Wema Sepetu: Najuta kutoa mimba ya Marehemu Kanumba

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,739
32,874
image.jpeg


Katika Mahojiano yake na Waandishi wa Kampuni ya New Habari(2006) Ltd,Wema Sepetu anaanza kwa kusema

"Nilipokuwa na uhusiano na Marehemu Kanumba,nikiwa naishi na wazazi wangu,niliwaza kama wakijuwa nina Mimba wangejisikiaje?Na pia sikuwa tayari kwa kipindi hicho kuwa na mimba,na utoto pia ulichangia,nikatoa"

"Wanaume wote waliofuata hapo akiwemo Chalz Baba,Jumbe na Diamond sikuweza kupata huo ujauzito wala aina yoyote ya kichefuchefu,Lakini nilipoachana na Diamond alipokuwa na mwanamke mwingine nikasikia amepata ujauzito,kiukweli niliumia sana,nikafikiria kwamba mimi ndiye nina tatizo au ile mimba niliyotoa wakati wa Kanumba ilikuwa ndio pekee niliyojaliwa na Mungu,baada ya hapo nikaanza kumsumbua Daktari wangu,daktari alinipa dawa mbalimbali na kuweka sawa viamsho mwilini,lakini dawa hizo zikaishia kuninenepesha tu"

Wema Sepetu anaendelea kusema
"Wakati nikiwa na Idriss,nikashangaa baadhi ya watu wakaniambia nina mimba,lakini sikuamini nikaenda kupima nikiwa na lengo la kusafisha kizazi lakini daktari akaniambia vipimo vinaonyesha kweli nina ujauzito.Nilifikia uamuzi wa kusafisha kizazi sababu nilichoka kuitwa mgumba"

"Baada ya kukugundulika ujauzito huo nikapiga picha na kuzituma kwenye mitandao nikionyesha tumbo langu,ili kuwaonyesha watu kuwa si mgumba ambapo wengine walishika tumbo langu wakifurahia,hii ikanifanya kuwa na furaha na mpenzi wangu Idriss"

"Siku moja nilipoamka nilikwenda asubuhi kwa haja ndogo,cha ajabu nikahisi kama kitu kimeshuka na nilipoangalia nikaona damu.Hapo hapo nikampigia Mama na kumwambia mimba imetoka,alilonijibu ni kwamba alinambia mimba haitangazwi.Maneno hayo alishaniambiaga kwamba nisitangaze mimba niliyokuwa nayo lakini sikumsikiliza kwa kuwa nilitaka kuwaziba midomo watu waliokuwa wakinitupia maneno ya matusi."

"Niliumia sana ilipotoka ile mimba,kwani ni kitu nilichokuwa nakitaka kwa muda mrefu,nimechoka kuitwa mgumba,lakini sijakata tamaa najua ipo siku nitapata tena"
 
Nilichojifunza hapa Wema

Anaweweseka

Anaijutia historia yake kwa kuandikwa sana na wino wa kalamu nyekundu..

Hana Amani ya nafsi japokuwa anatabasamu mbele za watu.

Neno "ninge" nadhani linazunguka katika medula Oblangata yake kila mara kwa speed ya Koboko.

Binafsi nimemsamehe, wengi wameishi maisha kama ya wema ila tu hawakupata nafasi ya kuandikwa magazetini.
 
Kioo cha jamii!

Ametutangaza kimataifa!

Ajngewe mnara!

Phyuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!. Hata shetani ana makao.

cc; Nape Nnauye Waziri wa habari, WASANII na michezo. Shughuli yako ya "shujaa wa taifa" imeanza kulipa. Naona Wema hataki kukuangusha anaongeza jitihada za kujitangaza na kuitangaza nchi.
 
View attachment 350824

Katika Mahojiano yake na Waandishi wa Kampuni ya New Habari(2006) Ltd,Wema Sepetu anaanza kwa kusema

"Nilipokuwa na uhusiano na Marehemu Kanumba,nikiwa naishi na wazazi wangu,niliwaza kama wakijuwa nina Mimba wangejisikiaje?Na pia sikuwa tayari kwa kipindi hicho kuwa na mimba,na utoto pia ulichangia,nikatoa"

"Wanaume wote waliofuata hapo akiwemo Chalz Baba,Jumbe na Diamond sikuweza kupata huo ujauzito wala aina yoyote ya kichefuchefu,Lakini nilipoachana na Diamond alipokuwa na mwanamke mwingine nikasikia amepata ujauzito,kiukweli niliumia sana,nikafikiria kwamba mimi ndiye nina tatizo au ile mimba niliyotoa wakati wa Kanumba ilikuwa ndio pekee niliyojaliwa na Mungu,baada ya hapo nikaanza kumsumbua Daktari wangu,daktari alinipa dawa mbalimbali na kuweka sawa viamsho mwilini,lakini dawa hizo zikaishia kuninenepesha tu"

Wema Sepetu anaendelea kusema
"Wakati nikiwa na Idriss,nikashangaa baadhi ya watu wakaniambia nina mimba,lakini sikuamini nikaenda kupima nikiwa na lengo la kusafisha kizazi lakini daktari akaniambia vipimo vinaonyesha kweli nina ujauzito.Nilifikia uamuzi wa kusafisha kizazi sababu nilichoka kuitwa mgumba"

"Baada ya kukugundulika ujauzito huo nikapiga picha na kuzituma kwenye mitandao nikionyesha tumbo langu,ili kuwaonyesha watu kuwa si mgumba ambapo wengine walishika tumbo langu wakifurahia,hii ikanifanya kuwa na furaha na mpenzi wangu Idriss"

"Siku moja nilipoamka nilikwenda asubuhi kwa haja ndogo,cha ajabu nikahisi kama kitu kimeshuka na nilipoangalia nikaona damu.Hapo hapo nikampigia Mama na kumwambia mimba imetoka,alilonijibu ni kwamba alinambia mimba haitangazwi.Maneno hayo alishaniambiaga kwamba nisitangaze mimba niliyokuwa nayo lakini sikumsikiliza kwa kuwa nilitaka kuwaziba midomo watu waliokuwa wakinitupia maneno ya matusi."

"Niliumia sana ilipotoka ile mimba,kwani ni kitu nilichokuwa nakitaka kwa muda mrefu,nimechoka kuitwa mgumba,lakini sijakata tamaa najua ipo siku nitapata tena"
kama kweli anakiri mbele ya uma kufanya kosa hili, kosa la kuua, akamatwe mara moja afunguliwe kesi. kama kuna mtu mwenye audio utakuwa ushahidi mzuri dhidi yake.
 
Iwapo anaamini uwepo wa Mungu atubu hiyo dhambi ya kuua kama bado hajafanya hivyo, Mungu mwema atamsamehe na kumjalia haja ya moyo wake.
 
Jmn ucchana na ujana kila mtu anaupitia,ila upumbavu wa wema ni mmoja kuaniaka hta vtu ambavyo vinamcoast na hili ni tatizo la bongo movie krbu wte hawajitambui kbsa wwpo mbele ya media wanaropoka tuu!!!rejea mahojiano ya jack na zamarad ni uupuz mtupu!!mengne ni aibu inabid tuu yabak moyon lla wao ili wazid kuandikwa bac ya chumban yte hadharan lol!!!
 
Hajatajwa muda mrefu ke' wenzake wapo busy na ndii ndii ndiiii....Kaamua kutoka kivingine.. Umaarufu kweli mzigo
 
Back
Top Bottom