Weekend story: Bad wives

Weekend story: Bad wives

Hii sehemu imezidi utamu wa kushawishi kuisubiri hata siku nne .....thank you Lara moko
 
Mmmhhh yan najikuta nasoma na sina cha kuchangia...asante lara1 hii stor niko speechless
 
Nacomment kabla cjasoma I missed u badly lara

Mi naogopa kudandia gari kwambele sikunyingi sana sijaingia humu sa Nawaza hapa ntaanzaje kusoma ili twende sambamba majukumu nayo yameniandama???? na ili nielewe vizuri mpaka nianze mwanzo ila scenes za update nazoongea zina utamu wake. Too late for me argh!!
 
Duh, wanawake sio wa kuwaamini kabisa, yaani pamoja na love yote anayoshow askari bado dem anataka kumzunguka,
 
Hata mimi Sidney na Mr wananipa wakati mgumu. Sidney hapana, mhurumie mtoto wa mwanamke mwenzio. Ahsante Lara1, hii kitu si ya kitoto!!!
 
Hahaha eti mtoto angekua wako angeshakufa kabisa lol mama si kwa kumtetea mwanae haha... Samaanini ndokwanza nimeanza lol head girl atulie Sydney kipya kinyemi hohooo
 
The Exit Game. Sidney, Amar, Mr. Police.

Amar.

Nilipotea mda mrefuuuu sanaaa, nilikuwa Israel huko nafanya michakato, nikaenda na Urusi kufanya michakato. Sasa kupata vibali vya kusafirisha yale mambo sio rahisi, ikabidi niende Sudan, kutafuta vibali vya kuagiza silahaaa. Yaani nimefight nimefight mpaka nikafanikisha. zitaenda Sudana na baada ya Sudan zitakuja Bongo na meli.

Nimerudi bongo nasikia tu Sidney kaolewaaa, mmmh nikashangaa kundoka kidogo tu kaolewa tena anakaribia kuzaaa. Nikapiga mahesabu yangu nikaona mara ya mwisho kulala nae mbona kama mimi ndo baba. Nikawa nikimpigia akisikia sauti yangu anakata simj. Hataki kunionaaa kabisaaa.

Nikaja kusikia kazaa mtoto, roho inaniambia bwana mtoto wako. Sasa kimbembe kamuhamishia kule quaters siwezi kabisaa kumpata. Alivokuwa Regency anakaa na mkwewe sijui mda wote. Nikaona kazi kubwaaa ila yule wangu najua jinsi ya kumpata.

Nikaenda kwa mama yake Sidney na kumwambia najua mtoto ni wangu, sasa mwiteni niongee nae, ama sivo naenda kutibuaaa kule. Mama anafadhaika na hivi alivokuwa hanipendiiiii. Akakubali kumita akampigia simu. Nasikia Sidney anasema sitaki kujaaa, sitakii aniache. Mama anamwambia ndo baba wa mtoto njoo tu tuta yamaliza.

Akaja basi eti haniangaliii usoni jamaniiii. Na mimi simuangaliii usoni Basi hasemiii. Nikamwambia mama tupishe tuongeee. Mi nikajua na ufirauni wangu wa hapo kati haitakuwa kazi rahisi, ila baada ya mtoto nilikuwa tayari kubadilika kabisaaa. Nikamchukua kwanza mtoto kweli damu yangu kananichekea, Sidney haniangalii usoni.

Nikamuomba kwanza msamaha, nikamwambia zile hela zimefika a good time, Mungu katuletea double joy. Nikaanza how i love her so much ma nataka kuondoka nao, turudi marekani. sisi bado tulikuwa na green card zetu, so haikuwa ishu kabisaaaa. Nikamwambia tunaenda Congo, tukitoka ni one way USA.

Akaanza kusita sita simsomi, nikamdaka kwanza na denda moja balaaaaa. Basi nimewakumbatia wote na mwanangu. One happy familly. Kumpa mate akakumbuka mimi nani kwake. Akaanza kuniambia Police anakusaka, anajua kila kitu we jisalimishe tu atakusaidia. Nikamwambia wa kutusaidia ni Mungu tu. we unafikiri mi na huyu mtoto naweza kufanya makosa. Niamini mimi Sidney sijawahi kushindwa.

