"we ua tu baba ..si ndoa yako hii!!"

"we ua tu baba ..si ndoa yako hii!!"

ngoshwe

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2009
Posts
4,141
Reaction score
950
Siku moja wakati naingie "filling station" pale Kimara Resort ORYX, yapata saa saba na madakika fulani mchana, mara ikaja gari ndogo, jamaa nae alikuwa anataka kuweka mafuta, akasimamisha karibu na mashine ya mafuta, akashuka akaelekea upande wa pili, akafungua mlango wa abiria. Ghafla tukashtukia anamchapa makofi dada aliyekaa upande wa abiria kumbe ni mkewe ..."waaap, wap,wap' kisha akasonya.."swiiiiiiiii, pumbavu" ..Mama akawa bado amekaa kimya, akafunika sura na mikono akaanza kulia...

Binafsi na watu tuliokuwepo hapo hatukupendezwa na ile tabia. Lakini mama hakushuka kwenye gari na jamaa akaiingia akaomba awekewe mafuta, alipomaliza wakaondoka haooooooooo....

Baadae nikajiuliza sana, sikujua kisa lakini nikakumbuka wakati fulani nilisikia visa vya kina mama wa kingoni wakati huo nasome sekondari kule Songea (Peramiho) wakipigwa na waume zao hawataki kutoka nje wala kuruhusu mtu aingile ugomvi ..wanasema kwa kingoni "KOMAI TU BABA,...KWANI NDOA YA NANI, SI NDOA YAKO HII??" ...yaaaani "WE UA TU BABA ..KWANI NDOA YA NANI, SI NDOA YAKO HII??"!! (samahani wangoni kama nimekosea mnaweza kusahihisha lugha hapo). Tafsiri yake ni kuwa Mke alikuwa akitetea mdoa yake, atajitahidi kuvumilia hata kwa kipigo cha namna gani. Wakati ule, hata mke akiumizwa namna gani, atamfichia mumewe siri, hakuna atakae jua na hata wakijua, ukipeleka shauri kwa "Mjumbe", mwanamke hawezi kwenda kutoa ushahidi.

"
Jamaa aliefahamika kwa jina la Kwingwa Mhina wa Kigogo Luhanga akimpiga mkewe mara baada ya kuhitilafiana"


Najiuliza tena na tena kwa nini, baadhi ya wanaume katika jamii zetu (Ukiondoa kule kenya ambapo kuna wanawake wanapiga waume zao) ni wepesi sana wa kupiga wake zao.??

Nini tafsiri yake kumpiga mwenzio? Unamfundisha, unamwadhibu au unamdhalilisha??, Je, unapompiga unamfananisha na mtoto kuwa hasitaili kufanya vile alivyofanya??...Wapo wengine ambao hawana staa, wanaweza kupiga mke hata mbele za watu, wakubwa waliowazidi umri nk..hii inatokana na nini? ni hasira, mfumo Dume, AU ??

Tujadili..

mwanamke-akimpiga-mwanaume.jpg


Mwanamke wa kikenya akimpa kichapo mumewe,utamaduni huu umechukua sura mpya kwa sasa nchini KENYA

 
Last edited by a moderator:
Kwetu sijapigwapo, ukanipige wewe?!
 
LOL! Mimi hiyo picha ya Mhina wa Kigogo Luhanga ndo imeniacha hoi. Hilo likaptula alilolivaa mweeeeeeeeh!

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Pengine kwenu hukuwa na fujo. Wengine msipopigwa mnahisi hampendwi....

Mtu asipopigwa utotoni ambapo hata akili za kufikiri vyema hana, maana yake hahitaji kupigwa utuuzimani ambapo akili zake zishakomaa

Kama wapo wanaohisi wasipopigwa hawapendwi, mimi si mmoja wao
 
Hapo naona umeongeza "ngeli"...!

