Waziri Mkuu imulike PSPF kuna uozo

Waziri Mkuu imulike PSPF kuna uozo

Malilambwiga

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2015
Posts
485
Reaction score
296
Nimestaafu tangu mwezi June 2015 na hadi sasa bado sijalipwa mafao yangu.

Mwezi Novemba nilipokwenda makao makuu ya PSPF nikaambiwa mafao yangu yako tayari na jalada langu lilikuwa ofisi ya malipo kuandikiwa hundi lakini serikali ilikuwa haijawasilisha fedha inazodaiwa na mfuko huo.

Nilivuta subira hadi niliposikia tamko la Naibu Waziri wa fedha akiwapa siku saba PSPF kuwalipa wastaafu.

Juzi siku ya Ijumaa tarehe 15.01.2016 nikaenda tena PSPF makao Makuu ofisi ya malipo majira ya saa 4 asubuhi.

Nilijibiwa na mtumishi wa ofisi hiyo kijana wa kiume aliyekuwa zamu kuwa hundi yangu iko tayari isipokuwa hawawezi kunikabidhi hadi aje mwakilishi anayetambuliwa kutoka idara ya Polisi makao makuu ndiye atasaini kuchukua hundi hiyo.

Nilichapa mguu hadi makao makuu ya Polisi kitengo cha wastaafu na kumkuta Sgt David ambaye baada ya kumweleza mara moja akamtuma askari kufuatilia hundi hiyo.

Hata hivyo kabla ya kuchukua jukumu la kwenda makao makuu ya polisi niliomba kuonana na Meneja wa huduma kwa wateja lakini pia nilijibiwa yuko likizo na hakuna mbadala wake.

Kutokana na imani niliyokuwa nayo niliondoka kurejea nyumbani nikiamini mambo yako sawa.

Majira ya saa tisa alasiri nilimpigia simu Sgt David na kwa masikitiko makubwa akanieleza mafao yangu bado na lugha aliyotumia mtumishi wa PSPF ilikuwa ni njia ya kuniondoa tu.

Hayo ndiyo majanga ya mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umma.
Nina imani mamlaka husika zitafuatilia utendaji wa taasisi hii ya umma kwani ule msoto wa wastaafu uliokuwepo miaka ya nyuma hadi watu kupiteza maisha bila kulipwa unerudi kwa kishindo.
 
Pole sana mkuu mambo ya Tanzania yahitaji uvumilivu sana.....!!!
 
Nimestaafu tangu mwezi June 2015 na hadi sasa bado sijalipwa mafao yangu.

Mwezi Novemba nilipokwenda makao makuu ya PSPF nikaambiwa mafao yangu yako tayari na jalada langu lilikuwa ofisi ya malipo kuandikiwa hundi lakini serikali ilikuwa haijawasilisha fedha inazodaiwa na mfuko huo.

Nilivuta subira hadi niliposikia tamko la Naibu Waziri wa fedha akiwapa siku saba PSPF kuwalipa wastaafu.

Juzi siku ya Ijumaa tarehe 15.01.2016 nikaenda tena PSPF makao Makuu ofisi ya malipo majira ya saa 4 asubuhi.

Nilijibiwa na mtumishi wa ofisi hiyo kijana wa kiume aliyekuwa zamu kuwa hundi yangu iko tayari isipokuwa hawawezi kunikabidhi hadi aje mwakilishi anayetambuliwa kutoka idara ya Polisi makao makuu ndiye atasaini kuchukua hundi hiyo.

Nilichapa mguu hadi makao makuu ya Polisi kitengo cha wastaafu na kumkuta Sgt David ambaye baada ya kumweleza mara moja akamtuma askari kufuatilia hundi hiyo.

Hata hivyo kabla ya kuchukua jukumu la kwenda makao makuu ya polisi niliomba kuonana na Meneja wa huduma kwa wateja lakini pia nilijibiwa yuko likizo na hakuna mbadala wake.

Kutokana na imani niliyokuwa nayo niliondoka kurejea nyumbani nikiamini mambo yako sawa.

Majira ya saa tisa alasiri nilimpigia simu Sgt David na kwa masikitiko makubwa akanieleza mafao yangu bado na lugha aliyotumia mtumishi wa PSPF ilikuwa ni njia ya kuniondoa tu.

Hayo ndiyo majanga ya mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umma.
Nina imani mamlaka husika zitafuatilia utendaji wa taasisi hii ya umma kwani ule msoto wa wastaafu uliokuwepo miaka ya nyuma hadi watu kupiteza maisha bila ku
lipwa unerudi kwa kishindo.

May be wanasubiri ufe ndo waandae malipo yako.

Just joking!!
 
Haki yako haiwezi kupotea mbele ya JPM. Huu uzi wahusika wakiuona next week unajaa pesa la sivyo jipu litatumbuliwa.
 
Kilichoniuma siyo kusubili bali ni kitendo cha mtumishi anayelipwa mshahara kuniongopea kwa makusudi. Hilo jambo limeniuma sana
 
We mtoa mada ni mpole saaana mm hao jamaa nitakuja piga mmoja wao ngumi ya jicho kwaaap!! Mother wangu wanamsumbua saaanaa siku nkifika ofisini kwao nitakuja andika thread hapa Jf.
 
Kilichoniuma siyo kusubili bali ni kitendo cha mtumishi anayelipwa mshahara kuniongopea kwa makusudi. Hilo jambo limeniuma sana
Piga ngumi haoo jamaa wasumbufu saaana pesa zetu na wao wako hapo kwa ajili yetu piga haoo kwaaaap!
 
Hawa jamaa ni jipu sijui kwa nini hawakamuliwi, malalamiko ni mengi kuliko mafanikio
 
ungeweka jina la huyo aliyekujibu hapa jamvini waziri husika angeanza kumtumbua huyo kijana kesho asubuhi hawa vijana wa siku hivi wakishaendesha Altezza, wakijua kwenda century cinemax, wakijua kwenda kuangalia mpira samaki samaki , wakiwa na demu wa ifm, wakiwa na samsung galaxy, wakiwa na kiwanja mbweni basi wanaona wamemaliza na kama yuko kitengo cha customer care utachoka
 
Back
Top Bottom