Elections 2010 Wengi hawajui Nguvu ya Maaskofu

Status
Not open for further replies.
HEBU ISIKILIZENI HII YA ASKOFU WA HUKO IRINGA, ANASEMA WAO NI WANASIASA DAIMA.. Naungana nae, Huwezi tenganisha Siasa na Maisha ya Wananchi.. Anasema, kama ma-askofu watavua majoho kina MAKAMBA WATAVUA NINI??

Francis Godwin ni mzee wa matukio daima: ASKOFU DKT MDEGELLA AMPA ONYO KALI KATIBU WA CCM ARUSHA ....

Mkuu kwako wewe ni sawa askofu kupanda madbabahuni na kuhubiri mfano jk hafai ameiba kura msimchague mchagueni dr slaa.
Na misikitini waseme mchague jk slaa hafai.
unadhani nini kitakachofuata?
 
Mkuu Anold bahati nzuri sana watz ni wepesi sana kusahau askofu fulani alipata kusema as individual jk ni chaguo la Mungu, matusi na kejeli alizopata kutoka kwa wana jf ni tofauti kabisa na hao hao wanaounga mkono kauli ya maaskofu kutomtambua meya na kutompa ushirikiano ndio waliomtaka askofu huyo avue joho ajiunge ccm

Nirejee ktk mada yako, kwanza nikupe pongezi kwajinsi ulivyojitahidi kuiwasilisha hoja yako kwa umahiri mkubwa wenye kushawishi tuamini ulichoandika ni sahihi.
Ulichojaribu kukieleza hapo ni jinsi gani kanisa lilivyo wekeza ktk huduma mbali mbali za kijamii, na ukaenda mbali zaidi na kuita hii ni "siasa" na ukaona kuwa hii ndio "nguvu" ambayo watu hawaitambui nguvu hii ya maaskofu kama ulivyoainisha ktk heading ya topic yako.

Umeniacha hoi kabisa uliposema kama wanataka maaskofu wasiingilie siasa basi wavunje huduma zao zote maana kwako wewe hii ndio siasa na unashangaa kwanini iwe ajabu wao kuingilia jambo "dogo" kama la meya wa arusha.

In short hiyo uliyoita "nguvu ya maaskofu" kwa mujibu wako ndio inayowapa uhalali wa kuingilia maswala ya kisiasa tena kwa kutoa matamko mazito ya maamuzi ya mamlaka nyingine ya kisheria.
Ni matamko kama kukemea ufisadi na kutaka maadili yazingatiwe ndio matamko yanayotarajiwa toka kwa viongozi wa dini.
Kwa hili la kupingana na maamuzi ambayo vyombo husika vimelipitisha kwa taratibu husika na kisha chama fulani kikagoma kwa hisia zao za kuonewa au iwe wameonewa kweli kisha maaskofu wanakurupuka na kusema hatumtambui hii si sahihi kabisa, ya kaisari aachiwe kaisari.
Je ikithibitika kisheria ilikuwa ni halali nini itakuwa credibility ya maaskofu?
Kanisa kuwa na vyuo au hosipitali(ikumbukwe ni misamaha ya kodi) sio kibali cha kuingilia maswala ya siasa.
Ninacho kuhakikishia hapa ni kuwa siasa zitaanza kuhubiriwa madhabahuni na misikitini kwa msingi huo wa kipuuzi unaotushawishi tuamini kuwa huwezi kuwaepusha maaskofu na siasa.
Ni mpumbavu pekee asiyeweza kuona hatari inayotunyemelea kwa kuacha viongozi wa dini wawe wanatoa matamko hovyo tu, hawa ni binadamu na wanautashi wao binafsi kama binadamu yeyote.

Pia ujue dini ni imani kali yenye kugusa hisia anachotamka askofu sikuzote ni sahihi mbele ya muumini no matter kiweje, mimi ni mkristo safi lakini kwahili ntasimamia hapana

Watu wengi wamekupa thanx na kuunga mkono hoja yako sababu tu wamesikia kile wanapenda kusikia bila kujali kina mantiki gani. watu wanashindwa kuona mbali sababu tu for this time wao ndio wanabenefit na tamko hilo la maaskofu

Mwisho nawaheshimu sana maaskofu lakini kwa hili wanakwenda mbali sana maana kwa mwendo huu watakuja kutoa tamko tubaki midomo wazi tusiamini masikio yetu.

