Waziri Mkuu Majaliwa, umeiweka wapi funguo ya demokrasia nchini? Tunaiomba

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,137
17,908
Ni jambo la wazi kabisa kuwa nchi imepoa. Wananchi hawana furaha. Furaha ya kidemokrasia. Furaha ya kuwasikia na kuwaona wanasiasa majukwaani wakisema na kutenda. Kisiasa na kisasa. Lakini, kwasasa nchi iko kimya na pweke kidemokrasia.

Tangu Waziri Mkuu Majaliwa alipotoa kauli ya kupiga marufuku mikutano ya kisiasa (ile ya kushukuru wananchi), demokrasia imefungiwa kwenye chumba chenye giza nene. Demokrasia inahitaji kutolewa ilikowekwa. Ili iweze kujionesha na kujidhihirisha. Mambo kama ya ubomoaji yangesikika kwenye majukwaa. Mambo ya Zanzibar pia.

Waziri Mkuu Majaliwa, umeiweka wapi funguo ya demokrasia? Tunaiomba. Wapenda demokrasia tunakuomba. Tunataka kuwasikia hata makada wa CCM yetu wanavyojibu bila aibu hata hoja za wapinzani wetu. Makada wana hoja za haja za kuwasambaratisha wapinzani.

Ukimya huu wa kidemokrasia, hakika, unaua vyama vya kisiasa kikiwemo hata CCM. Demokrasia ni mikutano ya kisiasa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Ni jambo la wazi kabisa kuwa nchi imepoa. Wananchi hawana furaha. Furaha ya kidemokrasia. Furaha ya kuwasikia na kuwaona wanasiasa majukwaani wakisema na kutenda. Kisiasa na kisasa. Lakini, kwasasa nchi iko kimya na pweke kidemokrasia.

Tangu Waziri Mkuu Majaliwa alipotoa kauli ya kupiga marufuku mikutano ya kisiasa (ile ya kushukuru wananchi), demokrasia imefungiwa kwenye chumba chenye giza nene. Demokrasia inahitaji kutolewa ilikowekwa. Ili iweze kujionesha na kujidhhirisha. Mambo kama ya ubomoaji yangesikika kwenye majukwaa. Mambo ya Zanzibar pia.

Waziri Mkuu Majaliwa, umeiweka wapi funguo ya demokrasia? Tunaiomba. Wapenda demokrasia tunakuomba. Tunataka kuwasikia hata makada wa CCM yetu wanavyojibu bila aibu hata hoja za wapinzani wetu. Makada wana hoja za haja za kuwasambaratisha wapinzani.

Ukimya huu wa kidemokrasia, hakika, unaua vyama vya kisiasa kikiwemo hata CCM. Demokrasia ni mikutano ya kisiasa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Mzee wangu mbona Chama Chenu Kimeruhusiwa kufanya Mikutano?Maana mmeshinda kiti cha urais,ila wale walioshindwa ndiyo wamenyimwa hawaruhusiwi hata kwenda kusema asanteni kwa kunisikiliza eti wataleta vurugu.

Chama Chenu kimeruhusiwa maana wabunge ,madiwani,Katibu Mkuu na Mwenyekiti wenu wanaruhusiwa,wanasubiri Waziri Mkuu au waziri akienda kuwatembelea watanzania huko majimboni na wao wanaenda kufanya kampeni za 2020 na kuendelea kuwananga wapinzani!!!!!!!!!!!

Kwani si hata yule anayeshughulikia na issue za vyama kanyamaza maana anajua linawahusu wapinzani tu!!!!!!!!!!!!Hujaona hata walivyowabagua MACHOTARA na USOMALI hata serikali imekaa kimya maana ndiyo SERA mama ya Chama Chenu Cha Majambazi.

