waziri wa jinsia uko wapi?

waziri wa jinsia uko wapi?

Bado vichwa vya waafrika vinafikra mgando, Ona hata uzi unaoanzishwa, michango mingine ni ovyo kabisa!
Itachukua muda kubadilika, mleta mada kaulizia maswala ya makundi haya kutendewa "ndivyo sivyo", watu
wanalewa mzaha! ovyo kabisa!
 
Waziri wa jinsia na watoto si ni yule kada maarufu wa chama chetu cha mshikamano; na Kingozi wa Jumuia ya wanawake wa CCM - inasikitisha sana kweli kwa jambo hili wanawake mnatosana wenyewe kwa wenyewe.

Na uzuri zaidi mnae pia Madam Spika wa Bunge letu tukufu mwanamama pia, sasa kwa hili tunapata wasiwasi juu ya kauli mbiu yenu mnapenda kuitamka kila mara kwamba "Wanawake Tunaweza". Tungetemea mambo kama haya na mengine yanayovuma mitandaoni juu ya uyanyasaji wa wanawake na watoto mngeyashughulikia wa umoja wenu kama wafanyavyo wanawake wa nchi nyingine duniani.

Tunapata wasiwasi mkubwa juu ya mshikamano wenu. Mnaruhusu mfumo DUME uendelee kutawala? kama jinsi mnavyoona wanawake wanavyoteswa, kupewa vilema vya maisha, kubakwa, kuuawa, kudharauliwa, kunyanyaswa- just because ni wanawake na nyie mpo mnakula bata tu Bungeni - hasa nyie wabunge viti maalum.

Yule Mwenyekiti wa UWT!
 
huyu joyce ndiyo yule mmewake anamwagia watu tindikali ukiolewa na mwizi lazima usaidie kuiba na ukiolewa na mwagia watu tindikali lazima na wewe uwe unamwagia watu tindikali ndivyo alivyo joice kwa sasa.

We .......unatafuta ...hapa
Mtu mzima ovyo
 
Hii Dunia sasa watu hawaoni huruma kwa wengine
 
hapo ndipo tunapobaini wabunge wamekwenda mjengoni kwa maslahi ya nani. tumeona ushahidi wanapodai pesa zaidi. ma tunaona tena wanaposhindwa hata kudai uchunguzi juu ya mkasa huu.
 
Waziri wa wanawake, Jinsia na Watoto kazi yake ni kuwatisha wanawake walioolewa na wapinzani....Wasiwape unyumba mpaka watakapohamia CCM.
 
:A S 39: Tanzania ukiteuliwa wadhifa fulani basi na uhuru wa kufikiri unaondolewa
 
huyu joyce ndiyo yule mmewake anamwagia watu tindikali ukiolewa na mwizi lazima usaidie kuiba na ukiolewa na mwagia watu tindikali lazima na wewe uwe unamwagia watu tindikali ndivyo alivyo joice kwa sasa.

Huyu ndiyo moja ya kijana imara wa Chama cha Mchina akiwakilisha Wachina wenzake
 
Katika wanawake wanaofanya kazi kwa maslahi mapana ya Taifa ni Bi Joyce Kiria. Anafanya kazi zaidi ya viongozi wetu tuliowachagua kutuongoza na hata kututetea huko Bungeni. Mbaya zaidi wabunge wengi hasa wanawake wamekuwa wakila bata tuu badala ya kupigania masuala kama haya ya unyanyasaji dhidi yao.

Tumuunge mkono Bi Joyce aendelee kuwaonyesha wabunge na viongozi wetu jinsi ya kutumikia wananchi na siyo wao wabobee kula nchi.
 
Sijawahi kumsikia Sophia Lion akikemea haya, really too sad! Watu wanajichukulia sheria mokononi

Si yeye tu, bali wabunge wote wanawake hawajalichukua suala la Ukatili dhidi yao kama Agenda muhimu sana, na wakaisukuma kwa nguvu.

Kazi ni kusema "Wanawake Tunaweza" naona wanaweza kujichubua tu na siyo kuwasaidia wenzao waliowatuma Bungeni kuwapigania hasa kwa mambo ya msingi kama haya ya ukatili, Huduma mbovu za Afya, Maji n.k
 
huyu joyce ndiyo yule mmewake anamwagia watu tindikali ukiolewa na mwizi lazima usaidie kuiba na ukiolewa na mwagia watu tindikali lazima na wewe uwe unamwagia watu tindikali ndivyo alivyo joice kwa sasa.
wewe siyo mzima una matatizo sijui tindikali imekujaje hapa
 
huyu joyce ndiyo yule mmewake anamwagia watu tindikali ukiolewa na mwizi lazima usaidie kuiba na ukiolewa na mwagia watu tindikali lazima na wewe uwe unamwagia watu tindikali ndivyo alivyo joice kwa sasa.

Damu na kilio cha hoa mama kiwe juu yako na uzazi wako.
 
Wako wapi wanawake wanaoweza kumtetea yule yatima aliyebakwa na kigogo? Au ni kwa sababu ni mwanachama na kada wa chama chetu?? Kuna wizara kweli inayotetea wanawake?
 
Haiwezekani Wanawake wafanyiwe unyama huu wakati tuna Wizara tena inayosimamiwa na Wanawake wenzetu! Haiwezekani Wanawake tunafanyiwa unyama mkubwa kama huu na wengine kuuwawa kikatili na Wanawake viongozi/wabunge wamepiga kimya!

Haiwezekani hata kidogo! Kwa matukio kama haya nilitegemea Wabunge Wanawake wawe wamoja na ikiwezakana watoke nje ya bunge ili sheria kali zitungwe na pia Kampeni kubwa sana ifanyike nchi nzima ya kutokomeza unyama huu dhidi ya Wanawake...

Kama Waziri yupo kimya, Wabunge Wanawake Je?

Umoja wenu TWPG unafanya kazi gani ya maana kuliko maisha na Usalama wa Wanawake wemzenu? Haya matukio yakiwatokea ninyi je, mtaendelea kuwa kimya?


Unyama huu umefanyika mwezi wa nane huko kijiji cha Nyantira Tarime Mara.

Ajabu ni kwamba baadhi yetu tumekuwa tukiwasifu ndugu zetu wa Mara hasa wanaume kwamba ni kawaida sana mambo haya wao kufanya, badala ya kukemea tunawasifu. Najua hata hapa kwenye uzi huu tutawasifu kwa ukatili huu wa kutisha.

Wakati mwingine wanawake tunaona hatupo salama kama ambavyo wengi mnadai Tanzania tuna Amani! Kwa habari zaidi bonyeza www.wanawakelivetv.com

naomba radhi kwa picha za kutisha....

Yuko bize na vijana wadogo wadogo.
 
Back
Top Bottom