Shukrani kwa mchango wako, yani tukishindwa kuona tatizo hilo basi tunaelekea kuchinjana.. If great thinkers cannot see this obvious problem, imagine hao wananchi wa kawaida.. Ignorance will kill us.....Maaskofu wamevuka mpaka kama vile waliposema Kikwete ni chaguo la mungu..
 
Nimeshangazwa na kauli za baadhi ya viongozi wa CCM pamoja na viongozi wa Dini fulani mkoani Arusha kupinga tamko la Maaskofu walilolitoa baada ya kotokea vurugu mkoani Arusha. Pamoja na shutuma nyingi, maaskofu hao wametakiwa kujitenga na mambo ya kisiasa badala yake wajihusishe tu na Mambo ya kiroho na si vinginevyo!

Ni rahisi sana kutoa tamko la namna hiyo kama huna muda wa kutafakari na kujihoji wewe mwenyewe kujua sababu za maana zilizosababisha Maaskofu kutoka kwenye makanisa yao na kuingilia moja kwa moja mambo ya kisiasa hususan sakata la Meya wa Arusha.

Maaskofu hawa walikuwa na sababu za msingi kabisa kumpinga Meya wa mji wa Arusha kutokana na sababu kadha wa kadha. Zaidi ya Asilimila 70 za huduma za kijamii kama Hospitali, shule achilia mbali miradi ya maji n.k Mkoani Arusha tu zinamilikiwa na kanisa. Kanisa limekuwa halina ubaguzi wa Kidini katika utoaji wa huduma zake hivyo kuwa msaada mkubwa kwa wananchi na serikali. Kwa miaka mingi tumeshuhudia kanisa likifanya juhudi kubwa kuhakikisha kuwa wananchi wa Tanzania wanaondokana na tabu zisizo za lazima kwa kujihusisha moja kwa moja na shida za jamii. Kanisa la Tanzania limekuwa likithubutu hata kushawishi nchi mbalimbali kama Ujerumani, Uingereza n.k kuziomba zitusamehe madeni, yote hayo ni katika kuhakikisha kuwa mwananchi wa Tanzania anapata nafuu bila kujali chama, dini au rangi. Hivi harakati zote hizi nilizotaja sio siasa hizi? Iweje suala dogo la kumpinga meya liwaondoe wanaharakati hawa katika siasa?

Nimeamua kuyaweka maelezo hayo machache ili nikufikirishe utambue umuhimu wa kanisa katika Nchi hii. Kimsingi MEYA wa jiji la Arusha hawezi kujitenga na kanisa kwa namna yote ile kwani kwa kiasi kikubwa kanisa linategemea kiongozi wa kisiasa ambaye kwa pamoja watashirikiana bega kwa bega ili kuendeleza zile juhudi kubwa zilizofikiwa na ambazo ni changamoto kwa maendeleo ya wanachi wa Mkoani humo. Huwezi kumtoa Askofu katika siasa, maana kwa upana wake siasa inagusa maisha ya kila siku kwa kila mtu, Askofu anahitaji Amani, maendeleo pamoja na huduma muhimu.aidha ieleweke wazi kuwa kazi ya kanisa si kutoa mapepo na kuombea wagonjwa tu, bali pamoja na hayo ni kuhakikisha kuwa maisha ya kawaida kwa maana ya mahitaji ya kimwili yanaguswa kwa namna mbalimbali.