Kwa sasa tunaomba mshughulikie ile UDA yetu
 
Mzee wangu mbona Chama Chenu Kimeruhusiwa kufanya Mikutano?Maana mmeshinda kiti cha urais,ila wale walioshindwa ndiyo wamenyimwa hawaruhusiwi hata kwenda kusema asanteni kwa kunisikiliza eti wataleta vurugu.

Chama Chenu kimeruhusiwa maana wabunge ,madiwani,Katibu Mkuu na Mwenyekiti wenu wanaruhusiwa,wanasubiri Waziri Mkuu au waziri akienda kuwatembelea watanzania huko majimboni na wao wanaenda kufanya kampeni za 2020 na kuendelea kuwananga wapinzani!!!!!!!!!!!

Kwani si hata yule anayeshughulikia na issue za vyama kanyamaza maana anajua linawahusu wapinzani tu!!!!!!!!!!!!Hujaona hata walivyowabagua MACHOTARA na USOMALI hata serikali imekaa kimya maana ndiyo SERA mama ya Chama Chenu Cha Majambazi.

Kwa sasa tunaomba mshughulikie ile UDA yetu

Nimekupata binti yangu Tetty

Mzee Tupatupa
 
Ila kwa sasa naomba umuelimishe tu Nape kwamba aanze na Mwenyekiti wake,maana haingii akilini ya UDA na mengineyo.Naona kama usiku wa kiza umeingia kwenye TAIFA..............

Pia waelimishe vijana wako kwamba UPINZANI si UADUI but catalyst ya MAENDELEO.
NENO
 
Ni jambo la wazi kabisa kuwa nchi imepoa. Wananchi hawana furaha. Furaha ya kidemokrasia. Furaha ya kuwasikia na kuwaona wanasiasa majukwaani wakisema na kutenda. Kisiasa na kisasa. Lakini, kwasasa nchi iko kimya na pweke kidemokrasia.

Tangu Waziri Mkuu Majaliwa alipotoa kauli ya kupiga marufuku mikutano ya kisiasa (ile ya kushukuru wananchi), demokrasia imefungiwa kwenye chumba chenye giza nene. Demokrasia inahitaji kutolewa ilikowekwa. Ili iweze kujionesha na kujidhihirisha. Mambo kama ya ubomoaji yangesikika kwenye majukwaa. Mambo ya Zanzibar pia.

Waziri Mkuu Majaliwa, umeiweka wapi funguo ya demokrasia? Tunaiomba. Wapenda demokrasia tunakuomba. Tunataka kuwasikia hata makada wa CCM yetu wanavyojibu bila aibu hata hoja za wapinzani wetu. Makada wana hoja za haja za kuwasambaratisha wapinzani.

Ukimya huu wa kidemokrasia, hakika, unaua vyama vya kisiasa kikiwemo hata CCM. Demokrasia ni mikutano ya kisiasa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
We siku hizi huna maana kabisa, ulikuwa unaheshimika zamani.
 
Ila kwa sasa naomba umuelimishe tu Nape kwamba aanze na Mwenyekiti wake,maana haingii akilini ya UDA na mengineyo.Naona kama usiku wa kiza umeingia kwenye TAIFA..............

Pia waelimishe vijana wako kwamba UPINZANI si UADUI but catalyst ya MAENDELEO.
Maneno mazuri sana haya...Amani iwe kwako mkuu
 
Huu ni muda wa kufanya kazi na sio kutafuta funguo ya demokrasia, muda wa kuzalisha, sio kupiga domo majukwaani, halafu hotuba ikimalizika masikini kwa wingi wao wanaendelea kupiga mihayo na matajiri wanapanda magari mapya yenye viyoyozi. Huu ni muda wa kubuni miradi mbalimbali yenye tija kwa jamii, miezi ya siasa ilimalizika baada ya rais wa awamu ya tano kuapishwa. Tuwaonee huruma walio wengi ambao wanatumika kama mitaji ya watu kwenye siasa zisizo na ukomo.
 
Back
Top Bottom