Wazo tete: Kila kituo cha polisi ijengwe mortuary!

Wazo tete: Kila kituo cha polisi ijengwe mortuary!

Ileje

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
13,318
Reaction score
20,768
Kutokana na wimbi la mauaji yanayofanywa na jeshi la polisi kote nchini inashauriwa kuwa kila kituo cha polisi ijengwe mortuary ili maiti zote zinazotokana na mauaji ya polisi zihifadhiwe huko! Hii itapunguza msongamano wa maiti katika mortuary za hospitali na pia kupunguza adha inayowapata watunza mortuary za hospitali hizi za umma!

Tafadhali tujadili kwa hoja!
 
Kutokana na wimbi la mauaji yanayofanywa na jeshi la polisi kote nchini inashauriwa kuwa kila kituo cha polisi ijengwe mortuary ili maiti zote zinazotokana na mauaji ya polisi zihifadhiwe huko! Hii itapunguza msongamano wa maiti katika mortuary za hospitali na pia kupunguza adha inayowapata watunza mortuary za hospitali hizi za umma!

Tafadhali tujadili kwa hoja!

Mkuu kuna kitu umesahau watengewe na maeneo ya kuwazika hao maiti ambao watakataliwa na ndugu zao sababu hii sasa imeshakuwa kawaida ya polisi kuuwa raia kimagumashi magumashi
 
Mkuu kuna kitu umesahau watengewe na maeneo ya kuwazika hao maiti ambao watakataliwa na ndugu zao sababu hii sasa imeshakuwa kawaida ya polisi kuuwa raia kimagumashi magumashi

Mkuu Django, hapa unamchokoza Pinda, atakapoulizwa swali bungeni juu ya watu wanaokataa amri halali za kuchua miili ya ndugu zao waliouwawa na polisiccm atajibu atajibu "nasema zitupeni barabarani karibu na nyumbani kwao tumechoka nasema polisi zitupeni hizo maiti."
 
Serikali kupitia waziri mkubwa inasema imechoka. Swali ni je, paele wananchi nao watakaposema wamechoka nini kitatokea?
 
Mkuu Django, hapa unamchokoza Pinda, atakapoulizwa swali bungeni juu ya watu wanaokataa amri halali za kuchua miili ya ndugu zao waliouwawa na polisiccm atajibu atajibu "nasema zitupeni barabarani karibu na nyumbani kwao tumechoka nasema polisi zitupeni hizo maiti."

Teh.. teh.. teh... mkuu unanifurahisha sana lakini kwa akili za viongozi wetu unayoyasema yanaweza kutokea
 
Serikali kupitia waziri mkubwa inasema imechoka. Swali ni je, paele wananchi nao watakaposema wamechoka nini kitatokea?

Punda akichoka kubeba mzigo hulala chini kama ishara ya kuchoka,binadamu akichoka hupumzika/shwa,vilevile serikali imesema imechoka kwa hiyo wananchi ipumzisheni.
 
Serikali kupitia waziri mkubwa inasema imechoka. Swali ni je, paele wananchi nao watakaposema wamechoka nini kitatokea?
Hata baadhi ya taasisi za serikali zimeonyesha kuanza kuchoshwa na vituko vya polisi! Hospitali ya Mwananyamala jana waligoma kupokea maiti ya mtu aliyeuawa na polisi baada ya kupata kipigo!
 
Mtu unajiuliza; kwa kuwafanyia wananchi unyama hawa polisi wanapata faida gani kama si kujenga uhasama kati yao na raia?!

Itafika wakati watajutia wanayofanya!
 
Nipo mikononi mwa Polisi maisha yangu bado ni mikosi.......afandeeeee!!x3
song by; Sugu a.k.a Mbunge.
 
Mkuu Django, hapa unamchokoza Pinda, atakapoulizwa swali bungeni juu ya watu wanaokataa amri halali za kuchua miili ya ndugu zao waliouwawa na polisiccm atajibu atajibu "nasema zitupeni barabarani karibu na nyumbani kwao tumechoka nasema polisi zitupeni hizo maiti."

Kweli kabisa, hana akili nzuri yule!Uongozi ukishaingiliwa na wendawazimu unategemea nini?
 
Polisi sio jeshi tena la ulinzi na usalama wa raia. Polisi wa leoni majambazi, ni wauaji, ni majangili, ni wauza mihadarati, yaani wana kila aina ya uchafu. Polisi wananuka kuanzia juu mpaka chini.

Hapa hatuna polisi ila tunawendawazimu waliopewa sare za polisi, virungu, bunduki na mabomu kwa ajili ya kuteketekeza raia. Upolisi ni zaidi ya sare, virungu, mabomu na bunduki. Sasa ukiwa na watu wa aina hiyo halafu kukawa na kiongozi mkubwa kabisa mwendawazimu zaidi ya hao akawapa amri "wapigeni!" unategemea nini? Mimi nimeshakata tamaa kabisa na kundi hilo la watoa roho ndio maana nikasema ukiona ndugu yako mwanaume amekamatwa na hao mnaowaita polisi anza kuanza usafiri wa maiti na mazishi!
 
Mie naamini polisi wa tz ni mkusanyiko wa wajinga wasiokuwa na mafuzo wala weledi ktk kazi zao zilizoainishwa kikatiba!

Ni mtazamo tu, mwenye wazo tofauti anaweza kunikosoa.
 
Mie naamini polisi wa tz ni mkusanyiko wa wajinga wasiokuwa na mafuzo wala weledi ktk kazi zao zilizoainishwa kikatiba!

Ni mtazamo tu, mwenye wazo tofauti anaweza kunikosoa.
​Hapana sidhani kama ni wajinga bali akili zao wameweka akiba hadi watakapostaafu na kwa sasa wanatumia za Pinda!
 
Kutokana na wimbi la mauaji yanayofanywa na jeshi la polisi kote nchini inashauriwa kuwa kila kituo cha polisi ijengwe mortuary ili maiti zote zinazotokana na mauaji ya polisi zihifadhiwe huko! Hii itapunguza msongamano wa maiti katika mortuary za hospitali na pia kupunguza adha inayowapata watunza mortuary za hospitali hizi za umma!

Tafadhali tujadili kwa hoja!

una mawazo mazuri ila yamelenga kutatua matatizo ya karibuni zaidi na sio yale ya mbele.
Ushajiuliza kuwa CCM watakapokuwa chama cha upinzani hii hali itaendelea kuwepo au la?
 
una mawazo mazuri ila yamelenga kutatua matatizo ya karibuni zaidi na sio yale ya mbele.
Ushajiuliza kuwa CCM watakapokuwa chama cha upinzani hii hali itaendelea kuwepo au la?
Tunapaswa kuweka kumbukumbu ya kudumu ya awamu hii ya nne kuwa ni awamu pekee tangu tupate uhuru kwa jeshi la polisi kuua watu wengi hadi mortuary za serikali zikazidiwa na kushindwa kuhifadhi maiti na hivyo polisi wakalazimika kujenga mortuary zao!
 
Naunga mkono hoja!Pia tunawashauri ndugu na jamaa zetu waepuke kusomea fani za kuua raia!
Kutokana na wimbi la mauaji yanayofanywa na jeshi la polisi kote nchini inashauriwa kuwa kila kituo cha polisi ijengwe mortuary ili maiti zote zinazotokana na mauaji ya polisi zihifadhiwe huko! Hii itapunguza msongamano wa maiti katika mortuary za hospitali na pia kupunguza adha inayowapata watunza mortuary za hospitali hizi za umma!

Tafadhali tujadili kwa hoja!
 
Back
Top Bottom