Nikamwambia rudi ili asistuke. Tukawa tunawasiliana sanaa, naenda kumuona clinic, au njiani, nikamwambia tengeneza passport ya dogo na jina silitaki hilo. Majina mengine damu haziendani yataleta nuksiiii. koo haziingiliani. We were set to go.

Akaja kunipigia maejuakuwa tunaondokaaa, ameniuliza indirect namwambia tulia hata akijua kwa ilipofikia hawezi kufanya chochote. Tarehe 3 usiku njoo, asubuhi saa 11 tunangoa kambi. Usimuage mama yako hanipendi hatari atampigia Polisi mi nakwambia.

Nikawa nampa mahaba mazitooo, ili mradi tu kumuweka vizuri. Basi ananiambia Polisi kajua unapita Congo tarehe 8 amejiandaa. Akasema ndo maana tunapita tarehe 5. Akija tarehe nane akute manyoya tu. Hio tarehe ilivofika usiku akaja na mtoto, na kibag. I was set to gi with my family, Usiku tumelala mwanangu hata hakusumbua kama alijua yuko na baba yake kipenzi.

Usiku Sidney hatulii ananiuliza maswali mia kama vile ana mashaka kwamba tutakamatwa. Ikabidi nimtoe shaka kuwa wazitooo wote wa nchi wametoa baraka zao. Ashtukaaa. Kwa hio Police mbona anasema tofauti. Nikamuhakikishia police hajua chochote by the time tunapita boda, he will remain nothing but a joke. Mi nina vibali vyote vya kupitisha hizi silaha. Zinapita kama za UN za kusaidia kulinda amani, wanaohusika wote washapewa chao. Nisingeweza ku risk maisha yako na ya baby wetu bila kuiamini hii kazi. Akasikitika maskini polisi. Namtoa shaka he will survive usiwe na shaka.

Siku ya safari ikawa inaenda ndivo sivo kwa mambo mengi sanaa. Yaani niliboreka na vitu vingi sanaa. Ila anyway nikawa niko off mood kabisa. Siku ya mikosi ni mikosi tupu, nimefika border Polisi huyu hapa yuko na timu yake nzima.

Akaja kunikagua sina shaka nikamuonesha vibali halalk hakuamini jicho lilimtoka sio kidogo. Anakagua vile vibali mara laki 5. Baadae akashindwa kuvumilia na kusema hata pamoja na vibali ananizuia pale pale na kuita press. Nikamuita chemba akaja kwa kujiamini akijua nataka kumpa rushwa. Nikamwambia tu, mzazi mwenzangu, kwa mda ambao sikuwepo ulinisaidia majukumu yangu, iko hivi i will do you one favor to settle the score.

Inside story ma boss zako muhimu wote washapewa chao kitambo. We umetumika tu kama kutusindikiza kuhakikisha hatupati matatizo au siwazunguki. Akawa anabisha muonho wewe amar kwani sikujui, you cant fool me. Nikamuonesha chats zangu na boss kubwa akinitakia safari njema na kusistiza mizigo yote ipitishiwe nchini ikibidi. Nikamionesha chat ya boss wake akiniambia keshamshughulikia kumtoa kwenye kesi hivo hatonisumbua. Nikamuonesha mpaka chati ya waziri. Alichoka. Nikamuonesha transfer za hela ndefu zilivofanyika kwa ndugu zao. Akajua pale hana kesi wala mjukuu wa kesi. Nikamwambia unanichelewesha, mke wangu ashatangulia atakuwa ananisubiria na mwanetu. Akaanza kuulizia sidney alipo, ilihusuuuu?

Nikavuka border lile kibabe nahisi nilimuacha na homa huku nyumaa. Al

********************************

Mr Policeman!

Sikuamini kama Amar kapita katikati yangu na kwenda zake, kama Yesu alivopita kati kati ua wale wana sinagogi waliotaka kumtupa nje. Nilikasirishwa na mambo mengi sanaa. I couldnt believe i was used beyond words na ma boss zangu. Ilikuwa nikifika tu Dar naacha kazi. Roho iliniuma kwa vingi. Nikawaza i could even have made Amar my partner. I was so stupid, i was so dumb, nilijilaani sio kidogo.