Unapomwambia Askofu ajitenge na na siasa ni kwamba Wavunje Hospitali zao za Rufaa? Shule zao zinazofanya vizuri na kuzalisha watu wenye akili? Wavunje vyuo vyao ambavyo ni vingi kushinda vya serikali? Wasihoji vile visima vyao vya maji na miradi ya umwagiliaji? Hapana!!!. Nafikiri kuna maeneo ambayo Viongozi hawa inabidi wahoji na kukosoa wanasiasa ili vile ambavyo walibuni na kuhakikisha kuwa vinawasaidia wananchi wakiwamo waumini wao havisimamiwi na viongozi wabovu au viongozi ambao kwa nia moja au nyingine wanania mbadala na isiokubalika kwa wananchi wa Tanzania. Viongozi wa Kanisa kamwe hawatakuwa mishumaa ya kuwamulikia watu waovu wakati wao wanateketea. Linapokuja swala la Maaskofu kujiingiza katika siasa Nguvu yao ipo katika Huduma na mambo ya msingi ambayo kama wataamua kumwachia Mungu watu waovu wanaweza kuifikisha Tanzania yetu mahali ambako sio salama. Kiongozi wa kidini ambaye haoni sababu za kujiingiza na kuhoji mambo ya siasa ujue hana cha kupoteza!!!!!!!!!

Nchi tajiri ndivyo wafanyavyo tuko pamoja mkuu. nathibitisha maoni yako na haya hapa ya serikali ya USA kupitia ubalozi wake nchini Tanzania ilipotoa misaada kwenye makanisa kwa ajili ya wananchi.

Mambo yanavyokwenda mrama huwa maaskofu hawataki kuona aibu hiyo ikiingia kwao.

Thanx.

blank780x5.jpg


Front Page 1
647%20Ambassador.jpg

On Monday, December 13, at the U.S. Embassy in Dar es Salaam, the U.S. Ambassador to Tanzania Alfonso E. Lenhardt presented grants totaling Tsh.190 million to fifteen community-based organizations from Arusha, Dar es Salaam, Tanga, Iringa, Kagera, Mafia, Manyara, Morogoro, Mwanza, Ruvuma and Zanzibar. The grants provided by the Ambassador's Self-Help Fund and Ambassador's Fund for HIV/AIDS Relief will be used to support communities in their commerce, education and water and sanitation projects as well as in programs to support care-givers affected by HIV and those supporting orphans and vulnerable children. Ambassador Lenhardt (center) with coordinators and managers of community-based projects that received the grants.

 
Nimeshangazwa na kauli za baadhi ya viongozi wa CCM pamoja na viongozi wa Dini fulani mkoani Arusha kupinga tamko la Maaskofu walilolitoa baada ya kotokea vurugu mkoani Arusha. Pamoja na shutuma nyingi, maaskofu hao wametakiwa kujitenga na mambo ya kisiasa badala yake wajihusishe tu na Mambo ya kiroho na si vinginevyo!

Ni rahisi sana kutoa tamko la namna hiyo kama huna muda wa kutafakari na kujihoji wewe mwenyewe kujua sababu za maana zilizosababisha Maaskofu kutoka kwenye makanisa yao na kuingilia moja kwa moja mambo ya kisiasa hususan sakata la Meya wa Arusha.

Maaskofu hawa walikuwa na sababu za msingi kabisa kumpinga Meya wa mji wa Arusha kutokana na sababu kadha wa kadha. Zaidi ya Asilimila 70 za huduma za kijamii kama Hospitali, shule achilia mbali miradi ya maji n.k Mkoani Arusha tu zinamilikiwa na kanisa. Kanisa limekuwa halina ubaguzi wa Kidini katika utoaji wa huduma zake hivyo kuwa msaada mkubwa kwa wananchi na serikali. Kwa miaka mingi tumeshuhudia kanisa likifanya juhudi kubwa kuhakikisha kuwa wananchi wa Tanzania wanaondokana na tabu zisizo za lazima kwa kujihusisha moja kwa moja na shida za jamii. Kanisa la Tanzania limekuwa likithubutu hata kushawishi nchi mbalimbali kama Ujerumani, Uingereza n.k kuziomba zitusamehe madeni, yote hayo ni katika kuhakikisha kuwa mwananchi wa Tanzania anapata nafuu bila kujali chama, dini au rangi. Hivi harakati zote hizi nilizotaja sio siasa hizi? Iweje suala dogo la kumpinga meya liwaondoe wanaharakati hawa katika siasa?

