Waziri wa Fedha Punguza Jazba

Waziri wa Fedha Punguza Jazba

Bowie

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2016
Posts
4,373
Reaction score
6,084
Jana kwenye taarifa ya habari saa 2 usiku niliona waziri wa fedha alipofanya ziara ya kushutukiza pale bandarini (dhow). Kwa kweli sikupendezwa jinsi waziri alivyokuwa akiwatuhumu watumishi wa TRA pale bandarini kuwa kiini cha kushuka mapato ya ukusanyaji za forodha.
Kwasasa kiuchumi hapa nchini kununua na kuuza bidhaa kumeshuka kwa kiasi kikubwa na hiyo imesababisha uagizaji wa bidhaa kutoka nje kushuka kwa kiasi kikubwa, ndugu waziri kwanza ukiwa waziri wa fedha na uchumi lazima ufanye utafiti nini kilichosababisha katika kipindi chako kama waziri iwe hivyo. Wafanyabiashara biashara wengi kwasasa wamekimbilia kupitisha mizigo Zanzibar kwanini? Unapotoa vitisho utawafukuza watumishi waliopo pale bandarini kwasababu ya kutokusanya kodi utafukuza wangapi?
Lazima Mheshimiwa Waziri ukae na wadau ujue tatizo liko wapi, kwasasa circulation ya pesa hapa nchini ipo chini sana na hilo ndio tatizo kubwa.
Leo ukimwondoa mfanyakazi wa TRA mwenye uzoefu na kumleta mfanyakazi mwingine kutoka chuoni asiye na uzoefu usitegemee kama kutakuwa na mafanikio. Kwasasa watumishi wote waliopo kazini wapo makini sana kwa masuala ya rushwa.
 
Ulitaka asemeje kwa mfano?
Wale si wapo chini ya wizara yake?
Kinachopigiwa kelele ni urasimu
wa watendaji wa TRA. Wafanya biashara
ukiwazingua wanakimbilia bandari za nchi jirani.
Na wewe unabaki na watu wanaohitaji mshahara
bila kukusanya kodi

Kwa nini asifoke?
 
Ulitaka asemeje kwa mfano?
Wale si wapo chini ya wizara yake?
Kinachopigiwa kelele ni urasimu
wa watendaji wa TRA. Wafanya biashara
ukiwazingua wanakimbilia bandari za nchi jirani.
Na wewe unabaki na watu wanaohitaji mshahara
bila kukusanya kodi

Kwa nini asifoke?
Mkuu kama kuna urasimu Takukuru itawashughulikia. Na sio kwamba wafanyabiashara wamekimbilia bandari zingine ni importation imeshuka kwa kiasi kikubwa. Tatizo lipo kwenye mzunguko wa pesa. Serikali hailipi madeni ya ndani, bajeti ya 2017/18 imepitishwa lakini hakuna fedha zilizopelekwa sehemu husika.
Wafanyabiashara wanaolipa VAT hawarudishiwi fedha hizo za VAT.
 
Hela kaficha mwenyewe,kasahau alipoficha,halafu anatulalamikia sisi,baadae,akija kujiangalia mfukoni,lahaula,anayo,atasemaaa alaaaaaa,yaani nimehangaika muda woote kumbe ni Mimi nilipunguza mzunguko wa pesa na nikawa nashangilia watu wanaposema hela imeadimika!!

Unasema unatunyoosha,sasa umeanza kunyooka na wewe pia,makusanyo puuuuu!! Chini, yameshuka,hao watumishi wa TRA wayatolee wapi kama biashara zetu mtaani zimedoda na hicho ndicho mkisikia zimedoda mnagonga chiaz huko kwenye viyoyozi!
 
Una viongozi hayajawahi hata kufanya biashara ya pipi maisha Yao yote afu waendeshe uchumi. Parchasing power ya mtanzania imeanguka hivyo mzunguko na imports zimesinyaa pia makusanyo ya kodi lazima yatasinyaa. Mabaya yanakuja hata wabunge wao akina aboud na yule wa dodoma mfanyabiashara na Heche walimtahadhalisha mpango kua tunaenda kugonga mwamba.
 
