Wenje asambaratisha CCM Sengerema

Wenje asambaratisha CCM Sengerema

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Mkurugenzi wa mambo ya nje wa CDM ambaye pia ni mbunge wa Nyamagana Ezekiah Wenje jana alifanya mkutano mkubwa wa hadhara mjini Sengerema ambapo wanachama 50 wa CCM walijitoa katika chama hicho na kujiunga na CDM.Mkutano huo unadaiwa kuwa mkubwa kuwahi kufanywa na chama cha siasa mjini hapo.

SOURCE:TANZANIA DAIMA
 
Je alifanikiwa kuwarejesha wale waliodaiwa kunyakuliwa na Ngeleja?
 
hapo kazi ipo

nadhani ndiyo maana waliodaiwa kuwa viongozi walizomewa na wananchi walipo kuwa jukwaani

Big up Wenje sasa bado Nyanza na KUKIIMARISHA CHAMA HUKO PIA PANGA UONGOZI IMARA
 
Siasa za Tanzania bana......Yaani ni kama Ze komedi flani hivi...

Haziishi kushangaza...
 
Wenje ni mbunge, waziri kivuli na mkurugenzi nje! Malipo mara 3!
 
Hizi mbona ni mvua za rasharasha? mafuriko yanakuja. Msishangae kusikia kijiji au tawi zima limeamia chadema maana watu wamechoka kwa ufisadi na usanii wa magamba.
 
Siasa za Tanzania bana......Yaani ni kama Ze komedi flani
hivi...

Haziishi kushangaza...

Ngeleja aibomoa CHADEMA

na Sitta Tumma na Stella Ibengwe, Sengerema

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja, ameibomoa ngome ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) baada ya viongozi wa chama hicho Wilaya ya Sengerema, mkoani Mwanza kurudisha kadi na kuhamia Chama cha Mapinduzi
Viongozi hao wa CHADEMA waliohamia CCM, ni Mwenyekiti wa Wilaya ya Sengerema, Ayub Malima, Katibu wa wilaya, Kesi Misalaba, Katibu wa Baraza la Wanawake, Sarah Mathayo na Mwenyekiti wa Vijana, Stanslaus Pastory. Viongozi wengine ni Katibu wa Vijana, Frank Dotto, Lusia Mussa na Sayi Busumabu (wajumbe) pamoja na mwanachama mmoja wa Chama cha Wananchi (CUF), Peress Essau, ambaye mwaka 2005 aligombea ubunge katika Jimbo hilo la Sengerema.

Katika mkutano ulioandaliwa na Waziri huyo ambaye ni mbunge wa Sengerema, viongozi hao wa upinzani walieleza kuchoshwa na sera za vyama vyao kwa madai kwamba havina mwelekeo mzuri. "Nimeamua kuhamia CCM baada ya kugundua kwamba vyama vya upinzani havina shukurani. Kuna mambo mazuri yamefanywa na Serikali ya CCM kama barabara za lami lakini wao bado wanabeza mafanikio hayo. "Kwa hiyo nimeona ni bora nihamie CCM kwa chama ninachokiona kina mwelekeo na sera mzuri, nawaomba wanachama wengine wa CHADEMA muondoke huko mje CCM chama kikubwa," alisema Malima, aliyekuwa mwenyekiti wa CHADEMA katika wilaya hiyo ya Sengerema.

Kabla ya Malima kuhamia CCM kutoka CHADEMA, aliwahi kusimamishwa Machi, mwaka jana kwa barua yenye kumbukumbu Na. CDM/J/SENG/01/2011 iliyotumwa kwa Katibu wa CHADEMA wa Mkoa wa Mwanza, kwa madai ya kusababisha mgogoro ndani ya chama hicho, lakini baadaye Baraza la Uongozi wa mkoa wa CHADEMA lilitengua uamuzi huo.
Awali Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Sengerema, Jaji Tasinga Gabanyaga, aliwapongeza viongozi hao wa upinzani kwa kuhamia CCM, kwa maelezo kuwa, hali hiyo inaonesha dhahiri kwamba sera za chama tawala ni nzuri.
Kwa upande wake, Ngeleja alifurahia ujio huo wa wanachama hao wa upinzani, kwa maelezo kuwa hali hiyo inaonesha wazi kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Nne inaleta maendeleo.


CHADEMA yajibu mapigo ya CCM

na Stella Ibengwe, Sengerema

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilayani Sengerema, mkoani Mwanza, kimejibu mapigo kwa Chama cha Mapinduzi (CCM), dhidi ya wanachama wake 15 waliochukuliwa, kwa kujipatia wanachama wapya 50.CHADEMA imejibu mapigo ya Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, ambaye ni mbunge wa jimbo hilo, ambapo siku za karibuni alibomoa ngome ya chama hicho cha upinzani.Akizungumza na maelfu ya wananchi wa mji wa Sengerema kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Mnadani mjini hapa, mbunge wa jimbo la Nyamagana, mkoani Mwanza, Ezekiel Wenje (CHADEMA), alisema kuwa huo ni mwanzo tu wa kuvuna wanachama hao na kwamba watahakikisha mwaka 2015 jimbo hilo, linachukuliwa na upinzani."Ndugu zangu kwanza tunaipongeza CCM kwa kutuondolea uchafu uliokuwa umekithiri ndani ya chama chetu; tumefurahi sana kwa hatua waliyoichukua ya kuamua kuondoka…..CHADEMA hatuna muda wa kukaa na watu wanaotaka kukibomoa chama ni bora wameenda huko kulikojaa ufisadi wa kila aina," alisema Wenje.Wenje alisema milango iko wazi kwa wanachama wengine wa CCM wanaotaka kujiunga na CHADEMA na kuwapongeza wale wote waliojiunga na upinzani.Kwa upande wake katibu wa CHADEMA mkoa wa Mwanza, Wilson Mushumbusi, alisema kuwa chama hicho hakina wenyeviti wa wilaya bali kina waratibu wa wilaya na kuonyesha kushangazwa na baadhi ya watu waliojiunga CCM kujitambulisha kuwa wao ni viongozi wa chama hicho wakati walishafukuzwa.

Ngeleja akirudi tena sijui itakuwaje hata, inakuwa kama igizo flani hivi....
 
Back
Top Bottom