Nimeamua kuyaweka maelezo hayo machache ili nikufikirishe utambue umuhimu wa kanisa katika Nchi hii. Kimsingi MEYA wa jiji la Arusha hawezi kujitenga na kanisa kwa namna yote ile kwani kwa kiasi kikubwa kanisa linategemea kiongozi wa kisiasa ambaye kwa pamoja watashirikiana bega kwa bega ili kuendeleza zile juhudi kubwa zilizofikiwa na ambazo ni changamoto kwa maendeleo ya wanachi wa Mkoani humo. Huwezi kumtoa Askofu katika siasa, maana kwa upana wake siasa inagusa maisha ya kila siku kwa kila mtu, Askofu anahitaji Amani, maendeleo pamoja na huduma muhimu.aidha ieleweke wazi kuwa kazi ya kanisa si kutoa mapepo na kuombea wagonjwa tu, bali pamoja na hayo ni kuhakikisha kuwa maisha ya kawaida kwa maana ya mahitaji ya kimwili yanaguswa kwa namna mbalimbali.

Unapomwambia Askofu ajitenge na na siasa ni kwamba Wavunje Hospitali zao za Rufaa? Shule zao zinazofanya vizuri na kuzalisha watu wenye akili? Wavunje vyuo vyao ambavyo ni vingi kushinda vya serikali? Wasihoji vile visima vyao vya maji na miradi ya umwagiliaji? Hapana!!!. Nafikiri kuna maeneo ambayo Viongozi hawa inabidi wahoji na kukosoa wanasiasa ili vile ambavyo walibuni na kuhakikisha kuwa vinawasaidia wananchi wakiwamo waumini wao havisimamiwi na viongozi wabovu au viongozi ambao kwa nia moja au nyingine wanania mbadala na isiokubalika kwa wananchi wa Tanzania. Viongozi wa Kanisa kamwe hawatakuwa mishumaa ya kuwamulikia watu waovu wakati wao wanateketea. Linapokuja swala la Maaskofu kujiingiza katika siasa Nguvu yao ipo katika Huduma na mambo ya msingi ambayo kama wataamua kumwachia Mungu watu waovu wanaweza kuifikisha Tanzania yetu mahali ambako sio salama. Kiongozi wa kidini ambaye haoni sababu za kujiingiza na kuhoji mambo ya siasa ujue hana cha kupoteza!!!!!!!!!

Anold,
Kwanza asante sana kwa kuwajuza watu kuhusu umuhimu wa kanisa.
Kanisa kwa kweli limefanikiwa sana kuendesha miradi yake ya kijamii kwa ufanisi mkubwa mno. Hospitali, mashule na vyuo vyote vyenye mafanikio, sehemu kubwa ni mali ya kanisa.
Hawa viongozi katika siasa hasa wa CCM lazima wajue kuwa wanaongoza watu, na watu hao hao ndo wanawafanya wao wawe viongozi hata MAASKOFU ni sehemu ya watu. Maaskofu hawapatikani kwa zengwe kuu kama ilivyo kwa wanasiasa wetu hapa Tanzania.

Nguvu ya watu ya kujikomboa kifikra ndo inaleta haya yote. CCM wamezoea kupeleka mambo vile wao wanaona itakuwa na manufaa kwa mfumo wao wa kiutawala pasipo kujua hii nchi si ya kwao peke yao, Tanzania ni yetu sote.
:peace:
 
Mary Chitanda is a nut! She is a MONSTER! She must be stopped immediately once and for all!

Huyu mwananke hana adabu kwa kuwakashifu maaskofu. Tayari amekataa kuomba msamaha kwa madai kuwa alichosema ni sahihi!

Huyu mwanamke yaonekana si Mkristo yawezekana hili jina ni la kutafutia mkate tu. I believe ana dini yake mfukoni anayoijua yeye.
Ninachotaka kusema ni kuwa HUYU MAMA TUMPENI JUST SOME FEW DAYS HATUTAMSIKIA TENA!!!!

Huwezi kusababisha DAMU IMWAGIKE NA UTUKANE WATUMISHI WA MUNGU HALAFU UBAKI SALAMA. DAMU ILIYOMWAGIKA 'A TOWN' HAKIKA ITAMTAFUNA HUYU KIGAGULA MPAKA DUNIA IMSAHAU KAMA ALIWAHI KUWEPO MARIA KITANDA.

GOD OF ABRAHAM,GOD OF ISAACK,GOD OF JACOB SHALL DEAL PERPENDICULARLY WITH MARY CHITANDA. SHE IS AN ABOMINATION TO OUR SOCIETY. SHE MUST BE STOPPED IMMEDIATELY BEFORE SHE CREATES ANOTHER DISASTER.
 
