumbe ZZK anawasanifu! Snitch mkubwa yule bwana, bora ajitenga wamwache Lissu na Mnyika waendeleze libeneke, yeye limemshinda kwa tamaa!

Hivi wewe hujiulizi ZZK alitoa wapi jeuri ya kutangaza kuwa hatogombea tena ubunge Kigoma, alikuwa anajua kuwa dhamira yake ya kukisambaratisha chama itakuwa imetia, bahati njama zake zimejulikana kabla hajatekeleza dhamira yake!
 
Kwa akili zako wewe unaona hicho kilichofanywa na akina Zito ni uhaini? seriously? Eeee Mungu katuumba tofauti aiseeee! Na hayo ya ufujaji wa mali za chama ya Slaa na Mbowe tuyaite nini? Hivi inamaana hata hufahamu maana ya neno KUYUMBA mpaka useme CHADEMA haijayumba? Mimi niendeshe propaganda dhidi ya Chadema nifaidi nini? Ifike wakati nyie wanachama ama wapenzi wa Chadema wenye shingo ngumu muanze kupima nguvu ya hoja kabla ya kufyatuka na kutetea uovu mkidhani kila anayeandika dhidi ya chama chenu ni CCM. Kwa taarifa yako Niichukiavyo CCM ndivyo niichukiavyo Chadema. Wote wale wale tu.
kasome katiba ya chama ukomo wa wa uanachama ile ibara ya 5.4.3 wewe kilaza,muulize Zitto mara ya mwisho kufika pale ofisini kwake ofisi ya chama Ufipa,kumbuka mfadhili wa kina mwampamba na Juliana,then uniambie kwanini alikuwa hashiriki oparation zote kubwa na wenzie hata uzinduzi tu wa oparation,kuhusu suala la matumizi mabaya ya fedha ambayo nyinyi kama propaganda yenu kuu yalishatolewa ufafanuzi na mkurugenzi wa fedha Komu muda mrefu na nyalaka mkaonyeshwa na hakuna matumizi ya chama yoyote yaliyotumika bila kufuata chanell tena kwa maagizo ya chama na si Mbowe kama unaushahidi kuna matumizi mabaya ya fedha za chama zilizotumika nje ya maagizo halali ya vikao vya chama onyesha tena kwa ushahidi wa document za manunuzi.Nionacho kwako unaijua CHADEMA ya magazetini tena ya uhuru na mzalendo na TBC CCM sumbua kichwa ndugu usipende vitu rahisirahisi.
 
Huo ushaidi wa Zitto kukisaliti chama uko wapi mbona hatuuoni au kuandaa mkakati wa 2013 ndio usaliti? Acha kukaririshwa mambo bila kufikiri. Leta ushahidi kuwa Zitto ni msaliti na sisi tutakuamini. Unatumia waraka ulioandaliwa kumchafua ndio uasema ushahidi? Mbona mkanda wa video ya ugaidi ya Lwakatare mnasema ni wa kutengeneza? kwa nini waraka wa kumchafua Zitto huamini kuwa ni wa kutengeneza pia?


Unaliza kondomu zilizotumika kwenye viwanja ulipokesha mwenge?

Kama huyajui madhambi ya Zitto siwezi kukushangaa kwakuwa hata M/kiti wa ccm Taifa hajui kwanini watz ni masikini wakati waandamizi wake wana utajiri usioelezeka.
 
Huo mchanganyiko ulikuwa haumfai Zitto, wakati wenzake wanadhamira ya dhati ya kuleta mabadiliko, kumbe ZZK anawasanifu! Snitch mkubwa yule bwana, bora ajitenga wamwache Lissu na Mnyika waendeleze libeneke, yeye limemshinda kwa tamaa!

Hivi wewe hujiulizi ZZK alitoa wapi jeuri ya kutangaza kuwa hatogombea tena ubunge Kigoma, alikuwa anajua kuwa dhamira yake ya kukisambaratisha chama itakuwa imetia, bahati njama zake zimejulikana kabla hajatekeleza dhamira yake!

Kua ukuwe, hata kama huyo zitto ni msaliti lakini utakuwa ni ujuha wa aina yake kama hautotambua uwezo wa Zitto katika kuchambua na kuzungumzia hoja mbalimbali. Ni ujuha wa kutotambua hilo, regardless what is going now, but the guy is smart-equal weight with Myika and Tundu Lissu. Haya ni kwa mujibu wa uhalisia ambao upo kwenye ushahidi mbalimbali. Hizo za usaliti ni hearsay ambazo imeshindikana kuziaminisha kwa jamii yote ya watanzania (at least). Unadhani kinachoendelea sasa nini? Kwani CDM ni mara ya kwanza kufukuza wanachama wake? Mbona hatukuona mtikisiko kama huu? Ni kwasababu Zitto amejenga uimara madhubuti miongoni mwa watanzania, ni hali kama hiyo siku utakayoskia mtu kama Tundu lisuu anafukuzwa au anaondoka chamani. Tuache hisia badala yake nyeupe tuite nyeupe.
 
Wewe Nyakanazi kwa hoja ni mwepesi sana kama ukuni, nikwambie sasa, hata ukioa alafu ukaacha kesho kamwe hauwezi ukalinganishwa na yule ambaye hajawahi kuoa na ndo maana huwa tunauliza umewahi kuoa hata siku 1? ndoa hata ya siku 1 kukaa na mwanamke si sawa na kula pipi

Sasa kama haujaoa ama haujawahi hauwezi kamwe ukawa kundi 1 na wengine, kwasababu bila hivyo kuna vitu wanaume wenzio watakudharau utake usitake,huyu dogo anakosa hilo daraja ndo maana anabwatuka hovyo ...ya ndani ni ya ndani kijana.
 
Back
Top Bottom