Waziri Mkuu aainisha utoaji taarifa rasmi za coronavirus

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,331
24,240
March 21, 2020
MAJALIWA - Wapotosha kuhusu Corona kukiona
Published on 21 Mar 2020


Waziri mkuu, Kassim Majaliwa ameonya juu ya upotoshwaji na utoaji holela wa taarifa kuhusu ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababisha na virusi vya corona (COVID 19) unaofanywa na watu mbalimbali nchini.

Amesema kuanzia sasa taarifa hizo zitatolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na ikilazimika zitatolewa na Waziri Mkuu na ikilazimika sana zitatolewa na viongozi wakuu wa nchi ili kuepusha mikanganyiko.

Aidha Waziri Mkuu ameiagiza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ifuatilie watu wote wanaofanya upotoshaji kwa kupitia mitandao ya kijamii ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

“Watu wote wanaopotosha umma na kuleta taharuki kuhusu ugonjwa wa corona badala ya kuelimisha namna ya kujikinga, wafuatiliwe na kuchukuliwa hatua,” amesisitiza.

Source: Azam TV

More info :

Baada ya mkanganyiko wa utoaji taarifa kuhusu gonjwa la SARS -:Covid - 19 coronavirus na tamko la waziri kivuli wa Afya kuhusu mkanganyiko huo.

Mh. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ametoa utaratibu mpya ya namna ya kutangaza uwepo wa coronavirus kuwa utaratibiwa moja kwa moja na wizara ya Afya na si vinginevyo.

Waziri Mkuu Mh. Majaliwa anaongeza kuwa serikali imeamua kuweka utaratibu huu ili kuondoa hali ilivyo sasa ambapo taarifa zinarushwa na vyanzo vingi na kuleta mtafaruku na hofu bila uthibitisho wa wataalamu wa maabara kuu iliyo chini ya Wizara ya Afya.

Waziri Mkuu amesema kunapogundulika uwepo wa coronavirus ktk eneo lolote baada ya uthibitisho kwa vipimo, taarifa hizo kupitia waganga wakuu wa mikoa kwa kushirikiana na kamati zao za ulinzi za mikoa zilizo chini wa wakuu wa Mikoa / Wilaya, zipelekwe moja kwa moja Mganga Mkuu wa Serikali wa wizara ya Afya na waziri wa Afya wizara hiyo ndiyo amekasimiwa rasmi kazi ya kutangaza uwepo wa coronavirus.

IMG-20200321-WA0043.jpg
IMG-20200321-WA0044.jpg
 
Afadhali maana habari za kila mtu kuwa msemaji zinakanganya
March 21, 2020



Baada ya mkanganyiko wa utoaji taarifa kuhusu gonjwa la SARS -:Covid - 19 coronavirus na tamko la waziri kivuli wa Afya kuhusu mkanganyiko huo.

Mh. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ametoa utaratibu mpya ya namna ya kutangaza uwepo wa coronavirus kuwa utaratibiwa moja kwa moja na wizara ya Afya na si vinginevyo.

Waziri Mkuu amesema kunapogundulika uwepo wa coronavirus ktk eneo lolote baada ya uthibitisho kwa vipimo, taarifa hizo vipelekwe moja kwa moja wizara ya Afya na wizara hiyo ndiyo imekasimiwa rasmi kazi ya kutangaza uwepo wa coronavirus.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kabisa, maana sasa kila mtu ni msemaji wa coronavirus , sanitizer na vikohozi.

Serikali ijenge utaratibu Waziri wa Afya kila siku saa kumi na mbili jioni awe anatoa taarifa kuhusu idadi ya wagonjwa waliogundulika kuwa na maambukizi, maeneo na ushauri juu ya jinsi ya wananchi kunawa mikono mara kwa mara na sabuni na kuepuka misongamano.
 
March 21, 2020



Baada ya mkanganyiko wa utoaji taarifa kuhusu gonjwa la SARS -:Covid - 19 coronavirus na tamko la waziri kivuli wa Afya kuhusu mkanganyiko huo.

Mh. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ametoa utaratibu mpya ya namna ya kutangaza uwepo wa coronavirus kuwa utaratibiwa moja kwa moja na wizara ya Afya na si vinginevyo.

Waziri Mkuu Mh. Majaliwa anaongeza kuwa serikali imeamua kuweka utaratibu huu ili kuondoa hali ilivyo sasa ambapo taarifa zinarushwa na vyanzo vingi na kuleta mtafaruku na hofu bila uthibitisho wa wataalamu wa maabara kuu iliyo chini ya Wizara ya Afya.

Waziri Mkuu amesema kunapogundulika uwepo wa coronavirus ktk eneo lolote baada ya uthibitisho kwa vipimo, taarifa hizo vipelekwe moja kwa moja wizara ya Afya na wizara hiyo ndiyo imekasimiwa rasmi kazi ya kutangaza uwepo wa

Genge la Bashungwa ambao sio wataalam wa Afya wamefanya nini leo
 
March 21, 2020
MAJALIWA - Wapotosha kuhusu Corona kukiona
Published on 21 Mar 2020

Waziri mkuu, Kassim Majaliwa ameonya juu ya upotoshwaji na utoaji holela wa taarifa kuhusu ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababisha na virusi vya corona (COVID 19) unaofanywa na watu mbalimbali nchini.

Amesema kuanzia sasa taarifa hizo zitatolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na ikilazimika zitatolewa na Waziri Mkuu na ikilazimika sana zitatolewa na viongozi wakuu wa nchi ili kuepusha mikanganyiko.