Kiswahili uwanja mpana, kuna cha Kimvita, Kiunguja, Kimombasa, Kipemba na cha kule Mrima

Kama hujaelewa sema ueleweshwe, manake naona hata "ngeli" ni nini bado hujaijua
 
Mwanaume ampigaye mkewe kwa lugha nyepesi tu ni kwamba hana akili....
If you believe kwamba mke ni sehemu ya mwili wako sasa kwa nini unampiga, mbona mguu ukikupelekea ujikwae kidole huwa unajikunyata kwa maumivu na kushirikisha parts nyingine za mwili kufariji kidole na hatimaye maumivu kuyeyuka...iweje huyu ambaye ni nyama na damu kati ya nyama na damu yako apokee kerebuuu.
.....I doubt watu wanaoa wanawake ambao hawakupaswa kuwa wao...
 
Unajua hili la kupiga, huwa nalitafakari sana halafu nashindwa kupata jibu.
Unampiga mkeo, kisa? I mean kosa gani linalostahili kipigo? (kukutukana, kukusaliti, kutokukupikia au?
Mfano kakutukana, maana yake si hakiheshimu; sasa ukimpiga ndio ataanza kukuheshimu?

Au labda umekamata text message ya mapenzi; ukimpiga ndio utamfutia feelings za huyo anacheat naye?

Au una mpiga kwa kuwa umekasirika:
Je kupiga ndio reaction yako kila unapokasirika? Boss wako akikukasirisha unampiga? Au mwanaume mwenzako unampiga? Obvious ni hapana.

Unampiga mkeo kwakuwa ni dhaifu wewe (coward), umeshindwa kureason naye ndio maana unaishia kupiga mtu ambaye si sawa yako, kwa maana hawezi kujitetea. Na kwa ukawardi wako huna uwezo wa kumuacha au kumfanya akupende, akuheshimu kama mwanaume. Ukawardi wako ndio umemfanya akudharau in the first place. Kipigo sio tu kitaongezea dharau bali kitaleta chuki na uhasama pia.

MWANAUME hapigi mwanamke, bali anasababisha respect, admiration, love n dependency.

Hii ni conclusion niliyofikia mimi Kaunga.
 
Unapigwa vizuri sana! Tena makofi ndo dawa yao ili kumuonyesha kuwa nani ni superior kati yenu! Tena kama wewe unayejidai mbishi ndo mzuri kweli....

So you are not superior ndio maana unajihakikishia kuwa wewe ni superior, Mungu wangu pole sana. Ndio maana walisema violent people are very inferior; umenihakikishia Leo.
 
Prophet Muhammad said "Those who do so (beat their wives) are not the best among you".

Ujumbe umefika.
 
Ngumu sana aisee. Paw akitaka kufa, aniguse, namaanisha!
Abusive relationships are too unhealthy na zinaathiri hata watoto. Mkiona mnapigana bora muachane miwe mnatembeleana! Brainwashing ya kwamba sijui nalinda ndoa is total ----!
 
Unapigwa vizuri sana! Tena makofi ndo dawa yao ili kumuonyesha kuwa nani ni superior kati yenu! Tena kama wewe unayejidai mbishi ndo mzuri kweli....
mwanaume anaempiga mwenza wake ni mwoga (coward). Mie siwezi kumheshimu mwanaume anaenipiga. Face your issues. Jieleze kama mwanaume, kurusha ngumi ni kumnyamazisha mkeo ili asijue uoga wako.
 
hebu rusha hilo kofi uone?

Kama hujaziona kor.dani zinaelea angani kama kunguru.

Unapigwa vizuri sana! Tena makofi ndo dawa yao ili kumuonyesha kuwa nani ni superior kati yenu! Tena kama wewe unayejidai mbishi ndo mzuri kweli....
 
So you are not superior ndio maana unajihakikishia kuwa wewe ni superior, Mungu wangu pole sana. Ndio maana walisema violent people are very inferior; umenihakikishia Leo.

No tatizo kuna wanawake wana midomo mirefu sana! Sasa inafikia kipindi wewe pilipili zako zishakupanda umekaa kimya kabisa ila yeye anaendeleza kuchonga tu! Ukimpatia kofi moja la haja lazima akae kimya.....
 
Back
Top Bottom