Maumivu mengine nikawa nawaza Sidney kaniacha tenaaa, after everything i have done for her. Nilikuwa na maumivu mengi sanaaa. Nikawaza huu ndo ule muda wenzangu wanasafisha bunduki zao na kujielekezea kichwani. Niliwaza jinsi gani jeshi lilivooza. Nikawaza yani wanawake wengi kwanini nahangaika na yule boyaaa, niliwazaaaa sanaaaa.

Nikawaza asingeondoka i would have been the happiest man in my life ila ndo kaondoka tenaaaa. Kufika dar toka Kigoma japo nilipanda ndege ila nilichoka sanaa, kama mfu, nikasema ngoja niende nyumbani kwanza nikapate akili kwanza. Nimefika home hivi kuingia naona nyota nyota nikaamua kwenda police mess. Nikanywa, nikanywa nikanywaaa. Nilikunywa sanaa basi tu, kupata valium ya matatizo.

Jioni nikiwa nimelewa chakari nikajikokote mpaka kwangu nikaingia ndani. Nikawa namuona Sidney, namuona katoto ka Angela, yaani naona tunakaa anaisemesha vitu sielewi vitu gani ila tumeongeaa kabisaa, nikamwambia naenda kulala. Pombe sio chai.

Nimestukaa asubuhi nasikia shower inawakaaa bafuni, nikasema ulevi huu nitakuwa nilifungua usiku sikuifungaaa. Nikawza maruwe ruwe ya jana. Hamad nasikk kitoto kinalia. Nikasema akili zangu tu. kikalia tena. Nikakiona kipo kabisaa kitandani kwake.

Nikafurahiii, nikajua kumbe ndo maana hakuwa kwenye gari la Amar, alirudi kwa ajili yangu. Nikaruka kukawahi katoto. Kanichekeaaa. Nikajua Sidney yupo bafuni. Kitoto kile kikalala tena, sikukawia nikawahi huko huko bafuni, hakukuwa na mda wa kupoteza. Nimefika bafuni nikamuwahi na mate mali zangu mwenyeweeee.

Sikuuliza nini wala nini. Na yeye hakusema nini wala nini tukapena mambo moto moto mazitooo, matamu balaaaa. Kule kule bafuni. Hata sikumuuliza kama Dr alimruhusu au vipi. Baadae ndo nakuja kukumbuka kumuuliza kama Dr. alimruhusu, akasema ndio alimruhusu.

Sikwenda kazini wala nini, nilitaka kukaa, na baby wangu siku nzima tunapeana mambo. Mchana nikapigiwa simu kuna dharura niende, nikaenda ghafla, Kufika boss ananionesha habari za online

AMAR KAFARIKI HUKO CONGO, JANA HIO BAADA YA KUVUKA TU BORDER AKAPIGWA RISASI. HABARI ZIMETOKA GAZETI LA CONGO, NA PICHA YA MAITI YAKE IKIWA IMEVUJIA DAMU.

Habari zilikuwa kifaransa ila baada ya kutranslate ikaonesha imeandikwa raia wa tanzania mwenye kibali cha kuishi marekani Amar Mohamed Ali, amekutwa amekufa akiwa amepigwa risasi kadhaa mwilini. Passport yake ikawekwa pale. na green card yake.

Nikachoka mwili na roho.

INAENDELEA SAA 5 NA NUSU USIKU HUU.
 
Sterling hafi mapema hiviiii...anaaanzaje sasa!? Hahahah...hiyo ni chenga la macho kwa Mr. Policeman! Uwiiiii hii story sio ya mchezo kabisa... Aiseeeeeeeeh
 
EPILOUGE!

Sidney!
Kifo cha Amar kilibadilisha mambo mengi maishani mwangu, sikutegemea itafika siku Amar angefariki, nilijua tu he would be luckier and luckier. Nikawaza tungekuwa wote wa 3 ndo tumekubwa na kiama kile, kama sio kumtoroka hotelini asubuhi siku ile tunbekuwa wote wa 3. Jamani.

