Waziri Mkuu amelidanganya bunge na watanzania wote

Sijui ni mimi tu, naona kama attachment hazijakaa sawia! Aliyeziona vizuri naomba azipost tena jamani.


Haya hii hapa.
UKWELI WA KILICHOTOKEA TAREEHE 17-12-2010 KWENYE UKUMBI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ARUSHA
Hakika, damu za waliopoteza maisha katika kutafuta haki Arusha tarehe 5-01-2011 zitawalilia Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa - - Aruasha, na wasimamizi wa kikao cha tarehe 17/12/2010 kutoka TAMISEMI – Dar es Salaam.
􀂾 Baada tu ya Madiwani wa Chadema kupokea taarifa ya Mkutano maalum wa baraza la madiwa la halmashauri ya manispaa wa tarehe 17/12/2010, pamoja na agenda na ratiba, walibaini kuwa agenda haikuwa na kiapo cha madiwani, bali ratiba ilikuwa na agenda hiyo kama shughuli ya 3 ya siku hiyo.
􀂾 Kanuni za kudumu za mikutano na shughuli za halmashauri, Sura ya 6(VI), Kanuni Na 67, inaainisha wazi kuwa “ kila diwani, kabla ya kushika wadhifa wake kama diwani na kabla ya Mkutano wa kwanza wa halmashauri, atakula kiapo.
􀂾 Ratiba pia ilionyesha kuwa Shughuli na.6 ya siku hiyo, “Uchaguzi wa Meya wa halmashauri ilipangwa kusimamiwa na Mkurugenzi wa manispaa, wakati kanuni na. 10 (1) (b), inatamka wazi kuwa, “Kama mwenyekiti na makamu mwenyekiti hawapo, mmoja kati ya wajumbe wa mkutano atateuliwa kuendesha mkutano”
􀂾 Mkurugenzi anatakiwa kuwa KATIBU wa vikao VYOTE vya baraza kikiwapo kikao cha kwanza, (Kifungu Na. 24(8) cha sheria za serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji Na.8 ya mwaka 1982, pamoja na marekebisho).

TAREHE 17/12/2010:
􀂾 Madiwani wa Chadema walifika Manispaa saa 3.45 asubuhi na kwa mshangao kukuta askari wengi wakiwa wametanda eneo lote la halmashauri, bila kujua mipango ya mkurugenzi. Waliingia ukumbini na kukuta wenzao wa CCM wameshabana upande mmoja wa ukumbi na kuacha wazi upande mmoja, kaubaguzi ka kiaina fulani.
􀂾 Tarehe 16/12/2010, mkurugenzi alikodi gari la matangazo kupita katika mitaa yote ya manispaa ya Arusha, kuwatangazia wananchi kuja kushuhudia madiwani wakiapa na kumchagua Meya wao tarehe 17/12/2010. Kinyume chake wananchi waliofika, zikiwamo familia za madiwani hawakuruhusiwa kabisa kukaribia eneo la manispaa na hata vyombo vya habari havikuruhusiwa kama kanuni Na. 12 inavyoagiza. Wananchi waliojaribu kukaribia eneo hilo, walipigwa na hata wengine kupelekwa mahabusu na wameshitakiwa mahakamani hadi leo.
