Waziri Muhongo azomewa!

Waziri Muhongo azomewa!

Hivi we ukoje?

Nipo kama Bwana wako! Mwendesha Bodaboda akimzomea Professor، Prof atapungukiwa na nini au hao Maboda boda wataongezeka nini, Kwanza hiyo habari ni ya kutunga kuwaliza Akili kipunje kama wewe!
 
Churaaaaaa profesa angekuwa mwalimu wangu nisinge ingia clac kwel churaaaaaa la profesali nasikia anaenda zenji na scania ya tot anashow na machuraaaaaas
 
Inabidi hii tabia iendelee kwa viongozi wadhalimu kama hawa mana wanaona wananchi kama mburula vile
 
Kuzomewa na Wendawazimu, Vichaa na Wehu ni Faraja sana kwa Profesa! Profesa chapa kazi kwa Jeuri ya Cham,a tawala Chama cha Mapinduzi
Kashfa,dharau na kejeli ndizo zilizomfanya azomewe na kwa kuwa wewe nawe una akili za ki CCM unafanya makosa hayo hayo ya kuwadharau watanzania kwa kuwaona hawana akili wanapodai haki zao,subiri tu utatoka mapovu sana kwani jeuri tunaiona,zilikuwepo jeuri za KANU Kenya,jeuri ya Gadafi,Saddam nini jeuri ya chama tawala
 
Katika hali isiyo ya kwaida jioni hii, waziri muhongo amepetwa na kadhia ya aina yake hapa Dodoma alipokuwa akitoka kwenye duka la madawa. Vijana ambao wanasadikiwa kuwa madereva wa Bodaboda na wachuuzi, yaani wamachinga, walianza kumzomea kumuita “chura! Chura! Chura! Chura!” hali iliyompelekea Bw. Muhongo kutembea kwa haraka kuelekea kwenye gari iliyokuwa ikumsubiria pembezoni mwa barabara. Baada ya kufika kwenye gari, waliondoka kwa kasi ya ajabu kuelekea ofisi za bunge huku vijana wakiendele akumzomea !

My Take:
Huu ni mwanzo mbaya kwa hawa viongozi wenye dharau na wakorofi wa CCM. Watazomewa sasa hivi mpaka watakoma. Huyu muhongo angejaribu kujifunza ustaarabu kutoka kwa Mawaziri wasaidizi wizara ya Nishati na madini waliomsaidia kujibu maswali

images


Mtu yeyote aliyepewa madaraka kwa kupitia nguvu za giza ni incompetent na siku zote kazi zake huzifanya kimiujiza kwani haelewi akifanyacho. Cha kusikitisha, yeye Muhongo anajiona ana akili ile mbaya na pengine anawaza kugombea urais huyu in 2015 ili aboronge na kuiuza nchi kwa wamalawi au majirani wengine na kusingizia kuwa Tanzania ilikuwa ni mkoa tu siku zote.
 
sipati picha 2015, kwanza huyu profesa si ni mbunge wa ikulu?, anajifanya mtu wa data wakati hakuna lolote niliwakubali sana manaibu wake the way walivyojibu hoja kwa ufasaha. just curious to know kama raisi atakayekuja atampa favour tena au ndo hivyo tena chukua chako mapema.
 
AMA kweli Adui ujinga ataendelea kututesa Wa Tz,Leo mnamtukana prof. Kumbe hamjaelewa Kabisa alichokisema. Nyie ndio ma mburula kweli kweli. Mnachotakiwa kuhoji ni uwazi Wa mkataba Wa gas ili tusije pata hasara,maana wanaoingia mkataba si malaika wanaweza kulaghaiwa na Wawekezaji baadae tukalia ,hii ni Mali yetu sote .
 
Si mlaumu Prof shida ni kuwa bado hajui kuwa yeye kwa sasa sio mwalimu bali ni mwanasiasa kwa bahati mbaya analeta mambo ya shule UBABE hajui kuwa uku hakuna wa kumpa supplimentary.
Anyway maish ni kujifunza pia kuna kkujikwaa na kuanguka
 
Si mlaumu Prof shida ni kuwa bado hajui kuwa yeye kwa sasa sio mwalimu bali ni mwanasiasa kwa bahati mbaya analeta mambo ya shule UBABE hajui kuwa uku hakuna wa kumpa supplimentary.
Anyway maish ni kujifunza pia kuna kkujikwaa na kuanguka
Dah hao wanatakiwa wachukuliwe hatua za kinidhamu, yaani wanamuita professor chura haha haha....
 
mkuu umejaribu kumwangalia vizuri dk slaa usoni ndiye hasa anafanana na chura wala siyo muhongo waangalie vizuri wote halafu linganisha vizuri.

Habar ya dkt slaa imekujaje wakati 2nazungumzia habari ya prof. muongo kuzomewa? kawaeleze waliomzomea huko dodoma. sio kazi ye2 kujua nani kafanana na chura kikubwa muongo kazomewa leo.
 
Dr Slaa anahuskaje tena hapa?? We nae bhana;ustutukanie msomi wetu bana sawa bogus??
 