Ilichukua muda kuamini he was gone for good, and he was not going to come back. Ingekuwa people can come back from the dead Amar angekuwa wa kwanza kurudi. He was gone and never coming back. Kila nikimkumbuka mpaka kesho nalia, nalia machozi. Alizima kama nyota ya jaha, ghafla tu. Life can be so short.

Police tumeona kabisaa na nimezaa watoto wengine 2 wa kiume, wakike yule yule wa Amar, we are going strong. siku hizi ana hela hela sijui anapata wapi, na yale mambo yetu anayawezaa. Kungwi alinielekeza mambo ni kupendanaaa tu, zile ishu mnaelekezana tu mbona atakuja kuweza mpaka ufurahi. Unamuelekeza anaelewa, wanaume hawanaga shida wanawake woga wetu.

Nikamuelekeza akaelewa tu, basi toka nimtoroke Amar na kurudi huku ananipenda sanaa, anafanya chochote nitakacho mwambia, hadi chumvini anazama kabisaa, hahaaa, bado tu ile ya bangi sijamjaribishia namuhesabia tu siku.

**************************************************************

Mr. Policeman

"Afande tusaidie wenzio tuna mzigo unataka kupita naona mambo magumu." Nikawaangalia machoni na kuwaambia "Itakuwa million 15 kufumbia macho na kuhakikisha vijana wote hawaoni huo mzigo ukipita na 25 millions kama mtahitaji escort yetu. Wakajadiliana wakakubalina kutoa 25million.

Hakukuwa na mla rushwa mkubwaa pale kama mimi. Nilikula kila rushwa, na kila hongo. hata alizokataa DCI na IGP mimi nilikula. Sikuogopa nini wala nini, sikujali nini wala nini. Amar taught me EVERY BODY HAS A PRICE, AND I JUST FOUND MINE.

IF YOU CANT FIGHT THEM JOIN THEM .

*******************************************************************

Amar!

Baada ya kuvuka border nikakuta Singa anningoja na wanamgambo wa kiislamu, Alshabab. Kumbe ule mzigo ulikuwa hauendi Congo ila unaenda somali. Singa singa akasimamia show, ikaishaa, wakalipa wale wanamgambo, kabla hawajaondoka Sibga singa akaniuliza do you wanna be my partner. Nikajibu Yes. nataka mgao, maana anga zimebadilika angani sikuwa na jinsi tenaaa.

Singa singa akanitwanga risasi moja ya kifua. Nikaona giza. Nikajua ule ndo mwisho, picha ilionijia mwisho ni ya mwanangu. Ghafla nikashtuka naitwa General Umar! General Umar, nikashangaa inamaana nishafika Kuzimu na General tayari, makubwaaa. Nikawa nashangaaa, nawaona warabu tu wale wenyewe.

Akaja Singa Singa, nikawa namtizama tu, akaniambia samahani kwa kukutwanga risasi, ilibidi ufe kwanza kabla hujawa partner wangu. Ilibidi ufe, uache identity yako, makaratasi yako na document zako zizikwe pamoja na wewe.

Tunavoongea kila mtu anajua umekufa na technically umekufaaa, maana kifo chako kilitangazwa magazeti mengi sanaa. Ndugu zako wote wanajua umekufa, tuliwapelekea mwili wakauzika kabisaaa. Ulikuwa umeharibika vibaya so wasingeweza kushtuka.

Now you ar my partner, you have no name, no identity, nothing, you are like a ghost. You can travel any where any time, unachagua tu documents unazotaka kutumia. Uwe raia wa nchi gani. Sisi sio magaidi perse ila tuna wa supplly magaidi silaha. their wars are not our wars, but we give them the means to win if they can afford.

Welcome to your new life. Usijaribu kuwasiliana au kurudi kwenye familia yako, utakuwa vulnerable, magaidi wataitumia familia yako kukufanyisha kazi za bure. Just be like me, a man without a name, or family. leo Singa singa kesho bohora, kesho kutwa mpakistan navotaka mwenyewe.

I ALWAYS WANTED TO DO SOMETHING BIG WITH MY LIFE, I WNATED TO BE IN BIG CRIMES, NOW I WAS INVOLVED IN REAL WARS, OF REAL CALIBER. AND BIG ,ONEY IS IN BIG WARS.I KIND OF LIKED MY NEW LIFE!

THE END.
 
Back
Top Bottom