􀂾 Mkurugenzi aliingia saa 4.10 asubuhi, akifuatana na viongozi wa TAMISEMI.
􀂾 Aliwasalimia wajumbe na kuwasisitizia kuwa yeye ndiye mwenyekiti wa kikao cha siku hiyo, na wakati huo huo akisisitizia wajumbe kusaini kwenye kitabu cha mahudhurio ili akidi ya mkutano iweze kutimia na mkutano uanze.
NB: Mkurugenzi aliamini kuwa madiwani wa CHADEMA ni wageni na hawajui lolote kuhusu Kanuni za Kudumu za Mikutano na Shughuli za Halmashauri, lakini kwa mshangao vijana wa Chadema walianza kumtajia na kunukuu kanuni hizo kutoka vichwani kuhusu kuapa kwanza kabla ya kutafuta akidi ya mkutano wa kwanza.
Wakaenda mbele zaidi na kumtahadharisha kuhusu ukomo wa uenyekiti wake kuishia kwenye kuapisha madiwani na kumwachia mjumbe mteule kati ya wajumbe waliopo kusimamia uchaguzi wa Meya na kisha Meya atakaye chaguliwa kusimamia uchaguzi wa naibu Meya. “Hatua hii ilimshangaza na kuanza kutoka jasho hadi kichwani bila kuelewa lakufanya tena.
Wakati akitafakari aina ya watu walioingia kwenye baraza kipindi hiki, alisimama mjumbe mmoja na kumtahadharisha kuhusu mjumbe HARAMU wa mkutano huo “ Mary Chatanda kutoka Tanga.”
Hapo ndipo hali ya hewa ilipoanza kuchafuka ndani ya ukumbi ule kwa siku hiyo.
Mabishano na kelele zilianza na kuendelea kwa takriban saa nzima hadi kikao kikaahirishwa kwa saa 1, ili watu wakapekue sheria na nyaraka mbalimbali za uthibitisho, na wapate chai katika kipindi hicho.
Vijana wa Chadema waliporudi, walikuwa na nyaraka za kimtandao kuwa Mary Chatanda alichaguliwa na wajumbe kule Tanga, akiwa wa pili kwa kura 490, wa kwanza alikuwa na kura 514 na wa tatu alipata kura 460. Vijana hawa walilithibitishia baraza kuwa, waliomchagua kule Tanga wanamuhitaji akawatumikie, na sio wananchi wa jiji la Arusha.
Meza ilichanganyikiwa baada ya kupata taarifa hizo,na siku iliharibika kabisa.
Walianza kutafuta vielelezo na ushahidi bandia wakumhalalisha mjumbe huyo, bila mafanikio, hadi mkurugenzi alipoamua kuwa basi kama ndivyo. Madiwani waapishwe ili siku isipotee bure.