Nakushukuru Anold kwa ufafanuzi mzuri kabisa. Hivi lini giza likakaa pamoja na mwanga. Utasikia au tulishaona mtu alie na mapepo yanapowaona maaskofu hata kabla hajaongea utasikia, yanapanda na kumsumbua sana yule aliyenayo wakati mwingine yanamuumiza. Kwahiyo huitaji kuambiwa nani alie na mapepo wakati yanashuhudia maaskofu, watahangaika mno mpaka yatolewe na maaskofu haohao. Amini usiamini, Makamba na Chatanda lazima wawaombe radhi maaskofu other wise hawatakua na amani mioyoni mwao, na baadae laana kwao itajidhihirisha kwa uma.
 
Bila kusoma comments naenda momja kwa moja kwenye tahadhari. Kama tunanaungama na kutubu mbele yao imetokea nini kuwaita mashetani watu unaowasududia> kweli Yuda ni mfano. Yesu alikutufia. Ila nahisi hatrudi tena. Yuda isakaliote MAKAMBA (Kafiri) ni mshindi.
 
CCM wanataka waheshimiwe viongozi wa kiislamu tu. Hao wakisema kila mtu kimya maana wao lao moja tu. Yao yote upangiwa msikitini.:A S-fire1:
 
pamoja mkuu,kati ya wakristo na waislamu nani wanahubiri udini kisiasa???jk,makamo,igp,jaji mkuu,ccm katibu mkuu,kinana nk,wanatupeleka kwenye udini nami naomba sasa 2015 maaskofu wapige kampeni wazi wazi am damn tired with religious politics mana ccm ndo wanaofanya dat stuffff....
 
Umesema vizuri sana. Kwani huyo Chitanda ni dhehebu gani? Na kwanini yeye na familia yake wasitengwe na kanisa kwa kukosa adabu hadi hapo atakapo tubu dhambi zake?

Kwani kanisa likimtenga mtu anakuwa ndiyo kanyanganywa dini? Kama si hivyo anapungukiwa nini katika ibada kwa kutengwa? Kosa kwa binaadamu mwenzio linaweza kumnyima mtu haki ya ibada kwa Mungu wake? Duu unaweza kuachishwa dini kama anavyoachishwa mtu kazi.
 
Mauwaji ya kimbali ya Rwanda yalikuwa ni ya kikabila siyo ya kidini! Acha uzoba wako, maaskofu wa Rwanda walikuwa wanampinga nani serikalini, je waliokuwa madarakani walikuwa mashehe au maimamu? Angalia percentage ya wenye imani kama yako ya Rwanda na wumini wa madhehebu mengine na dini za asili atapata jibu!

Nimekustukia, kubishana na wewe unaestruggle kwenda akhera ni kupoteza muda maana unafikiri kinyume nyume kama maandishi ya kiarabu!

Huyu Anko Sam anasema kiarabu kinaenda kinyume nyume, hii ni kwasababu kazaliwa kaona watu wanasoma kushoto kwenda kulia basi kingine chochote lazima kiwa kinyume. Atoke shimoni afuatilie vitu ataona hata maisha yake yanajiandika na yanasomwa kulia kwenda kushoto. DNA ambayo ndiyo chip ya maisha ya binaadamu, inajiandika kutoka kulia kwenda kushoto, na kusomwa inasomwa kwa muelekeo huo huo, kama QURAN inavyosomwa. Si hayo tu yako mengi, dunia unayoishi inazunguka katika mhimili wake kutoka kulia kwenda kushoto na ndiyo ukapata majira ya usiku na mchana jua kuchomoza mashariki na kuzama magharibi. Yapo mengi, hakika hapo kuna mambo ya kufuatilia....
 
