Waziri Makamba: Ninatukanwa sana lakini nitalipa kisasi kwa matokeo

Kulwa Jilala

JF-Expert Member
Sep 6, 2022
3,510
7,755
"Siku moja hapa umeme umekatika Bungeni, kumetokea hitilafu. Ghafla bwana “fukuza Waziri, fukuza TANESCO”. Kumbe kuja kuchunguza waala!.

Umeme umekatika kwenye uwanja wa mpira, “fukuza Waziri, fukuza TANESCO”. Kumbe ni mambo mengine. Jamani, sio wakati wote ni TANESCO, sio wakati wote ni Wizara.

Sisi tutachukua wajibu wetu pale inapotokea” Waziri wa Nishati, January Makamba.

Haya maneno yanatuongezea hamu na hamasa ya kupata matokeo. Sisi hamasa yetu ni imani ya Mheshimiwa Rais kwetu, hamasa yetu ni matokeo ya kazi yetu kwa uhai wa chama chetu.

Hamasa nyingine ni kuwasaidia Watanzania kwa majukumu tuliyopewa. Lakini hamasa ya mwisho ni maneno haya, mtu akikusema wewe hufai maana yake unajitahidi ili uonekane unafaa. Kwa hiyo haya maneno yanatusaidia. Lakini pia haya maneno yanatusaidia kwa sababu yanawaamsha wanaotupenda na wanaotutakia heri ili watuombee dua na sala.”- Waziri January Makamba

“Maneno haya yanatusaidia kwa sababu yanatufundisha ukomavu, yanatufundisha kuwa na subra, yanatufundisha kuwa na uvumilivu na yanatujenga kuwa viongozi bora zaidi. Sisi tumesema waendelee kwa sababu yanatusaidi. Sisi kisasi chetu ni MATOKEO. Hatutabishana, hatutatupa maneno, hatutajitetea, tutalipa kisasi kwa matokeo” Waziri wa Nishati, January Makamba.
 
huyu jamaa simkubali kama kiongozi kwa namna yoyote ile. huwenda hata kama angepewa ubalozi wa nyumba kumi mtaani kwetu bado nisinge mkubali.
Nafsi yangu inaona ni kama mtu aliyebebwabebwa tu kwa nguvu kubwa ya mzazi wake napata tabu kukubali kama anaweza kuwa na maarifa ya kutosha katika taifa hili lenye watu zaidi ya milioni 60.
 
dude has never fitted anywhere. bora angebaki kuwa muandika speech za Kikwete, at least he was good at that.
Wewe una chuki zako tu za hovyo. Makamba ni waziri mzuri sana na hajawahi kushindwa katika wizara yoyote. Kumbuka yeye ndie aliyefanikisha suala la kuondoa mifuko ya plastiki bila hata kumuumiza au kumfunga yoyote. Wewe maumivu yako ni kwa Kalemani kuondolewa pale na si vinginevyo.
 
jambazi kubwa, kisasi pekee atakacholipiza ni kuiba pesa zaidi.

we jitu gani kila linapokwenda linachukiwa, anadhani ni coincidence tu?? kajamaa kanajifanya kajanja sana lakini tamaa zake zinamfanya avurunde.
Kwenye wizara ya Mazingira alihakikisha hakuna mifuko ya plastiki na kazi nyingi tu za alama. Hapa kwenye nishati the fact kwamba as a minister of wazungu wamekubali kuweka $40B kwenye LNG Lindi, mradi mkubwa katika historia ya nchi.

Haya mradi mkubwa wa solar East Africa unaanza June, haya biggest investment in grid ever inafanyika sasa hivi. Bado vijiji 2000 tu nchi nzima kufikiwa na umeme.

Sooo talk your shit. But its probably hate driven.

😂😂



Soo
 
Wakati wa Utawala wa Mkapa hakuna kiongozi aliekuwa anachukiwa kama Sumaye....kila lawama Sumaye..
Ufisadi ukatungwa anamiliki shirika la ndege n.k...

Kumbe yote yalikuwa uwongo....mtupu..alibatizwa jina Zero...Kwa chuki tu...

Hatari sana
 
Kwenye wizara ya Mazingira alihakikisha hakuna mifuko ya plastiki na kazi nyingi tu za alama. Hapa kwenye nishati the fact kwamba as a minister of wazungu wamekubali kuweka $40B kwenye LNG Lindi, mradi mkubwa katika historia ya nchi.