KIAPO BANDIA:
Baada ya hakimu kufika, Mkurugenzi kwa kofia ya mwenyekiti, alitamka kuwa, kutokana na wingi wa wajumbe wanaotakiwa kuapa, haitawezekana kuapa mmoja mmoja na hivyo kulazimika kuapa kwa pamoja wote. Wajumbe walihoji, kulikoni,wengi wangapi? 30 tu! Licha ya wajumbe kulalamika, Mkurugenzi alisisitiza kuapa kwa pamoja.
Ndipo madiwani wote waliposimama kwa pamoja na kusoma hati za kiapo kwa sauti kama watoto wa shule za awali na kutakiwa kutia saini pale mwisho. Wakati huo, Kitabu cha mahudhurio ya mikutano ya baraza bado hakina sahihi hata moja ya madiwani wa CHADEMA, na hadi leo hakuna sahihi zao.
Je, hati za kiapo za madiwani, ambao wanatakiwa kuapa kabla ya kikao cha kwanza kuitishwa ndizo zinazolazimishwa kutumika kama akidi ya kikao hicho cha kwanza cha tarehe 17/12/2010?!

KULAZIMISHA UCHAGUZI WA MEYA:
Baada ya Mkurugenzi kuona kuwa madiwani wote wameapa na hati husika kusainiwa na kurudishwa kwake, ndipo alipoanza kulazimisha kuendelea na uchaguzi wa meya, hata kufikia kusema wasiotaka kuendelea na uchaguzu watoke nje.
Akaanza kugawa karatasi za uchaguzi. Vijana wa Chadema walimtahadharisha tena kuhusu akidi za mikitano ya uchaguzi, Kanuni Na. 8(2), na kura ya siri, Kanuni Na.9(1), kwamba akidi haikutimia na mazingira ya kura ya siri hayakuwepo.
Licha ya tahadhari hizo, aling’ang’ania kuendelea na ndipo vijana wote wa Chadema waliposima na kujaa katikati ya ukumbi kupinga hatua hiyo Polisi, wakiongozwa na OCD waliingia ndani ya ukumbi wakitaka kuingilia kati kabla yakutahadharishwa na mjumbe mmoja na kutakiwa watoke nje.
KUAHIRISHA KIKAO
Baada ya hali ya sintofahamu kuendelea kwa muda, mjumbe mmoja alimkumbusha Mkurugenzi kurejea kwenye Kanuni Na. 17(2), ili kuahirisha kikao hicho na akafanya hivyo.
RATIBA YA TAREHE 18/12/2010:
Kutokana na Kikao cha tarehe 17/12/2010 kuisha katika hali ya kutoelewana, madiwani wa chadema walijua kikao hicho kingeendelea siku nyingine na kwa taarifa mpya.
Ratiba ya awali ilionyesha kuwa Jumamosi tarehe 18/12/2010 na Jumatatu tarehe 20/12/2010, madiwani walikuwa wawe kwenye semina elekezi kule Olasiti Garden, na ndiko walikoelekea siku iliyofuata.
Kumbe wenzao wa CCM, baada ya kikao cha tar.17/12/2010 kuahirishwa, walikutana na kusubiri taarifa mpya za kikao cha Jumamosi tarehe 18/12/2010, wakati barua 14 za taarifa za kikao hicho za vijana wa CHADEMA, zilipelekwa na kuachwa kwenye baa moja huko suye na kuachiwa mhudumu kwa maelekezo kuwa akitokea yeyote kati yao akabidhiwe. Barua hizo zilipatikana Jumatatu tarehe 20/12/2010 saa 8 mchana.
Chakushangaza, tarehe 18/12/2010, wakati madiwani wa Chadema wakiwa kule Olasiti Garden, wenzao wa CCM, kwa taarifa walizosambaziana usiku wa tarehe 17/12/2010, waliingia manispaa na kuanza na agenda ya kwanza kwa haraka haraka ya uchaguzi wa Meya, kana kwamba kulikuwa na dharura. Hadi madiwani wa Chadema wanapata taarifa kuwa, wenzao wako Manispaa, Meya na Naibu Meya walishachaguliwa.
Walipokimbia kutoka Olasiti Garden hadi Manispaa wakakuta mambo yamefanyika ndivyo sivyo, ndipo walipoanza kuhoji taratibu zilizotumika na hapo vurugu zikaanza hadi Mbunge wetu kupigwa na kuwekwa mahabusu.
Siku hiyo polisi walikuwa wengi kuliko jana yake, na walitawanyika eneo lote la mita 200 kutoka lango kuu la halmashauri, na walikuwa katika mazingira ya UTAYARI kwa mapambano yoyote. Mazingira kwa vyovyote vile, yaliashiria kufanyika uhalifu fulani kwa nguvu.

TUNASISITIZA KUWA:
􀂙 Muda wa taarifa ya mkutano wa tarehe 18/12/2010 haukufuata kanuni (Na. 7).
􀂙 Baada ya kuahirishwa kwa mkutano wa tareh 17/12/2010, mkutano wa tareh 18/12/2010 ulikuwa unajitegemea na ulihitaji maandalizi mapya kama zilivyofanyika kwenye halmashauri nyingine nchini.
􀂙 Akidi kwenye mkutano wa tarehe 18/12/2010 haikutimia na hivyo kuufanya mkutano huo kuwa batili.
􀂙 Mary Chatanda alikuwa mjumbe batili wa mkutano huo wa uchaguzi na anaendelea kuwa batili.
VIAMBATANISHO:
Pamoja na barua hii, tunaambatanisha:
• Nakala za barua, agenda na ratiba za shughuli za tarehe 17/12/2010 hadi 20/12/2010,
• Nakala ya taarifa ya mkutano wa tarehe 18/12/2010 zilizokuwa zimeachwa baa huko Suye na kupatikana tarehe 20/12/2010
 