Aidha Waziri Mkuu ameiagiza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ifuatilie watu wote wanaofanya upotoshaji kwa kupitia mitandao ya kijamii ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

“Watu wote wanaopotosha umma na kuleta taharuki kuhusu ugonjwa wa corona badala ya kuelimisha namna ya kujikinga, wafuatiliwe na kuchukuliwa hatua,” amesisitiza.

Source : Azam TV

More info :

Baada ya mkanganyiko wa utoaji taarifa kuhusu gonjwa la SARS -:Covid - 19 coronavirus na tamko la waziri kivuli wa Afya kuhusu mkanganyiko huo.

Mh. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ametoa utaratibu mpya ya namna ya kutangaza uwepo wa coronavirus kuwa utaratibiwa moja kwa moja na wizara ya Afya na si vinginevyo.

Waziri Mkuu Mh. Majaliwa anaongeza kuwa serikali imeamua kuweka utaratibu huu ili kuondoa hali ilivyo sasa ambapo taarifa zinarushwa na vyanzo vingi na kuleta mtafaruku na hofu bila uthibitisho wa wataalamu wa maabara kuu iliyo chini ya Wizara ya Afya.

Waziri Mkuu amesema kunapogundulika uwepo wa coronavirus ktk eneo lolote baada ya uthibitisho kwa vipimo, taarifa hizo kupitia waganga wakuu wa mikoa kwa kushirikiana na kamati zao za ulinzi za mikoa zilizo chini wa wakuu wa Mikoa / Wilaya, zipelekwe moja kwa moja Mganga Mkuu wa Serikali wa wizara ya Afya na waziri wa Afya wizara hiyo ndiyo amekasimiwa rasmi kazi ya kutangaza uwepo wa coronavirus.

Waione akina Steve Nyerere na wenzake wawili!
 
Mpaka kina Bashite nao walikuwa wasemaji!
Msemaji mkuu kitaifa ni Rais wa JMT
Wasemaji wakuu wa kisekta ni mawaziri
Wasemaji wakuu wa kiutendaji ni makatibu wakuu
Wasemaji wakuu wa Taasisi ni wakuu wa Taasisi
Wasemaji wakuu wa territories ni wakuu wa mikoa kwa mikoa na wakuu wa wilaya kwa wilaya.
Hivyo wakuu wa mikoa ya Arusha na DSM had all the rights kuongelea Corona mikoa yao.
The right to information inatoa fursa kwa kila mtu kuwa msemaji wa eneo lake.
P
 
Msemaji mkuu kitaifa ni Rais wa JMT
Wasemaji wakuu wa kisekta ni mawaziri
Wasemaji wakuu wa kiutendaji ni makatibu wakuu
Wasemaji wakuu wa Taasisi ni wakuu wa Taasisi
Wasemaji wakuu wa territories ni wakuu wa mikoa kwa mikoa na wakuu wa wilaya kwa wilaya.
Hivyo wakuu wa mikoa ya Arusha na DSM had all the rights kuongelea Corona mikoa yao.
The right to information inatoa fursa kwa kila mtu kuwa msemaji wa eneo lake.
P
Kuhusu taarifa za corona umeshaambiwa hakuna cha mkuu wa mkoa wala wilaya, msemaji ni Waziri wa Afya au Waziri Mkuu au Makamu wa Rais au Rais mwenyewe.
 
March 21, 2020
MAJALIWA - Wapotosha kuhusu Corona kukiona
Published on 21 Mar 2020


Waziri mkuu, Kassim Majaliwa ameonya juu ya upotoshwaji na utoaji holela wa taarifa kuhusu ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababisha na virusi vya corona (COVID 19) unaofanywa na watu mbalimbali nchini.

Amesema kuanzia sasa taarifa hizo zitatolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na ikilazimika zitatolewa na Waziri Mkuu na ikilazimika sana zitatolewa na viongozi wakuu wa nchi ili kuepusha mikanganyiko.

Aidha Waziri Mkuu ameiagiza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ifuatilie watu wote wanaofanya upotoshaji kwa kupitia mitandao ya kijamii ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

“Watu wote wanaopotosha umma na kuleta taharuki kuhusu ugonjwa wa corona badala ya kuelimisha namna ya kujikinga, wafuatiliwe na kuchukuliwa hatua,” amesisitiza.

Source: Azam TV

More info :

Baada ya mkanganyiko wa utoaji taarifa kuhusu gonjwa la SARS -:Covid - 19 coronavirus na tamko la waziri kivuli wa Afya kuhusu mkanganyiko huo.

Mh. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ametoa utaratibu mpya ya namna ya kutangaza uwepo wa coronavirus kuwa utaratibiwa moja kwa moja na wizara ya Afya na si vinginevyo.

Waziri Mkuu Mh. Majaliwa anaongeza kuwa serikali imeamua kuweka utaratibu huu ili kuondoa hali ilivyo sasa ambapo taarifa zinarushwa na vyanzo vingi na kuleta mtafaruku na hofu bila uthibitisho wa wataalamu wa maabara kuu iliyo chini ya Wizara ya Afya.

Waziri Mkuu amesema kunapogundulika uwepo wa coronavirus ktk eneo lolote baada ya uthibitisho kwa vipimo, taarifa hizo kupitia waganga wakuu wa mikoa kwa kushirikiana na kamati zao za ulinzi za mikoa zilizo chini wa wakuu wa Mikoa / Wilaya, zipelekwe moja kwa moja Mganga Mkuu wa Serikali wa wizara ya Afya na waziri wa Afya wizara hiyo ndiyo amekasimiwa rasmi kazi ya kutangaza uwepo wa coronavirus.

Hii imekaa sawa.ili nchi Kama nchi iweze kuongeza lugha moja.
 
Back
Top Bottom