Mdarasat +hiyo dini=0!wanaijua roma iweje tanzania msiwajue maaskofu??hakuna nchi duniani isiyoendeshwa na ukristo mkubali mkatae ukweli ndiyo huo jiulize nchi zote zenye nguvu kwanini zinaongozwa kikiristu??,hata zakiarabu nowdays zipochiniya imaya yakikiristu!
 
asante kwa post nzuri,ukweli ni kuwa viongozi wetu wamelewa madaraka na kwa vile hawawajibishwi kwa yale wanayoongea,wana kiburi cha kusema wayatakayo.hakuna mtu ana nguvu kama kiongozi wa dini kwa kuwa asilimia kubwa ya watanzania ni waumini wazuri wa dini yao...kwenye imani ndiko tunakotafuta majibu ya masuala magumu kwenye maisha yetu including haya maisha magumu nchini kwetu,hatutegemei majibu kutoka kwa wanasiasa bali kwa mungu.na mtumishi wa mungu ana heshima ya kipekee na nguvu kubwa na imani ya wale anaowangoza,kwa hiyo ni kosa kubwa kudharau maaskofu na ni kukosa pia busara.maaskofu wana uwezo wa kuleta vita na serikali na kuepusha vita na serikali?kwa kuwa ndio wanaolea watu kiroho,hakuna kosa kwenda kuzungumza roho zinazolia kila siku kwa yale serikali inayofanya.ccm arusha walikosea sana,na itachukua muda kumaliza hiyo chuki walioijenga si tu na viongozi wa dini bali na waumini wao,kwa kuwa ukimdharau askofu haiwezekani unaniheshimu muumini.

waache akina makamba walewe madaraka kama wamesahau kuwa mtu akilewa huwa nafanya mambo ya aibu bila kujali ni nani anamwangalia kwakuwa watajikuta wakivua nguo zao hadharani wakidhani ni umaarufu eti hawaogopi kitu kama mlevi anavyojisikia fahali kuurinate hadharani
 

Nimeshangazwa na kauli za baadhi ya viongozi wa CCM pamoja na viongozi wa Dini fulani mkoani Arusha kupinga tamko la Maaskofu walilolitoa baada ya kotokea vurugu mkoani Arusha. Pamoja na shutuma nyingi, maaskofu hao wametakiwa kujitenga na mambo ya kisiasa badala yake wajihusishe tu na Mambo ya kiroho na si vinginevyo!

Ni rahisi sana kutoa tamko la namna hiyo kama huna muda wa kutafakari na kujihoji wewe mwenyewe kujua sababu za maana zilizosababisha Maaskofu kutoka kwenye makanisa yao na kuingilia moja kwa moja mambo ya kisiasa hususan sakata la Meya wa Arusha.

Maaskofu hawa walikuwa na sababu za msingi kabisa kumpinga Meya wa mji wa Arusha kutokana na sababu kadha wa kadha. Zaidi ya Asilimila 70 za huduma za kijamii kama Hospitali, shule achilia mbali miradi ya maji n.k Mkoani Arusha tu zinamilikiwa na kanisa. Kanisa limekuwa halina ubaguzi wa Kidini katika utoaji wa huduma zake hivyo kuwa msaada mkubwa kwa wananchi na serikali. Kwa miaka mingi tumeshuhudia kanisa likifanya juhudi kubwa kuhakikisha kuwa wananchi wa Tanzania wanaondokana na tabu zisizo za lazima kwa kujihusisha moja kwa moja na shida za jamii. Kanisa la Tanzania limekuwa likithubutu hata kushawishi nchi mbalimbali kama Ujerumani, Uingereza n.k kuziomba zitusamehe madeni, yote hayo ni katika kuhakikisha kuwa mwananchi wa Tanzania anapata nafuu bila kujali chama, dini au rangi. Hivi harakati zote hizi nilizotaja sio siasa hizi? Iweje suala dogo la kumpinga meya liwaondoe wanaharakati hawa katika siasa?

Nimeamua kuyaweka maelezo hayo machache ili nikufikirishe utambue umuhimu wa kanisa katika Nchi hii. Kimsingi MEYA wa jiji la Arusha hawezi kujitenga na kanisa kwa namna yote ile kwani kwa kiasi kikubwa kanisa linategemea kiongozi wa kisiasa ambaye kwa pamoja watashirikiana bega kwa bega ili kuendeleza zile juhudi kubwa zilizofikiwa na ambazo ni changamoto kwa maendeleo ya wanachi wa Mkoani humo. Huwezi kumtoa Askofu katika siasa, maana kwa upana wake siasa inagusa maisha ya kila siku kwa kila mtu, Askofu anahitaji Amani, maendeleo pamoja na huduma muhimu.aidha ieleweke wazi kuwa kazi ya kanisa si kutoa mapepo na kuombea wagonjwa tu, bali pamoja na hayo ni kuhakikisha kuwa maisha ya kawaida kwa maana ya mahitaji ya kimwili yanaguswa kwa namna mbalimbali.