Edited: Leo bungeni, Swali la Mbowe lilikuwa la kidiplomosia sana,juzi walikataa kuileta Dowans bungeni, kesi ambayo ICC imetoa hukumu tayari na tunasubiri tuzo eti iko mahakamani,Mh. Mbowe akamjaribu Pinda kwa kesi ambayo haijatolewa hata hukumu,badala ya kurudia kuwa kesi iko mahakamani,PM kaanza kushuka hukumu! Rais alisema akili za kuambiwa...Nazidi kumueleza mbunge Lema mwanzo kabisa aeleze kuwa hajasema pinda muongo,ila ameomba mwongozo afanyeje kama akidhibitisha kuwa pinda muongo? Hapa anapaswa apewe jibu kwa swali lake kuwa,akidhibitisha kuwa Pinda muöngo,hatua A,B,C zitachukuliwa dhidi ya pinda! Hapa ndo sasa aombwe kudhibitisha na akishindwa ndo awajibike mwenyewe! Hapa asikubali kupelekeshwa,apewe jibu kwanza kwa ombi alilotoa la hatua za kumchukulia pinda. UPANDE WA USHAIDI WAKE: Lema ktk kuleta ushaidi wake naomba auleze umma kupitia Bunge kuwa Pinda amelidanganya bunge kuanzia kikao cha kwanza cha bunge baada ya kuteuliwa kuchukua uPM kwa kuapa bila kunyanyua kitabu cha dini wakati ktk document zake nyingi anaonesha yeye ni mkatoliki na ana ndoa ya kikatoliki. Hapa aliudanganya umma,rejea video ya kuapa kuwa waziri mkuu. Pili,katiba inasema Waziri mkuu akijiuzulu,atateuliwa mwingine miongoni mwa wabunge ndani ya muda unaompa rais mamlaka iyo na mteule atashika madaraka kuanzia atakapothibitishwa na bunge mpaka kipindi cha miaka 5 kitimie,Mh.Lowasa alijiuzulu mwaka 2008,Pinda aliapa na kuanza kipindi cha miaka5. Hii inaisha mwaka 2013. Je mbona ktk kikao cha kilichfpita cha bunge la 10,ameliambia bunge ktk hotuba yake kuwa kateuliwa tena?hapa kuna uongo mwingne. Na kama amechaguliwa tena ni kwa kipindi cha kuanzia baada ya uteuzi wake unaokoma mwaka 2013,ina maana uPM wake unakoma mwaka upi? Tatu,kufuatia kikao cha jana cha bunge la 10,mnamo 10/02/11 pinda kaliaminisha bunge na jamii ya watanzania kuwa cdm walianzisha vurugu wakati Mahakama haijatoa hukumu bado inatafuta ukweli-hapa Pinda anaudanganya umma uamini ushaidi wake kuwa raia ndo wakorofi wakati ukweli utaletwa na mahakama. Nne,Pinda ametaja kuwa vita ya arusha imeletwa na kitendo cha cdm baada ya kuongeza route wakati waandamanaji waliopigwa walikuwa wote waliopita hata route zinazosemekana kuwa serikali ya ccm ilizitambua,upande mwingne IGPmwema ndo chanzo sababu polisi wa arusha walikubali kuwa maandamano sawa,yeye bila kuangalia hati halali alibatilisha maandamano kwenye vyombo vya habari bila kuwataarifu wananchi husika. Tano,Pinda kasema Lema ndo aliyevuruga vikao vya madiwani wakati vikao vingine vilifanyika kwa kubadilisha muda na mahali ili kuikwepa cdm! Sita,vifo vilivyotokea ni zaidi ya vitatu,Lema peleka Takwimu na data sahihi. Mwisho,ili kudhibitisha mwanzilishi wa fujo, Mh.Lema nenda bungeni na cd isiyohaririwa,usimpe Spika atachakachua,nenda na projector na laptop uiweke japo dk.10 ili wabunge wote wapate picha ya kuelewa mwenye fujo nani na kuwa kweli Pinda kaleta usanii. Usinshangae nenda na projector utakuwa hujavunja kanuni Tanzania ya leo inakubali ushaidi wa electronic. Kwa kuhitimisha,usitegemee sana kumbadili mawazo spika,jiandae unaweza kupata adhabu iyo,usisahau baada ya hapo kuja kwa wananchi tuijadili iyo adhabu tegemewa ya kukosa vikao5. Naitimisha: Spika atoe majibu kwanza,ichukuliwe hatua gani akidhibitika amelidanganya bunge? Akishajibiwa ndo atoe ushaidi,tofauti na hapo Lema atahukumiwa adhabu ya kosa ambalo si lake.
 
Nilimsikia PM akisema vurugu za chadema zimesababisha vifo vya watanzania watatu lakini taarifa zilizopo ni wawili na mkenya mmoja huu nao pia ni uongo nadhani Lema anaweza ongeza hii katika utetezi wake
 
Mi sioni ishu hapa kama CHADEMA wana ishu wangeanza na ile taarifa ya IGP iliyochapishwa kwenye magazeti kuhusiana na vurugu za Arusha. Kama hizo nazo ni za uongo basi serikali yote itakuwa imeongopa na hapo sasa ithibitishwe kwamba vyombo vya dola vya serikali vimeongea uongo na iwekwe njia ya kuviadhibu!

Otherwise CDM itaonekana ina agenda binafsi tu na PM... thats what i'm seeing here.
 
