tramadol
JF-Expert Member
- Oct 10, 2015
- 5,383
- 4,317
Ni marufuku kusafirisha kuuza mahindi nje ya nchi na ukitaka kusafirisha saga hayo mahindi kwanza then omba kibali Serikali.
Serikali inajaribu kukabiliana na njaa kwa watanzania kutokana na uhaba wa mahindi nchini
Na ameongeza ni vizuri kuongea value kwa maana ya kusaga mahindi ambayo itakuwa ni nafuu zaidi kwani itasaidia ajira kwa vijana nchini Kulikoni kuuza mahindi yenyewe
Hayo yamesemwa na Wazuri mkuu Kassim Majaliwa huko Moshi ktk Sikukuu ya Eid leo.
======
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amepiga marufuku usafirishaji wa chakula nje ya nchi bila kibali na kuwataka wafanyabiashara kuuza chakula kwenye maeneo yenye uhaba nchini.
Majaliwa ametoa agizo hilo leo, Jumatatu wakati akihutubia Baraza la Eid katika Msikiti wa Masjid Riadha mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.
Waziri Mkuu huyo amesema kuwa kuna maeneo ambayo wananchi hawakupata chakula vizuri kutokana na uhaba wa mvua hivyo wafanyabiashara wapeleke chakula kwenye maeneo hayo.
“Serikali bado haijatoa kibali cha kutoa chakula nje ya nchi, kama unaona kuna umuhimu kaombe kibali, lakini utapewa kibali cha kusaga upeleke unga na siyo mahindi,”amesisitiza Majaliwa.
Majaliwa ameonya kuwa kwa wale watakao kamatwa wakisafirisha mahindi nje ya nchi kinyume na utaratibu, mahindi hayo yatataifishwa na kupelekwa kwenye ghala la Taifa na magari yatapelekwa polisi.
Amesema kuwa Serikali imepokea barua za maombi ya kupeleka chakula nchi jirani, lakini bado haijatoa ruhusa.
Serikali inajaribu kukabiliana na njaa kwa watanzania kutokana na uhaba wa mahindi nchini
Na ameongeza ni vizuri kuongea value kwa maana ya kusaga mahindi ambayo itakuwa ni nafuu zaidi kwani itasaidia ajira kwa vijana nchini Kulikoni kuuza mahindi yenyewe
Hayo yamesemwa na Wazuri mkuu Kassim Majaliwa huko Moshi ktk Sikukuu ya Eid leo.
======
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amepiga marufuku usafirishaji wa chakula nje ya nchi bila kibali na kuwataka wafanyabiashara kuuza chakula kwenye maeneo yenye uhaba nchini.
Majaliwa ametoa agizo hilo leo, Jumatatu wakati akihutubia Baraza la Eid katika Msikiti wa Masjid Riadha mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.
Waziri Mkuu huyo amesema kuwa kuna maeneo ambayo wananchi hawakupata chakula vizuri kutokana na uhaba wa mvua hivyo wafanyabiashara wapeleke chakula kwenye maeneo hayo.
“Serikali bado haijatoa kibali cha kutoa chakula nje ya nchi, kama unaona kuna umuhimu kaombe kibali, lakini utapewa kibali cha kusaga upeleke unga na siyo mahindi,”amesisitiza Majaliwa.
Majaliwa ameonya kuwa kwa wale watakao kamatwa wakisafirisha mahindi nje ya nchi kinyume na utaratibu, mahindi hayo yatataifishwa na kupelekwa kwenye ghala la Taifa na magari yatapelekwa polisi.
Amesema kuwa Serikali imepokea barua za maombi ya kupeleka chakula nchi jirani, lakini bado haijatoa ruhusa.