Waziri Simbachawene: Watanzania wanataka amani, maendeleo, siyo Katiba Mpya

"Unakuta mtu anasema Katiba ya Tanzania mbaya kwa kipengele kimoja tu cha tume ya uchaguzi, baasi, lakini Katiba hii ndiyo inayopelekea Watanzania wanamiliki rasilimali na maliasili kwa umoja bila ya kuwa na ugomvi.

Shida ya Watanzania siyo Katiba mpya ila shida ni ya wanaotaka madaraka kwa njia nyepesi ndiyo shida yao wanaona ni Katiba, watu wachache ndiyo wanashida na Katiba kwa malengo na ubinafsi wao.
Utapeli endelevu wa CCM na vyombo vyake. Kama Kila Siku wanadai Tanzania ni nchi ya amani na kwamba CCM imeleta maendeleo..... The what is next.

Unless waje wazi kuwa CCM mpaka sasa haijaleta hayo maendeleo na nchi haina amani na sasa ndiyo wanataka kututimizia hayo kwa sasa. This tactics za kuhamishwa magoli kila awamu watanzania tumechoka. Tuna akili...!!
 
UKWELI UNAOKERA! NDIYO!
Kwa sasa Watanzania ninaowafahamu wengi wao hawapo tayari kupigania Katiba Mpya... ccm inajua hivyo!
Kwanza kwa elimu walizopewa za kuunga unga bado hawajui hata umuhimu wa Katiba!
Laiti kama wangelijua umuhimu wake wasingelikubali Jaji Warioba aporwe mchakato kienyeji-kali na kuishia mikononi mwa wanasiasa! Naam Wangelazimisha hadi wangeingia kwenye historia ya kujiandikia Katiba yao! Lakini sote tu mashahidi wa yaliyotokea!
Uzuri ni kuwa hawatabaki hivyo milele! Ipo siku watakataa kurubuniwa kwa siasa za ulaghahi za kuahidiwa huduma za kijamii na amani ya uzabaifu miaka nenda rudi. Wataamka na kudai Katiba waitakayo wao ili kupitia hiyo Katiba waweze kujipatia maji, elimu kamili na maisha bora. Kwa usawa na bila ulaghahi!

NB: Mchakato wowote wa kudai Katiba Mpya kwa utashi wa kisiasa hautokuwa na mwisho mzuri! Katiba ni ya wananchi. Kama hawajawa tayari msiwashurutishe! Mnaweza kulazimishia ikapatikana kwa sasa lakini akaja mfalme Jiwe mwingine akairarua na kuitupilia mbali!
 
Yaani ukitumia muda wako vizuri kuwasikiza kwa makini wanasiasa, unaweza ukahisi sio wanadamu hivi, yaani ni viumbe waliotoka huko anga za mbali na wameletwa duniani kuwapa adhabu wanadamu...
Mwanasiasa ni sawa tu na machinga na matapeli wa viwanja! Ukiwapa muda watakurubuni hadi uingie kingi! Be smart! Always don't follow the masses because "m" tends to be very silent or nonexistent!
 
Na kwe
"Unakuta mtu anasema Katiba ya Tanzania mbaya kwa kipengele kimoja tu cha tume ya uchaguzi, baasi, lakini Katiba hii ndiyo inayopelekea Watanzania wanamiliki rasilimali na maliasili kwa umoja bila ya kuwa na ugomvi.

Shida ya Watanzania siyo Katiba mpya ila shida ni ya wanaotaka madaraka kwa njia nyepesi ndiyo shida yao wanaona ni Katiba, watu wachache ndiyo wanashida na Katiba kwa malengo na ubinafsi wao.
Na kwenye mikutano yote ya ccm mbele kabisa hukaa makundi yasiyojielewa vizee watoto wadogo wakinamama zetu maskini na mataahira yaliyovaa ndala machache au ma wanakijiji yanayopekuwa miguu imeliwa na funza wajanja wanaojitambua hukaa nyuma kabisa au pembeni hivyo Basi kundi la less privileged ndio wapendwa wa ccm.
 
Back
Top Bottom