Hakuna haja ya kulalamika waliokufa ni collateral damage, mwanzo wa yote ni chadema kushindana na Polisi ukweli utabaki hapo! Kwani chadema wasingeandamana hao watu wangekufa? Kila upande ukubali kuwajibika kwa nafasi yake.

Usiwe mvivu wa kufikiri. Kazi ya polisi ni kulinda usalama, wangeweza kuchagua kulinda usalama badala ya kuonyesha misuli yao ambayo kila mtu anajua wanayo. Wangesindikiza maandamano wakayalinda na mwisho wa siku Chadema wakasema walichokusudia kusema na wakaenda nyumbani. Kesho yake yakaandikwa machache kwenye magazeti and the day after all is history. Sasa kwa sababu hawakuamua kutumia busara, madhara yake ni haya, loss of lives, kupoteza muda hadi bungeni kujadili jambo hilo etc. Yaani doa ni kubwa kuliko raha ambayo wangeipata Chadema kuandamana, and wewe na mimi ni vyema tukapima jambo hilo katika mizani hiyo
 
Lema anatakiwa Ajenge hoja kwa kusema Pinda kadanganya, bali aseme yeye aliuliza kutaka kujua ni nini kinafanyika iwapo mtu mkubwa kama Waziri Mkuu anadanganya!. just simple like that
 
Lema anatakiwa Ajenge hoja kwa kueleza kwamba "yeye Hajasema Pinda kadanganya", bali aliuliza ili kutaka kujua ni nini kinafanyika iwapo mtu mkubwa kama Waziri Mkuu anadanganya!. just simple like that
 
Pinda has never lied, and never will!!

wewe pinda.. saa hizi wenzako wamo ndani mjengoni....lakini wewe unahangaika humu JF kuutetea uongo wako....umeshaambiwa wewe ni muongo jitetee humo bungeni na si hapa JF
 
goood enough! sasa shirikiana na lema kukusanya ushahidi ili february 14 muwasilishe ushahid wa ukweli,
 
Mh. Pinda ungama kwa uongo uliotoa.... usiogope kuungama kwenye kanisa lako kwanza ...kwani sasa hivi kanisa katoliki limeruhusu kuungama kwa kutumia iPhone..... halafu njoo JF ungama kwa kutumia Id ya jina lako kamili .... hatuwezi kupotoshwa penye ukweli
 
Alilofanya Mzee pinda halishangazi sana kwa sababuu ametumia principal ya vita "IF YOU CAN'T FIGHT THEM JOIN THEM" Wakati alipokuwa mtoto wa mkulima alijitahidi kuwa mmkweli hadi analia bungeni kwa sababu ya machungu, Lakini sasa sio yule tena, ameshkuwa upande wao zamaniiiiii!!! sijui labda MGAO.
Kwanza waliokufa watu watatu mmoja ni Mkenya, ye katuambia Watanzania watutu, Je huo ni oungo au ukweli?? Kunahitaji shule????

Jambo linging linalotukera ni kuwa Viongozii wakuu wanajibu mambo kwa jazba. Mr. Lema Mbunge wa A Town aliomba muongozo kutoka kwa spika ENDAPO KAMA" kiongozi mkubwa akidanganya bunge na watanzania muongozo unasema aje?"! Jamani hii ni statement ya kisheria, namuomba TINDU LISU atusaidie. Je alimwita muongo?? Je Spika alichotakiwa kufanya ni nini?? Alitakiwa kutoa muongozo na statement hiyo ni condional statement, "IF" Kama amedanganya hatua ni A,B,C, kama hakudanya hatua ni D, E, F. Na sio kutoa majibu kwa hasira. wanatutisha watizamaji wa hili bunge tukufu!!

PEOPLES POWER
 
Alilofanya Mzee pinda halishangazi sana kwa sababuu ametumia principal ya vita "IF YOU CAN'T FIGHT THEM JOIN THEM" Wakati alipokuwa mtoto wa mkulima alijitahidi kuwa mmkweli hadi analia bungeni kwa sababu ya machungu, Lakini sasa sio yule tena, ameshkuwa upande wao zamaniiiiii!!! sijui labda MGAO.
Kwanza waliokufa watu watatu mmoja ni Mkenya, ye katuambia Watanzania watutu, Je huo ni oungo au ukweli?? Kunahitaji shule????

