Slim5
JF-Expert Member
- Jan 7, 2014
- 28,441
- 38,417
Hivi nchi ni Dar tu??!!!!
Ndio wanavoelewa wao
Hivi nchi ni Dar tu??!!!!
Waziri wa Afya aliyeteuliwa na JPM, leo atinga Hospitali ya Mwananyamala
Wafike na huku Ifakara St. Francis Hospital. Watu tunalazimishwa kupima HIV. Mgonjwa hushughulikiwi maradhi mengine mpaka kwanza upimwe HIV.
Ndio wanavoelewa wao
Natumaini aliyewateua anawafuatilia. . . .Wanakosa ubunifu so wanaenda kwa kuiga tu, Na kwa kutaka sifa watahangaika Dar kwenye uhakika wa vyombo vya habari ila hawana ubunifu kabisa wa kuweza kuchukua point 3 kirahisi
rais, waziri wa afya, naibu waziri na katibu mkuu wa wizara ya afya wafanye safari ya kushitukiza Mirembe, waingie kwenye wodi ya vichaa, nahisi kale ka dada mlinzi katapenya kwenye tundu la funguo kuokoa maisha yake
Waziri wa Afya aliyeteuliwa na JPM, leo atinga Hospitali ya Mwananyamala
hamna safari za ulaya na biashara ya kushinda kwenye maofisi na miradi binafsi hakuna tena kilichobaki ni kuwatumikia watanzania kwa kutembelea kila mahali waziri anapohusika.
hivyo sidhani kama wanauza sura ila ni amri toka kwa aliye wateua kwamba matatizo ya watanzania yatatuliwe na viongozi wao.
mwanzo mzuri,tuwaombee wafanikishe ili tusonge mbele.
Hivi nchi ni Dar tu??!!!!
huku si ndo kuna waandishi wanaopatikana kiurahisi...ili kuonesha sifa zao..