Ulitaka asemeje kwa mfano?
Wale si wapo chini ya wizara yake?
Kinachopigiwa kelele ni urasimu
wa watendaji wa TRA. Wafanya biashara
ukiwazingua wanakimbilia bandari za nchi jirani.
Na wewe unabaki na watu wanaohitaji mshahara
bila kukusanya kodi

Kwa nini asifoke?
Hivi ni urasimu ndo sababu pekee inayo weza kuwakimbiza watumia bandari?
 
Ulitaka asemeje kwa mfano?
Wale si wapo chini ya wizara yake?
Kinachopigiwa kelele ni urasimu
wa watendaji wa TRA. Wafanya biashara
ukiwazingua wanakimbilia bandari za nchi jirani.
Na wewe unabaki na watu wanaohitaji mshahara
bila kukusanya kodi

Kwa nini asifoke?
Na wewe unaona umechangia mada sasa akili yako hao wafanya kazi wakatoe hela mifukoni mwao wailete serekalin maana mkiambiwa wafanyabiashara wanafunga biashara hamtaki kusikia matokeo yake ndio hayo. sasa sijui watamtoza nani huo ushuru
 
Huo ushauri wape waume zako hapo ufipa .

Waambie wajenge ofisi ya chama
 
Huo ushauri wape waume zako hapo ufipa .

Waambie wajenge ofisi ya chama
Mkiambiwa mnatumia masaburi kufikiri,mnatukana!Hoja ni uchumi wa nchi we unaleta ujenzi wa ofisi kama sio upoyoyo ni nini!?Ofisi ya chadema inaathiri vipi maparo bandarini hebu think big brother hili ni jambo muhimu kujadili uchumi wa nchi na mwenendo wetu kama taifa.Tanzania ipo tu hata bila ccm,chadema,cuf n.k tunahitaji uchumi imara kuliko tunavyo vihitaji hivyo vyama vyenu.Muhimu ni mdororo huu unaoonekana kutuangusha utatuliwe sio mnaleta porojo zenu za kisiasa hapa
 
Umekosea tu apo the way ulipomwongelea mwanachuo, useless thinking,
 
Jana kwenye taarifa ya habari saa 2 usiku niliona waziri wa fedha alipofanya ziara ya kushutukiza pale bandarini (dhow). Kwa kweli sikupendezwa jinsi waziri alivyokuwa akiwatuhumu watumishi wa TRA pale bandarini kuwa kiini cha kushuka mapato ya ukusanyaji za forodha.
Kwasasa kiuchumi hapa nchini kununua na kuuza bidhaa kumeshuka kwa kiasi kikubwa na hiyo imesababisha uagizaji wa bidhaa kutoka nje kushuka kwa kiasi kikubwa, ndugu waziri kwanza ukiwa waziri wa fedha na uchumi lazima ufanye utafiti nini kilichosababisha katika kipindi chako kama waziri iwe hivyo. Wafanyabiashara biashara wengi kwasasa wamekimbilia kupitisha mizigo Zanzibar kwanini? Unapotoa vitisho utawafukuza watumishi waliopo pale bandarini kwasababu ya kutokusanya kodi utafukuza wangapi?
Lazima Mheshimiwa Waziri ukae na wadau ujue tatizo liko wapi, kwasasa circulation ya pesa hapa nchini ipo chini sana na hilo ndio tatizo kubwa.
Leo ukimwondoa mfanyakazi wa TRA mwenye uzoefu na kumleta mfanyakazi mwingine kutoka chuoni asiye na uzoefu usitegemee kama kutakuwa na mafanikio. Kwasasa watumishi wote waliopo kazini wapo makini sana kwa masuala ya rushwa.
Unatetea kibarua? TRA wale wanao verify declaration wanapenda sana kuonea waleta mizigo. Akili yenu lazima muiweke kwenye Business oriented,Competitive analysis na Customer expectation sio mnakurupuka tuu. HS Code zenyewe zinawapa shida mmekariri mnapelekea Tariff classification kuwa ya kuumiza.
 
Back
Top Bottom