Habari za muda huu wadau,kama kichwa cha habari kinavyosema,nimefanya wayaring ,nikaenda kuchukua fomu ya maombi ya awali ya kupata umeme kama wenyewe wanavyoita.
Fomu nilichukua tarehe 2.1.2013.na nikarudisha tarehe 7.1.2013.wakaniambia tupe namba ya simu tutakupigia ili savea aje.
Cha ajabu hadi leo.sijapigiwa simu na wala savea hajaja,sasa TANESCO kufanyiwa savey tu mwaka sasa je kuwekewa umeme si utachukua miaka kadhaa?
BADRA MASOUD,meneja uhusiano wa tanesco najua ni member humu aje atueleze kuhusu hawa masavea wa shirika.
Nilijaribu kuwauliza watu wengine wakaniambia unatakiwa umtafute pale ofisini na umpe angalau elfu thelethini ili akufanyie mambo yako haraka.
Sasa hawa si wanalipwa? Kwa nini tuwape tena hongo?
TANESCO jirekebisheni,ndio maana sasas hivi watanzania wengi wamehamia kwenye solar power kwa sababu ya usumbufu toka kwenu.