Daddy! My Daddy!"
Akamwambia sikiza bi mkubwa una mimba kivipiiiii? Nina mimba yako ndiooo. Okay so si unaitoa? Akajibu SITOI nazaa. Unazaa vipi na mumeo itakuwaje? Itakavokuwa! Itavokuwa vipi, manake mimi shombe shombe huyo mtoto lazima itajulikana ni wanguuu. Maana mashombe mtaa huu ni mimi na wapemba wa pale juu. Mi sitoi ndo nimekutaarifu.
K akasema wewe mama hunijui. Akamsikizia kama miezi miwili akaona kweli mimba inakuaaa, akanza design kuleta story aachane na mumewe waoane. Mxiuuuuuuu. Alihama nyumba usiku wa saa 7. Asubuhi watu kustuka hayupooooo. Kahamia sehemu tofauti kabisaaa, na pande hizo hakatizi kabisaaa mpaka kesho.
Mi namwambiaga mwanao anakaribia kuzaliwa kule, yupo atajijua. Mi sina mtoto. Hahahaaaaaa! Nikamwambia sio vizuri ujue. Akasema mwenyewe mtoto wa nje simjui baba yangu wala nini. Nimelelewa na baba wa kambo hivo hivo kibishi so my son or daughter will be good. Sema nitakuwa naangalia umri, mashombe umri wa mwanangu huko mbele nitakuwa sili manake nisije mla mwanangu wa kumzaa.
Nikamuuliza lakini baba wako wa kambo si alikufanyia wemaaa, kwanini usilipe wemaaa. Aaaah im my fathers son. Damu inafata mule mule tu. Too bad ila ndo imebidi iwe hivo. Baba wa kambo mwenyewe katili tu, mimi kisa mtoto wa nje kanisomesha shule za bei rahisi, hajaniandikia hata kitu kimoja cha urithi. Basi tu anamheshimu mama na kumtunza ndo maana namstahiiii.
Ila sijui kwamba namuona baba au vipi walaaaa. Mimi sikuwa mtu wa kuishi hivi. Baba ana uwezo mkubwaaa mnooo, ila hanisomagi kitambo tu, so na mimi nishaacha kufatilia, naishi nipo kama sipo. I just dont pay attention to details, na ndo maana siendi home, wala huniskii nikitaja home. Simuitagi baba, namuita baba flani jina la mdogo wake.
Nikamwambia maybe your step dad cut you loose sababu ya tabia zako hizi chafu chafu za umauuuni, na kutosjika dini ndo maana hamwendi sawa. Maybe hujiongezi kushukuru, maana japo sio mwanao kakulea ujue. Ukute hakupi kitu maana umeondoka home kama mna ugomvi. Sio vizuri ujue. We jaribu kujiongeza, it is not too late. Wewe sahivi unaweza lea mtoto wa mtu? Mmmmmh! Akakaaa kimya tu.
Basi akaja kuniuliza nijiongeze vipi? Nikamwambia mpigie simu, muite baba nakusalimia nimewakumbuka. Mxiuuuuuu! Akasema we humjui yule anakatisha tamaaa balaa. Nikamuuliza wewe na tabia zako unatia moyo? Ukizingayia mzee wako mtu wa dini hatariiii. Akasema nitajitahidi.
Akampigia, baba shikamooo! Nilikuwa nawasalimia. Akajibiwa leo ndo unajua mimi baba yako? Miaka yote huko uliko hukuliona hilo? Hata salamu? Mimi si baba yako, kamtafute baba yako. Akakata simu. Mmmmh! Akaniambia umeonaaa. Nikamwambia sio hivo, we ulifikiri umechuna miaka ukipiga leo atakupokea kwa vifijo? Unatakiwa upige kila siku mpaka hasira zitamuisha.
Ikawa anapiga anajibiwa kunya, hivo hivo. Mara aambiwe nimekaribia kufa nini mbona unanipigia sanaaa. Hahahaaaa! Ila yale majibu ya kunya yakawa yakipungua ukali. Basi baadae asipopiga baba yake anampigia, akamwambia njoo nyumbani. Ikawa sasa wako in good terms sio baba akingia K, anatoka nje. Mama yake akafurahiii. Akasema hatimae mmemaliza tofauti zenu naweza sema nina familia.
Ikawa siku baba yake akanza kumtumia 1 million anamwambia zuia tu hio ufanye mambo yako. Hivo. Kidogo ikawa hata akijisikia kwenda kwao hawaziii na kuwazuaa. Ila mtoto akawa ndo kamsusa kabisaa hataki hata kujua mimba inaendaje.
Ndo siku isio na jina akaafutwa na designer mkubwa sanaa Insta. Akamwambia ana show yake, kamuona muonekano utafaaaa, aende Masaki wakaongeee.
ITAENDELEA.