Haya mradi mkubwa wa solar East Africa unaanza June, haya biggest investment in grid ever inafanyika sasa hivi. Bado vijiji 2000 tu nchi nzima kufikiwa na umeme.

Sooo talk your shit. But its probably hate driven.

😂😂



Soo
ok
 
huyu jamaa simkubali kama kiongozi kwa namna yoyote ile. huwenda hata kama angepewa ubalozi wa nyumba kumi mtaani kwetu bado nisinge mkubali.
Nafsi yangu inaona ni kama mtu aliyebebwabebwa tu kwa nguvu kubwa ya mzazi wake napata tabu kukubali kama anaweza kuwa na maarifa ya kutosha katika taifa hili lenye watu zaidi ya milioni 60.
Kwenye maisha ya kawaida kila mtu anatamani kubebwa,kila mtu anatamani kufika sehemu fulani ya mafanikio!!

Swali langu Kwako,Je ungepata fursa ya kupata mtu wa kukubeba ungekataa?

Hata mimi,natamani nipate mtu aweze kunibeba lakini sina?,tuache wivu jamani kila mtu na bahati yake!!
 
Halafu yeye anautaka urais wa nchi hii
huyu jamaa simkubali kama kiongozi kwa namna yoyote ile. huwenda hata kama angepewa ubalozi wa nyumba kumi mtaani kwetu bado nisinge mkubali.
Nafsi yangu inaona ni kama mtu aliyebebwabebwa tu kwa nguvu kubwa ya mzazi wake napata tabu kukubali kama anaweza kuwa na maarifa ya kutosha katika taifa hili lenye watu zaidi ya milioni 60.
 
Kwenye maisha ya kawaida kila mtu anatamani kubebwa,kila mtu anatamani kufika sehemu fulani ya mafanikio!!

Swali langu Kwako,Je ungepata fursa ya kupata mtu wa kukubeba ungekataa?

Hata mimi,natamani nipate mtu aweze kunibeba lakini sina?,tuache wivu jamani kila mtu na bahati yake!!
Mhn! kwa kweli siwezi kumwonea wivu kwa mtu kama huyu kwa lipi hasa!? kwa bahati mbaya vingine haviandikiki tu hapa
 
"Siku moja hapa umeme umekatika Bungeni, kumetokea hitilafu. Ghafla bwana “fukuza Waziri, fukuza TANESCO”. Kumbe kuja kuchunguza waala!.

Umeme umekatika kwenye uwanja wa mpira, “fukuza Waziri, fukuza TANESCO”. Kumbe ni mambo mengine. Jamani, sio wakati wote ni TANESCO, sio wakati wote ni Wizara.

Sisi tutachukua wajibu wetu pale inapotokea” Waziri wa Nishati, January Makamba.

Haya maneno yanatuongezea hamu na hamasa ya kupata matokeo. Sisi hamasa yetu ni imani ya Mheshimiwa Rais kwetu, hamasa yetu ni matokeo ya kazi yetu kwa uhai wa chama chetu.

Hamasa nyingine ni kuwasaidia Watanzania kwa majukumu tuliyopewa. Lakini hamasa ya mwisho ni maneno haya, mtu akikusema wewe hufai maana yake unajitahidi ili uonekane unafaa. Kwa hiyo haya maneno yanatusaidia. Lakini pia haya maneno yanatusaidia kwa sababu yanawaamsha wanaotupenda na wanaotutakia heri ili watuombee dua na sala.”- Waziri January Makamba

“Maneno haya yanatusaidia kwa sababu yanatufundisha ukomavu, yanatufundisha kuwa na subra, yanatufundisha kuwa na uvumilivu na yanatujenga kuwa viongozi bora zaidi. Sisi tumesema waendelee kwa sababu yanatusaidi. Sisi kisasi chetu ni MATOKEO. Hatutabishana, hatutatupa maneno, hatutajitetea, tutalipa kisasi kwa matokeo” Waziri wa Nishati, January Makamba.
"Keep up the good work " January makamba lazima tuseme ili tuwaongezee speed kidogo ya kufanya kazi
 
Back
Top Bottom