Jambo linging linalotukera ni kuwa Viongozii wakuu wanajibu mambo kwa jazba. Mr. Lema Mbunge wa A Town aliomba muongozo kutoka kwa spika ENDAPO KAMA" kiongozi mkubwa akidanganya bunge na watanzania muongozo unasema aje?"! Jamani hii ni statement ya kisheria, namuomba TINDU LISU atusaidie. Je alimwita muongo?? Je Spika alichotakiwa kufanya ni nini?? Alitakiwa kutoa muongozo na statement hiyo ni condional statement, "IF" Kama amedanganya hatua ni A,B,C, kama hakudanya hatua ni D, E, F. Na sio kutoa majibu kwa hasira. wanatutisha watizamaji wa hili bunge tukufu!!

PEOPLES POWER


asante... lakini wewe ni pacha wa Mbunge Lema au ....?
 
Mi sioni ishu hapa kama CHADEMA wana ishu wangeanza na ile taarifa ya IGP iliyochapishwa kwenye magazeti kuhusiana na vurugu za Arusha. Kama hizo nazo ni za uongo basi serikali yote itakuwa imeongopa na hapo sasa ithibitishwe kwamba vyombo vya dola vya serikali vimeongea uongo na iwekwe njia ya kuviadhibu!

Otherwise CDM itaonekana ina agenda binafsi tu na PM... thats what i'm seeing here.

DMussa ,

you have all the wrights to think and state what you have stated,however i didn't write this tread kumshawishi au kumfanya mtu yeyote akubali nililosema but i wanted the Community via Jf to understand something,However i my self i was leaded with the information attached bellow.

View attachment Taarifa ya Maandamano - kiambatanisho no. 3-1.pdf
Concerning IGP,he is a great lier,natamani kama angejiunga Jf akatoa ufafanuzi i my self i talked to him on the same day. Kwakuwa Chadema always sio watu wa kukurupuka maadalizi ya msingi yanafanywa na ukweli utawekwa wazi.
Naomba tu kama kuna mtu anataarifa kimaandisha ya kuzuia maandamano haya aitoe na atueleze alimkabidhi nani kwa mda gani.

DMussa,hata kama wataendelea kutunyima haki zetu kwa wao kutumia ubabe siku itafika na Mungu atajidhihirisha kwa watu wake.
 
Rais - kila kitu hajui, waziri mkuu - muongo.

Waziri je , itakuwaje ?? Nchi inauliwa hivi hiv yaaaniiii!!!
 
Nimesoma kwa makini barua na kilichotokea. Kwa kweli inasikitisha sana. Halafu viongozi walafi wataendelea kuongoza kwa mabavu mpaka lini? Huu ni ukandamizaaji wa hali ya juu wa Demokrasia. CCM mnataka kutupeleka wapi?
 
kumbe pinda nae anasema uongo! jamani washamteka mafisad

Pinda ni muhuni asiyestahili heshima. Nawashangaa watu wanaomuita mtoto wa mkulima. Kajamaa kabaya sana kale usikaone kanalialia ovyo. Niliacha kukaheshimu baada ya mkutano wa Bunge uliosababisha Lowasa na wengine kujiuzulu. Pinda alienda moja kwa moja mpaka Igunga na katika mkutano pale ambao ulihudhuriwa na mbunge wa Igunga Rostam Aziz, Pinda alisema na ninamnukuu, "ROSTAM NI MTU MUADILIFU SANA, MAMBO YA BUNGENI NI MENGI SANA, NAWASHAURI MUYAACHE HUKO HUKO". Kauli kama hii hawezi kuitoa mtu muadilifu. Ni huyu huyu Pinda anayesadikika kushurutisha matokeo ya ubunge na urais katika mkoa Rukwa kuchakachuliwa. Anajiita mkatoliki lakini yeye alikuwa namba moja kuutukana ukatoliki kwa kumfananisha kikwete na Mungu, wabunge , Yesu na madiwani wa CCM Roho Mtakatifu. Huyu jamaa ni kinyaa na matapishi. Na hakuna kinachoniudhi kama anavyojifanya mwema wakati ni adui wa haki. Si afadhali Lowasa alikuwa akichakachua waziwazi? Sasa huyu nungunungu kazi ya uwaziri nkuu hawezi, na ukweli hana. KAzi kulia lia tu kama yule feki Dokta anayejiita rais anavyo cheka chekaovyo wakati watanzania wanaangamia na umaskini. Aisee naichukia CCM we acha tu
 
Back
Top Bottom