Waziri Mkuu Majaliwa: Viroba marufuku kuzalishwa wala kutumiwa kuanzia Machi 01, 2017

dah apa inabidi nitafute kinywaji kingine kwenda juu cwez inabid nishuke chini na utakua bila shaka ni mwendo wa gongo na viduchu vya mia mia
 
Masuala ya pombe sawa. Lakini main issue ni mazingira . Je maji ya plastic na mavitu yote ya plastic zinazochafua mazingira wamefumbia macho? Ewe Makamba ...
 


Amesema wameshakaa na wenye viwanda vya kutengeneza pombe hizo na kuwaambia viroba kuwa kuanzia tarehe 1/3/2017 ni marafuku kutengeneza viroba.

Amewataka watengeneze pombe zenye ukubwa unaokubalika kwani viroba vimekuwa vikitumiwa na wanafunzi.

Amesema zoezi hilo litaenda sambamba na zoezi la kupiga vita dawa za kulevya


kwa kuwa bado kuna stock ambayo pengine kodi yake serikali ishalipwa serekalini, kisha mnazipiga marufuku, si wangepewa muda wa kutosha kumaliza zilizopo sokoni? kwa sababu sio sumu issue ni packing material!
 
Wengine pombe kwetu ni mila na ibada utazuiaje

Anachofanya waziri mkuu ni sawa na kuzuia maji ya mfuko na kuruhusu ya chupa yaendelee kuwepo akiamini kwamba maji yote yanayouziwa kwenye chupa yana utofauti na ya kwenye mfuko.
 
Sijui itakuwaje sasa MALOKI hamna tena!
Kaka kwa kweli bado sijajuwa hasa maana yao, ni kupiga marufuku vile viplastiki sababu ya mazingira, au sababu vijana wanaharibika?! Na kama vijana walio chin ya 18yrs wanatumia loki wakushtakiwa na wauzaji na sio kutuumiza sie mkuu, mbona majuu tumeona kuna vinywaji vikali vya ujazo mdogo kama viroba kaka?!
 

Attachments

  • images.jpg
    images.jpg
    9.4 KB · Views: 33
  • 3.jpg
    3.jpg
    6.8 KB · Views: 32
  • 22.jpg
    22.jpg
    6.6 KB · Views: 31
Juhudi yoyote inayosaidia hata mtanzania mmoja au mwanafunzi asiyejitambua na kuokoa uchafuzi wa mazingira inapaswa kupongezwa na kuungwa mkono. Ila Viwanda muda wa kutosha ili wabuni kinywaji mbadala ambacho hakina athari lalamikiwa sio flexible kama kiloba

Namna gani mifuko ya plastic maarufu kama RAMBO ambayo ni mikubwa na inatumika kama vifungashio kila sehemu, madukani, sokoni, mikaa, buchani hadi hotelini!.? Au nayo ni sehemu ya viroba?
 
Namna gani mifuko ya plastic maarufu kama RAMBO ambayo ni mikubwa na inatumika kama vifungashio kila sehemu, madukani, sokoni, mikaa, buchani hadi hotelini!.? Au nayo ni sehemu ya viroba?
Mkuu hiki kina double disadvantages ukiacha uchafuzi wa mazingira maana mifuko yake inamills kubwa kikubwa zaidi vinachochea unywaji wa kilevi kwa kificho watu wa makundi mbalimbali wakiwemo watoto na wanafunzi. Kuhusu mifuko ya plastic serikali iliyopita ilishatoa maelezo ni mifuko na vifungashio vyenye sifa zipi na Mills ngapi vyafaa kutengenezwa ambavyo ni environmental friendly otherwise viwe reusable.
 
Mkuu hiki kina double disadvantages ukiacha uchafuzi wa mazingira maana mifuko yake inamills kubwa kikubwa zaidi vinachochea unywaji wa kilevi kwa kificho watu wa makundi mbalimbali wakiwemo watoto na wanafunzi. Kuhusu mifuko ya plastic serikali iliyopita ilishatoa maelezo ni mifuko na vifungashio vyenye sifa zipi na Mills ngapi vyafaa kutengenezwa ambavyo ni environmental friendly otherwise viwe reusable.

Itakuwaje kama mawakala wa ulevi wataondoa viroba, badala yake watengeneze vichupa vidogo vidogo vya plastic au vya vioo lakini vikawa na uwezo wa kufichika na kubebeka kirahisi?
 
Itakuwaje kama mawakala wa ulevi wataondoa viroba, badala yake watengeneze vichupa vidogo vidogo vya plastic au vya vioo lakini vikawa na uwezo wa kufichika na kubebeka kirahisi?
Sidhani kama inaweza kuwa hivyo maana uwepo wa Makampuni pamoja na kupata faida wanaangalia wellbeing ya society. Ila kwa maoni ya kina zaidi huwezi kuzuia ulevi kwa watoto au muda wa kazi kwa kubadil design ya vifungashio japo inapunguza kwa asilimia kadhaa. Nguvu kubwa zingewekezwa kwenye maadili ya familia maana mabadiliko ya technology yatatusogeza karibu na vitu vingi visivyofaa tena kwa spidi ambavyo wenda vingine visizuilike. Nimewahi kupanda bodaboda Bila kujua jamaa alikuwa na viroba mfukoni vingi tu na alikuwa amelewa. Itasaidia lkn kama ulevi ni addictive inabidi kama nchi tufikiri zaidi suluhisho la kudumu.
 
Back
Top Bottom