Waziri Nape ameua kabisa uhuru wa vyombo vya habari

Etwege

JF-Expert Member
Jul 4, 2018
5,738
15,211
Kesi iliyofunguliwa na jopo la Wanasheria wazalendo kule Mbeya kupinga mkataba wa bandari kila mtanzania ana hamu ya kufahamu nini kitaendelea mahakamani katika kesi hiyo, lakini cha kushangaza media za hapa bongo zimekaa kimya kabisa na kinafiki, si redio wala gazeti linaloripoti kuhusu kesi hiyo.

Mikutano ya Chadema na Sauti ya wazalendo licha ya kwamba waandishi wa magazeti na redio wanakuwepo kwenye mkutano lakini hawaruhusiwi kuandika chochote kuhusu mikutano hiyo! Je hapo utajisifu kwamba kuna uhuru wa vyombo vya habari Tanzania?

Nape Nauye kazi yako ya kuuwa vyombo vya habari imeonekana endelea hivyo hivyo kuhubiri mdomoni kuna uhuru wakati kivitendo ni tofauti kabisa.
 
Waandishi wa habariTanzania ni kama digidigi ndani ya mbuga. Yaani nyenzo ya vyombo vya habari kwa sasa vimerudi nyuma kuliko kipindi kile cha vitisho cha Magu.
Hii ni kuashiria kuwa matumizi ya rushwa katika awamu hii ya sita ni makubwa kupindukia. Kwa rushwa hizi lazima nchi ipigwe mnada ukizingatia waziri wa habari kwa sasa ni yule jamaa aliyezuia bunge kuwa live wakati wa Magu.
 
Vyama vya siasa vianzishe magazeti na radio msitegemee kupata favor hii ni vita kubwa sana .Kama wahariri wenyewe wanaongea maudhui tatanishi unategemea equal coverage? Tulipga kelele bunge live lakini baada ya ruhusa ni tv ngapi zilikuwa zinarusha?na hata kipindi kuna jambo nyeti la kujadili bungeni tv zinakatisha matangazo.
 
20230211_120334.jpg
 
Nyani atatema bungo soon,DP World wameshatoa angalizo kwamba kutokana na kesi iliyofunguliwa na Wazalendo kuzihami bandari zetu warudishiwe ile b 100 yao waliyotoa kama kilainishi hawataki tena hiyo biashara. Ndiyo fujo zote hizi hadi kutumia kete ya udini kwani hiyo hela washaigawana.
Hahahahah kumbe walikula bakshishi ya usd 40Millions
 
Uhuru wa vyombo vya habari na habari ulikufa mazima kipindi cha jiwe

Kuanzia hapo media zimekuwa chawa wa CCM na hazina meno ya kuhoji au kuripoti madhambi ya watawala
 
Back
Top Bottom