Unapomwambia Askofu ajitenge na na siasa ni kwamba Wavunje Hospitali zao za Rufaa? Shule zao zinazofanya vizuri na kuzalisha watu wenye akili? Wavunje vyuo vyao ambavyo ni vingi kushinda vya serikali? Wasihoji vile visima vyao vya maji na miradi ya umwagiliaji? Hapana!!!. Nafikiri kuna maeneo ambayo Viongozi hawa inabidi wahoji na kukosoa wanasiasa ili vile ambavyo walibuni na kuhakikisha kuwa vinawasaidia wananchi wakiwamo waumini wao havisimamiwi na viongozi wabovu au viongozi ambao kwa nia moja au nyingine wanania mbadala na isiokubalika kwa wananchi wa Tanzania. Viongozi wa Kanisa kamwe hawatakuwa mishumaa ya kuwamulikia watu waovu wakati wao wanateketea. Linapokuja swala la Maaskofu kujiingiza katika siasa Nguvu yao ipo katika Huduma na mambo ya msingi ambayo kama wataamua kumwachia Mungu watu waovu wanaweza kuifikisha Tanzania yetu mahali ambako sio salama. Kiongozi wa kidini ambaye haoni sababu za kujiingiza na kuhoji mambo ya siasa ujue hana cha kupoteza!!!!!!!!!
Huduma hizo zinazotolewa zinatolewa bure, Hospital, shule na vyote vinavyofanana. Hata kama wanatoa huduma wako kibiashara zaidi kuliko unavyozani, hata hawawezi kugoma kufanya au kusitisha kufanya biashara.
Hebu fikiria, kuna baadhi ya shule, mojawapo Loyola high school, Registration fee ni laki mbili, hilo ni kanisa linasaidia watu, na linaisaidia serikali, niambie ni nani wa kwenda hapo, na hapo wamesamehewa mpaka na hzo kodi, waache kuchonga chonga bwana, ila nao si wasafi kama wanavyojizani au kuzaniwa.
Nawasilisha.
 
Mkuu kwako wewe ni sawa askofu kupanda madbabahuni na kuhubiri mfano jk hafai ameiba kura msimchague mchagueni dr slaa.
Na misikitini waseme mchague jk slaa hafai.
unadhani nini kitakachofuata?

Hapo unawasemea. Ni wapi askofu alisema hivyo. Akisema tumieni kura zenu kuchagua viongozi bora hana maana JK sio bora, na kama JK au mbunge yeyote sio bora basi hastahili kuchaguliwa. Kiongozi wa kiroho ni wa jamii na ana wajibu wa kuelimisha jamii, sio kuchochea chuki.
 
Huduma hizo zinazotolewa zinatolewa bure, Hospital, shule na vyote vinavyofanana. Hata kama wanatoa huduma wako kibiashara zaidi kuliko unavyozani, hata hawawezi kugoma kufanya au kusitisha kufanya biashara.
Hebu fikiria, kuna baadhi ya shule, mojawapo Loyola high school, Registration fee ni laki mbili, hilo ni kanisa linasaidia watu, na linaisaidia serikali, niambie ni nani wa kwenda hapo, na hapo wamesamehewa mpaka na hzo kodi, waache kuchonga chonga bwana, ila nao si wasafi kama wanavyojizani au kuzaniwa.
Nawasilisha.

Wanakwenda wengi tu na nafasi hazipatikani. Wale wanaoenda kwenye shule kama hizo wanapunguza msongamanoi kwenye shule za serikali walala hoi wanapata nafasi. Kwa njia hiyo amekusaidia wewe na serikali.
 
hawa watu wnasindwa kutambua hivi zanzibar kuna kiongozi anaeweza kuongoza bila kuwa sambamba na masheee wa huko?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom