Joyce Kiria
Member
- Aug 6, 2013
- 50
- 112
Haiwezekani Wanawake wafanyiwe unyama huu wakati tuna Wizara tena inayosimamiwa na Wanawake wenzetu! Haiwezekani Wanawake tunafanyiwa unyama mkubwa kama huu na wengine kuuwawa kikatili na Wanawake viongozi/wabunge wamepiga kimya!
Haiwezekani hata kidogo! Kwa matukio kama haya nilitegemea Wabunge Wanawake wawe wamoja na ikiwezakana watoke nje ya bunge ili sheria kali zitungwe na pia Kampeni kubwa sana ifanyike nchi nzima ya kutokomeza unyama huu dhidi ya Wanawake...
Kama Waziri yupo kimya, Wabunge Wanawake Je?
Umoja wenu TWPG unafanya kazi gani ya maana kuliko maisha na Usalama wa Wanawake wemzenu? Haya matukio yakiwatokea ninyi je, mtaendelea kuwa kimya?
Unyama huu umefanyika mwezi wa nane huko kijiji cha Nyantira Tarime Mara.
Ajabu ni kwamba baadhi yetu tumekuwa tukiwasifu ndugu zetu wa Mara hasa wanaume kwamba ni kawaida sana mambo haya wao kufanya, badala ya kukemea tunawasifu. Najua hata hapa kwenye uzi huu tutawasifu kwa ukatili huu wa kutisha.
Wakati mwingine wanawake tunaona hatupo salama kama ambavyo wengi mnadai Tanzania tuna Amani! Kwa habari zaidi bonyeza www.wanawakelivetv.com
naomba radhi kwa picha za kutisha....
Haiwezekani hata kidogo! Kwa matukio kama haya nilitegemea Wabunge Wanawake wawe wamoja na ikiwezakana watoke nje ya bunge ili sheria kali zitungwe na pia Kampeni kubwa sana ifanyike nchi nzima ya kutokomeza unyama huu dhidi ya Wanawake...
Kama Waziri yupo kimya, Wabunge Wanawake Je?
Umoja wenu TWPG unafanya kazi gani ya maana kuliko maisha na Usalama wa Wanawake wemzenu? Haya matukio yakiwatokea ninyi je, mtaendelea kuwa kimya?
Unyama huu umefanyika mwezi wa nane huko kijiji cha Nyantira Tarime Mara.
Ajabu ni kwamba baadhi yetu tumekuwa tukiwasifu ndugu zetu wa Mara hasa wanaume kwamba ni kawaida sana mambo haya wao kufanya, badala ya kukemea tunawasifu. Najua hata hapa kwenye uzi huu tutawasifu kwa ukatili huu wa kutisha.
Wakati mwingine wanawake tunaona hatupo salama kama ambavyo wengi mnadai Tanzania tuna Amani! Kwa habari zaidi bonyeza www.wanawakelivetv.com
naomba radhi kwa picha za kutisha....