Uchaguzi 2020 Kauli ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kusema Wagombea wa Upinzani wasiwachafue wagombea wa chama tawala una lengo la kutaka kuwatisha

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Habari kubwa kwenye magazeti ya Leo ni kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kuwapiga mkwara mzito, wagombea wa vyama vya upinzani kuwa wasitumie majukwaa ya kisiasa katika kipindi hiki cha kampeni kuwachafua wagombea wenzao.

Ingawa hakuwataja kwa majina wagombea hao, ni dhahiri alikuwa na maana ya wagombea wa Chadema na ACT Wazalendo, ambao kwao CCM ndiyo wanawaona kuwa ni tishio kubwa sana kwao.

Ni jambo la kushangaza kauli hiyo kutolewa na kiongozi wa ngazi ya juu wa CCM, kwa kuwa katika kipindi chote cha miaka 5 iliyopita, chama cha CCM "kilijipendelea" kwa kufanya kampeni peke yao, nchi nzima, wakiwachafua na kiwatukana viongozi wenzao wa upinzani, huku wakivipiga marufuku vyama vya upinzani, kutofanya mikutano yoyote ya kisiasa ya kujibu mashambulizi hayo

Sasa inashangaza mno kwa viongozi hao wa upinzani wanapotumia fursa hii waliyoipata wakati huu kufanya kampeni kujieleza, Waziri mkuu anasema wasiwachafue viongozi wa CCM!

Hivi kwa mfano kauli iliyotolewa na kiongozi wa Chadema, ambaye pia ni mgombea wa nafasi ya Urais Tundu Lissu, kuwa Rais Magufuli ametumia nafasi yake ya Urais kujenga kiwanja cha ndege cha kimataifa, huko kijijini kwake Chato na "kulazimisha" kuwa na mbuga yao ya wanyama ya Burigi, kwa Maelezo ya waziri mkuu, ni kumchafua Rais Magufuli?

Ninavyoona Mimi kama raia wa Tanzania, ambaye nina haki ya kutoa maoni yangu, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 18(1) uamuzi wa busara kwa viongozi wa CCM ni kwa Rais Magufuli kujitokeza hadharani na kujibu mapigo hayo ni kwanini yeye ameamua kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa kwenye kijiji chake, kinyume cha viongozi waliomtangulia, akina Mwalimu Nyerere, Alli Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete, hawajafanya kama yeye, aende kwenye majukwaa ya kisiasa ili atoe maelezo kama maneno aliyoyatoa Tundu Lissu ni ya uwongo. OVA
 
Habari kubwa kwenye magazeti ya Leo ni kauli aliyoitoa waziri mkuu Kassim Majaliwa ya kuwapiga mkwara mzito, wagombea wa vyama vya upinzani kuwa wasitumie majukwaa ya kisiasa katika kipindi hiki cha kampeni kuwachafua wagombea wenzao...
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.

Huyo Dr. Magufuli ni Mungu? Anaambiwa ukweli ila tafsiri yenu ni kuwa anatukanwa. Hili ni tatizo la kupenda kusifiwa kupita kiasi, hivyo siku ikitokea ukapewa ukweli wao unaona umetukanwa.
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Ngumbaru la kahe.

Mbona jiwe anatukana watu hadi kutaka kupiga mashangazi?

Tunamdharau sana na ndio maana anatukanwa tu.
 
Habari kubwa kwenye magazeti ya Leo ni kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kuwapiga mkwara mzito, wagombea wa vyama vya upinzani kuwa wasitumie majukwaa ya kisiasa katika kipindi hiki cha kampeni kuwachafua wagombea wenzao...
Boss wake mbona anatukana na kudhalilisha watu hadharani mbona hajawahi kumueleza? Huyo Majaliwa atulie dawa imuingie atulize KIPAGO Mwamba Yupo GADO kuwapa za uso kipyenga kikipulizwa.
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Sio ndio vizuri huyo Lissu ajiharibie ili watu wamuelewe vizuri Magufuli?

Nyie ni sawa na mahayawani kweli! Wakati mnawaita Wapinzani ni MALOFA NA WAPUMBAVU mlikuwa mnajishangilia kweli kweli, lakini mkiambiwa mmejijengea uwanja wa ndege basi mnakashifiwa?

Pumbaf kabsa! Na bado mpaka kufikia octoba mtaongea hadi kisandawe, shubamit!
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Sasa nieleze matusi ni yapi hapo, kwa Tundu Lissu kuwaeleza wananchi, kuwa jipya alilolifanya Rais Magufuli ni kujenga uwanja wa kimataifa wa ndege, ambapo viongozi wenzake waliomtangulia hawakufanya hivyo?
 
Habari kubwa kwenye magazeti ya Leo ni kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kuwapiga mkwara mzito, wagombea wa vyama vya upinzani kuwa wasitumie majukwaa ya kisiasa katika kipindi hiki cha kampeni kuwachafua wagombea wenzao...
Hivi yale maneno ya boss mkubwa, kwamba wapinzani wakichukua madaraka watavunja madaraja na kuyauza kama skrepa... SIYO KUWACHAFUA WAPINZANI..!?? Au uchafu ni upande mmoja!?
 
Ni muhimu tuwajue viongozi wetu watarajiwa. Kuchaguliwa ni kupewa dhamana hivyo kama kuna mwenye uchafu, madharau, mvunja sheria, ubabe etc wananchi wanatakiwa wamjue ili wafanye maamuzi sahihi. Na hii haijalishi ni wa chama gani cha msingi isiwe mambo ya kutunga (uwongo), lakini umbea unaruhusiwa.

Yale tuliofichwa kwa miaka mitano ambayo tunatakiwa kuyafahamu wakati wake umefika.
 
Back
Top Bottom