Suala la Mtwara si la kutatuliwa kijiologia inahitaji viongozi wenye strong political acumen to be able to manage the political and economic concerns za wana Mtwara. Bahati mbaya sana waziri wetu (Prof Chura????) analeta utaalamu wake wa geology kwenye suala la maisha ya watu- livelihood!!!
 
sipati picha 2015, kwanza huyu profesa si ni mbunge wa ikulu?, anajifanya mtu wa data wakati hakuna lolote niliwakubali sana manaibu wake the way walivyojibu hoja kwa ufasaha. just curious to know kama raisi atakayekuja atampa favour tena au ndo hivyo tena chukua chako mapema.




Isije ikawa mafisadi wanamchukia prof kwa kazi Nzuri anayofanya pia isije ikawa waliopoteza uwaziri wanautaka Huyu ndie Mwenye nia ya kweli ya kutatua umeme na pia kuhakikisha tena hatusaini mikataba isiyo na masilahi
hii NI hazina mtakayo Ikubali baadaye! Kuna Misemo ya kiswahili! Kibaya chake NI nini?
 
Dodoma imejengwa kwa hela ZA Kanda ya ziwa, dar, na watanzania wote
Iko siku uranium ikipatikana wana Dodoma nao wanaweza thubutu sema haitoki,
Kibaya NI kile tu cha viongozi wa juu wa nchi hii na familia zao kuhamishia resource ZA Mikoa mingine kuzipeleka walikozaliwa viongozi na kuacha kiduchu au HAKUNA Kabila Huko ipatikanakoi, hii TABIA NI ya kishenzi sana na ikomeshwe
 

Souece;TZ Daima

BAADHI ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Tabora jana walipata wakati mgumu baada ya kuzomewa na wananchi kwenye mkutano wa hadhara.

Tukio hilo lilitokea kwenye mkutano wa hadhara ulifanyika viwanja vya stendi ya mabasi zamani ambako walihudhuria viongozi mbalimbai akiwemo mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Aden Rage.


CCM ilifanya mkutano huo baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kikiongozwa na Naibu Katibu mkuu wake, Zitto Kabwe, kufanya mkutano katika eneo hilo na kuwachongea wabunge wa CCM Tabora kuwa hawatetei wapigakura wao.

Dalili za zomeazomea zilianza mapema kwani baadhi ya wananchi walianza kuibua vicheko na kejeli kwa viongozi wa CCM huku wengine wakisikika wakisema hawataki majigambo, matusi bali barabara za lami

kutoka Tabora-Nzega, Tabora-Urambo na ile ya Itigi-Tabora na wengine wakisema 'Peoples Power'.


Wakati Katibu wa CCM Mkoa wa Tabora, Idd Ame, akizungumza kwenye mkutano huo, wananchi wachache waliokusanyika walianza kuzomea kila kiongozi huyo alipokuwa akijaribu kuikejeli CHADEMA.


“Ndugu zangu wananchi hebu angalieni mnavyodanganywa, hivi hawa CHADEMA wanajigamba kujenga barabara wakati wao siyo watoaji wa fedha…fedha zinatolewa na serikali ya CCM, hao CHADEMA ni wanafiki na waongo,” alisema Ame.


Alisema inashangaza kuona mtu anaacha jimbo lake Kigoma kwenda Tabora kuwafundisha siasa na kudai kuwa huo upumbavu.


Baada ya kauli hiyo, wananchi walipoanza kuzomea kwa nguvu na kudai wanataka sera na si matusi.


“Hapa tuko kamili endeleeni kuzomea tu…tutaumizana kwelikweli hapa msifikiri hatuwezi na tutawashitaki viongozi wa CHADEMA Tabora kwa kutufanyia fujo kwenye mkutano wetu,” alisikika akisema Katibu huyo wa CCM.


Wakati katibu huyo akitamka hayo, Mjumbe wa NEC John Mchele alikwenda jukwaani na kumnong`oneza katibu huyo, ndipo ilizuka fujo kubwa huku Green Guard wa CCM wakitembeza mkong`oto kwa baadhi ya wananchi waliokuwa wakionesha ishara ya vema.


Tafrani hiyo ilidumu kwa dakika 20 na ndipo askari polisi walipoongezwa na mkutano kuendelea.


Baada ya vurugu kutulia huku wananchi wengine wakiondoka, mbunge Tabora mjini, Rage alipanda jukwaani na kutoa sh milioni 68 kwa kata 10 za manispaa hiyo na kila kata ilikabidhiwa hundi yake kwa ajili ya miradi ikiwemo ujenzi wa vyoo, umaliziaji nyumba za walimu na madarasa.


Aidha mbunge huyo alikabidhi chama cha waendesha bodaboda pikipiki mbili na kutoa ahadi ya kuendelea kusaidia.


Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa CCM Tabora mjini Moshi, Abdurahaman Nkonkota alilaani Jeshi la Polisi kutolinda mikutano ya CCM hadi wanafanyiwa vurugu.


 
Ishara ya resistance kutoka kwa watawaliwa waliochoka na uongozi dhalimu wa serikali katili inayoongozwa na ccm chama cha mafisadi.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom